DEWJI ATOA MISAADA KATIKA JIMBO LA SINGIDA


E83A0131
Picha juu na chini ni Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mh. Mohammed Gullam Dewji akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kituo cha mabasi cha zamani mjini Singida.
E83A0112
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji kuzungumza na wananchi wa jimbo lake.
E83A0094
Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mh. Mohammed Gullam Dewji, akiwa anasalimiana na Wana CCM na wananchi wa Singida mjini kwenye kituo cha mabasi cha zamani mjini Singida.


Na Nathaniel Limu.
Mbunge wa Singida mjini (CCM) Mh. Mohammed Gullam Dewji amemwaga misaada mbalimbali ikiwemo kuwaongezea mitaji wauza kahawa chungu, ambayo haijawahi kutolewa jimboni humo na mbunge au mfadhili yeyote kwa wakati mmoja, kabla na baada ya Tanzania kupata uhuru.
Misaada hiyo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 87.9, ni pamoja na mabati 100 na mifuko ya saruji 100, kwa kila shule 17 za sekondari jimboni humo.
Misaada mingine ni vyereheni viwili kwa kila kata 19 na cherehani moja kwa kila tawi la CCM jimboni humo.

Pia vikundi 16 vya wajasiriamali vikiwemo vya kung’arisha viatu, mafundi baiskeli, wapiga debe wa vituo vya mabasi, wasukuma matoroli, wakereketwa wa mashina ya CCM, watengeneza viatu vya kienyeji na baba, mama lishe, kila kimoja kimeongezewa mtaji wa shilingi 500,000 taslimu.

Vifaa hivyo na mitaji ya biashara, vimetolewa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida.

Akizungumza kwenye mkutano huo wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya wana-CCM na wananchi kwa ujumla, Mh. Dewji amesema msaada huo ni mwendelezo wa misaada yake anayoitoa kwa ajili ya kuiunga mkono serikali katika kuwatumikia wananchi.

Amesema pia kuwa misaada hiyo ni sehemu yake ya utekelezaji wa ilani ya CCM katika kuwatumikia wananchi wa jimbo la Singida mjini.

Amesema “Tunatakiwa tujitume usiku na mchana, ili tuhakikishe kila tuliyoyaahidi kwenye ilani yetu, yote tumeyakamilisha, vinginevyo wananchi hawatatuelewa. Wananchi wanahitaji utimilifu wa ahadi na sio uhodari wa kujieleza kwenye majukwaa”.

Katika hatua nyingine, Mh. Dewji ametumia fursa hiyo kuwaomba viongozi na watendaji kuendelea na moyo safi wa kuwatumikia wananchi bila kuchoka.
Amesema pia wawe waaminifu na waadilifu kwa wananchi na waongozwe kwa dhamira iliyo njema, yenye uzalendo wa kuipenda nchi yetu na watu wake.

Mbunge Dewji amesema “Tuendelee kuhubiri amani na utulivu kwenye majukwaa, wakati wote tuwaelekeze wananchi kwenye kujiletea maendeleo endelevu ya wakati huu na wakati ujao”.

Kesi ya diwani wa kata ya Mungaa mkoani Singida kupitia tiketi ya CHADEMA ya kukatakata Ng’ombe sita kuunguruma kesho.


DSC01222

Diwani wa CHADEMA kata ya Mungaa jimbo la Singida Mashariki, Matheo Alex (wa pili kushoto aliyenyanyua mkono juu) akiwa katika chumba cha mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida akisubiri kusomewa shitaka lake la kukata kata ng’ombe sita mali ya Mary John mkazi wa kijiji cha Minyinga kata ya Mungaa.Wa pili kulia ni mtoto wa diwani Alex, Faraja na wa pili kushoto Bahati Sumbe (mwenye jacketi la njano) wameunganishwa kwenye kesi moja na diwani Alex.
Na Nathaniel Limu.
Kesi ya kukata kata ng’ombe sita inayomkabili diwani wa kata ya Mungaa kupitia tiketi ya CHADEMA, jimbo la Singida Mashariki Matheo Alex na washitakiwa wenzake wawili, inatarajiwa kuunguruma kesho asubuhi kwenye mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida.
Washitakiwa wengine ni mtoto wa diwani huyo Faraja Matheo na mwingine ni mjomba wa diwani huyo Bahati Sumbe.
Ng’ombe hao waliokatwa katwa ni mali ya Mary John mkazi wa kijiji cha Minyinga kata ya Mungaa jimbo la Singida mashariki na wana thamani ya zaidi ya shilingi milioni 3.5 milioni.
Mei 17 mwaka huu wakati washitakiwa hao walipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza, mwendesha mashitaka Mussa Chemu amedai kuwa mnamo Mei 13 mwaka huu saa 5.00 asubuhi huko katika kijiji cha Minyinga, kwa makusudi washitakiwa wote kwa pamoja walishirikiana kukata kata ng’ombe sita mali ya Mary John.
Washitakiwa wamekana shitaka hilo na wako nje kwa dhamana ya kila mmoja amedhaminiwa na watu wawili ambao kila mmoja ametoa ahadi ya dhamana ya shilingi milioni tano.
Washitakiwa hao wanatetewa na wakili maarufu Tundu Lissu ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Singida Mashariki.
 Chanzo Mo Blog

TANGAZO LA MAUZO YA NYUMBA ZA MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI WA UMMA (PSPF)


MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI WA UMMA
(PSPF)
 


MAUZO YA NYUMBA ZA PSPF
Mfuko unapenda kuwataarifu wananchi wote kwamba inauza nyumba zilizojengwa na Mfuko katika mikoa ya Dar es Salaam- Ilala (Buyuni), Morogoro (Lukobe), Tabora (Usule), Mtwara (Mang’amba) na Shinyanga (Ibadakuli).
Bei ya nyumba ni kati ya Tsh 59,000,000.00 hadi Tsh 80,000,000.00 (Bila ya VAT) kulingana na ukubwa wa nyumba na Mkoa nyumba ilipo.   Ukubwa wa nyumba ni kuanzia vyumba viwili hadi vinne. Fomu zinapatikana kwa gharama ya shilingi elfu tano (TShs. 5,000/=) kwenye ofisi za Mfuko zilizopo mikoa yote nchini.
Waombaji wanaohitaji kuona na kukagua nyumba wawasiliane na Mfuko kupitia namba 2120912/52 au 2127376.
“PSPF - Tulizo la Wastaafu”
Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Mkurugenzi Mkuu,
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF),
Golden Jubilee Towers,
Front Tower – Ghorofa ya 6-13,
Mtaa wa Ohio/Kibo,
S. L. P. 4843,
DAR ES SALAAM.
Barua Pepe: pspf@pspf-tz.org          


 Tovuti: www.pspf-tz.org  

PSPF YAFUNGUA OFISI ZAO NJOMBE NA KATAVI







Mh. Tundu Lissu amwaga sera ndivyo sivyo.

DSC01254
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki Mh. Tundu Lissu akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya nafasi ya udiwani kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi uliofanyika katika kijiji cha Iseke.
DSC01259
DSC01240
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Iseke tarafa ya Ihanja waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya udiwani kata ya Iseke uliofanywa na chama cha CHADEMA.
DSC01255
Baadhi ya viongozi wa CHADEMA waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya udiwani wa kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mgeni rasmi katika kampeni ya uzinduzi wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi Mh. Tundu Lissu, ameashindwa kuuza sera za CHADEMA na badala yake ametumia muda na nguvu nyingi kuhimiza sera yake ya ‘katazo’ la wananchi kuchangia maendeleo yao .
Mh. Tundu Lissu ambaye ni mbunge wa jimbo la Singida Mashariki kupitia tiketi ya CHADEMA, alipanda jukwaani huku akiwa mabeba makabrasha ya michanganuo ya bajeti ya serikali ya kuanzia mwaka wa fedha wa 2010/2011 hadi 2013/2014.
 Akisema na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika katika kijiji cha iseke, Mh Tundu Lissu aliweka wazi kuwa “Mimi sitaki kabisa kuzungumzia habari za Amosi Mghenyi ambaye ametusaliti kwa kuhama CHADEMA na kurejea CCM.  Amosi kisiasa ni mfu, kwa hiyo siwezi kupoteza muda wangu kuzungumiza mambo ya mfu”.
Amesema ufunguzi wake utajikita zaidi katika kuwaelimisha wananchi wa kata ya Iseke kwamba serikali inayo fedha nyingi na za kutosha kugharamia maendeleo ya wananchi.
Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, amesema kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, mkoa wa Singida, ulipewa zaidi ya shilingi milioni 903 za undeshaji wa shule, lakini zilizotumika ni zaidi ya shilingi milioni 464 na kubaki zaidi ya shilingi 438.2.
 Amesema fedha hizo zaidi ya shilingi 438.2 zilizobaki,  hazijaainishwa zilipelekwa wapi.  “Kwa vyo vyote zitakuwa zimeishia kwenye matumbo ya mgambo na watendaji wa serikali ya CCM”.
Mh. Tundu ambaye pia ni mwanasheria kitaaluma, amewataka wakazi wa kata ya Iseke, kumchagua Emmnuel Jackson Jingu awe diwani wao, ili waondokane na manyanyaso ya michango kama walivyojikomboa wakazi wa jimbo la Singida Mashariki.
 Wagombea wengine wa nafasi ya udiwani kata ya Iseke ni Amosi Munghenyi wa CCM na Abdallah Kinyenje maarufu kwa jina la Petro wa CUF.
 
 
 

CHANZO MO BLOG

MAHAKAMA ya Rufaa yamrejeshea ubunge wa Igunga-CCM Dr. Dalali Peter Kafumu asubuhi ya leo.



 Mbunge wa jimbo la Igunga-Tabora-CCM ndugu Dalaly Peter KAFUMU
 -
Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Igunga-Tabora ndugu Dalaly Peter KAFUMU amerudishiwa ubunge wake na mahakama leo hii asubuhi baada ya aliyekuwa mgombea kupitia CHADEMA ndugu Kashinde kushindwa kuwakilisha risiti ya hati ya kiwanja wakati wa kesi ya msingi ya kwanza,Hivyo CHADEMA wamepoteza huko Igunga.FUATILIA
 

Jela Miaka 30 kwa kunajisi mtoto

MAHAKAMA ya Wilaya Manyoni mkoani Singida imemhukumu mkazi wa kijiji cha Matangalala wilayani humo, Maduhu Dotto (31) kwenda jela miaka 30 baada ya kumkuta na hatia ya kunajisi mtoto. Aidha, Maduhu na mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo, Juliana Malungo (28), wametakiwa kulipa faini ya Sh 200,000 kila mmoja. Malungo ambaye ni mkazi wa mtaa wa Chang'ombe mjini Manyoni, alipatikana na hatia ya kula njama na Maduhu na kwamba ndiye aliyefanikisha kitendo cha kunajisi msichana mwenye miaka 14, kwa ahadi ya kumzawadia vitenge binti huyo. Mwendesha Mashitaka, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Hamis Fussi alidai mbele ya Kaimu Hakimu wa Wilaya ya Manyoni, Terrysophia Tesha kuwa Aprili 28 mwaka jana saa 6:45 mchana washitakiwa kwa pamoja walikula njama za kumnajisi binti huyo na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri. Fussi alidai kuwa siku ya tukio Juliana alikwenda nyumbani kwa mlalamikaji ( ambaye ndiye binti alinajisiwa) na kumshawishi binti huyo amsindikize mnadani. Hata hivyo, hawakwenda mnadani, badala yake mshitakiwa alimpeleka binti huyo nyumbani kwake, ambako alikuwepo Maduhu na Juliana alimfungia ndani binti huyo wakiwa na Maduhu, naye akaondoka. Alidai kuwa kutokana na kufungiwa huko, Maduhu aliamua kumwingilia kimwili binti huyo bila ridhaa yake na hivyo kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri. Fussi aliiomba Mahakama itoe adhabu kali kwa washitakiwa, akidai kuwa vitendo vya kunajisi vinachangia mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa, ikiwemo wa Ukimwi. Akitoa hukumu, Hakimu Tesha alisema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka, umethibitisha bila kuacha shaka yoyote kuwa washitakiwa walitenda makosa hayo. 
 Chanzo Habari Leo
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa