Home » » DADA WA KAZI AMUUA BOSI WAKE KWA KISU

DADA WA KAZI AMUUA BOSI WAKE KWA KISU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
SAKATA la wafanyakazi wa ndani kunyanyaswa na mabosi wao, limechukua sura mpya baada ya Valetina Kerenge (17), kumgeuzia kibao bosi wake.
Mfanyakazi huyo wa ndani, mwenyeji wa Wilaya ya Ukerewe, mkoani Mwanza, anadaiwa kumuua bosi wake, Asha Juma (24) kwa kumchoma kisu sehemu ya juu ya titi la kulia kwa madai ya kuchoshwa na manyanyaso.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida (SACP), Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo la kusikitisha limetokea jana majira ya saa nne asubuhi katika eneo la Sabasaba, Kata ya Utemini, mkoani hapa.
Alisema Asha alikuwa karani wa Mahakama ya Wilaya ya Singida na alikuwa akiishi na mfanyakazi wake huyo wa ndani kwa takribani mwaka mmoja sasa.
“Baada ya msichana huyo kumchoma bosi wake kwa kisu, alitoka nje ya nyumba na kukimbilia kwa majirani kwa ajili ya kuomba msaada, lakini wakati majirani wakiwa katika harakati za kumpeleka majeruhi huyo hospitali, alianguka chini na kufa papo hapo,” alisema Kamanda Kamwela.
 Kwa mujibu wa kamanda huyo, mtuhumiwa huyo alikimbia  baada ya bosi wake kufariki dunia, lakini majira ya saa nane alikamatwa akiwa kwenye harakati za kutoroka.
“Kwa ushirikiano na raia wema, tulifanikiwa kumkamata msichana huyo jana majira ya saa nane eneo la Uwanja wa Ndege akiwa katika harakati za kutoroka,” alisema Kamanda Kamwela.
Alisema mtuhumiwa anahojiwa kuhusiana na tukio hilo na uchunguzi zaidi unaendelea kujua chanzo cha mauaji hayo.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa