Home » » MISS SINGIDA 2012 KUJULIKANA JUNI MOSI.

MISS SINGIDA 2012 KUJULIKANA JUNI MOSI.


Mratibu wa Miss Singida mkoani Singida Aunt Borah Lemmy akizungumza na mwandishi wa habari wa MO BLOG (hayupo kwenye picha) juu ya maandalizi ya shindano la kumsaka Miss Singida 2012.
Miss Singida 2011 Lizpbeth Pertti (katikati) na kulia ni mshindi wa pili Nyange Warioba na kushoto ni mshindi wa tatu Esther Gidion. (Picha zote na Nathaniel Limu).


Na Nathaniel Limu.
Shindano la kumsaka Miss Singida 2012 Redds, linatarajiwa kufanyika Juni Mosi mwaka huu kwenye ukumbi wa mikutano wa Aque vitae mjini Singida.
Akizungumza na mwandishi wa habari wa MO BLOG ofisini kwake, Mratibu wa Miss Tanzania mkoani Singida Aunt Borah Lemmy, amesema maandalizi yote muhimu yanaendelea vizuri ikiwemo warembo kuendelea kujisajili.
Amesema warembo mbali mbali waliopania kuwania nafasi hiyo, wanaendelea kuchukua fomu ambazo zinatolewa bure.
Aunt Borah amesema kwa sasa hawezi kutaja majina ya warembo ambao wamejisajili, lakini atafanya hivyo muda ukifika.
 Aidha ametoa wito kuwa warembo ambao watajikagua vizuri na kubaini kuwa wana sifa zote zinazohitajika, wafike kwa wingi kwenye salon yake kuchukua fomu na kuzijaja.
Mtaribu huyo amesema anatarajia kupata washiriki wasiopungua watatu kutoka kila wilaya ya Manyoni na Iramba.
Aunt Borah ameongeza kuwa shindnao la mwaka huu, litapambwa na burudani kabambe itakayotolewa na malkia wa mipasho nchini Bi.Khadija Kopa.
Aunt Borah huku kitabasamu pia amesema Katibu wa uenezi na itikadi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Mnauye, atakuwa  mgeni rasmi kwenye shindano hilo .
Mratibu huyo alimeja viingilio kuwa vitakuwa  shilingi 10,000 kwa viti vya kawaida na 20,000 kwa viti vya VIP.
Alisema pamoja na shindano hilo kudhaminiwa na Redds, pia litadhaminiwa na kampuni ya Mohammed Enterprises Ltd ambayo Mkurugenzi wake Mkuu ni Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji.
Miss Singida wa mwaka jana (2011) Lizpbeth Pertti kutoka Itigi wilayani Manyoni hakuweza kushiriki miss kanda ya kati kwa kile akilichodaiwa ni kuwa na mimba. 
Kwa hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa