Home » » PICHA NA HABARI: CHADEMA KUPITIA MH. TUNDU LISSU YAIBUKA KIDEDEA KESI YA UBUNGE SINGIDA MASHARIKI.

PICHA NA HABARI: CHADEMA KUPITIA MH. TUNDU LISSU YAIBUKA KIDEDEA KESI YA UBUNGE SINGIDA MASHARIKI.


Wakili wa waleta maombi Wanaccm Godfrey Wasonga akitafakari kwa hisia kali muda mfupi kabla ya kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ubunge Tundu Lissu hayajatangazwa.

Mbunge wa jimbo la Singida mashariki CHADEMA),Tundu Lissu,muda mfupi baada ya mahakama kuu kutupilia mbali maombi yaliyotolewa na Shaban Selema na Pascal Halu wa CCM,kupinga matokeo yaliyompa ushindi wa ubunge.
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki (CHADEMA) Tundu Lissu akifutwa machozi na mke wake wakati wakitoka nje ya mahakama baada ya mahakama kuu kutangaza kuwa ushindi wake huo,ni halali.
Baadhi wa watu waliohudhuria kusikiliza kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Tundu kuwa mbunge muda mfupi baada ya maamuzi hayo kutolewa.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki (CHADEMA)Tundu Lissu imeigaragaraza vibaya CCM baada ya mahakama kuu kutupilia mbali hoja 11 zilizowasilishwa na waleta maombi wawili wanachama wa CCM za kutaka kutengua ushindi wake wa ubunge kwa madai kuwa, alikiuka sheria na taratibu za uchaguzi na kusababisha uchaguzi huo kutokuwa huru na wa haki.
Shabani Selema na Pascal Halu wote wanachama wa CCM na wakazi wa kijiji cha Makiungu tarafa ya Mungaa jimbo la Singida Mashariki, walifungua kesi ya kupinga matokeoa yaliyompa ushindi Tundu kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Jaji Mosses Mzuna wa makahama kuu Moshi mjini mkoa wa Kilimanjaro, katika kutoa hukumu hiyo, amesema ushahidi uliotolewa na upande wa waleta maombi, umeshindwa kuthibitisha bila kuacha shaka yo yote kuwa, mlalamikiwa wa kwanza, wa pili mwanasheria mkuu wa serikali na wa tatu msimamizi wa uchaguzi, kuwa walivunja/kiuka  sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi na kusababisha uchaguzi huo kutokuwa huru na wa haki.
Akitoa maamuzi ya makahama, amesema kuwa katika hoja zote 11 zilizoletwa na waleta maombi hao, ushahidi wote ni wa kuhisi, kusikia  na kushuku, ambao hauna uhalisia wa mambo yaliyowasilishwa.
Jaji Mzuna amesema kuwa mahakama yo yote haiwezi kutegua matokeo ya uchaguzi kwa kuambiwa maneno matupu bila ya maneno husika kuthibishwa kwa ‘document’ husika.
Amesema ushahidi wa upande wa walalamikaji pia umekuwa ni kama kinyonga, mara kwa mara ulikuwa ukukigeuka geuka.
Akifafanua zaidi, Mzuna ametaja  baadhi ya hoja ambazo zililetwa na waleta maombi kuwa ni mlalamikiwa Tundu kuandaa barua tano zinazofanana kwa mawakala wa CUF, TLP, AAPT Maendeleo, NCCR -Magezui na CHADEMA, kwa lengo la kujinufaisha katika zoezi la uchaguzi mkuu.
Ametaja hoja nyingine kuwa Tundu aliwapa chakula mawakala wa chama chake na wa vyama vingine isipokuwa wa chama cha CCM, kitendo ambacho kiliashiria ni hongo ili mawakala wasiokuwa wa chama chake nao wampigie kura.
HABARI KWA HISANI YA MO BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa