Home » » MIL.857/-KUKAMILISHA MIRADI YA MAJI MANYONI

MIL.857/-KUKAMILISHA MIRADI YA MAJI MANYONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WIZARA ya Maji imetenga sh milioni 857 ili kukamilisha programu ya maji vijijini na usafi wa mazingira katika vijiji 10 vya Tarafa ya Kintinku wilayani Manyoni, Singida vilivyopo kwenye mradi wa Benki ya Dunia.
Fedha hizo zilizotengwa kwenye mwaka wa fedha 2014/2015 ni sehemu ya sh bilioni 1.5 kwa ajili ya tarafa hiyo kuwawezesha wakazi wa vijiji hivyo kuwa na uhakika wa majisafi na salama kabla ya mwisho wa mwaka 2015.
Naibu Waziri wa Maji, Amosi Makala, alitoa ahadi hiyo alipozungumza na wakazi wa Kata ya Chikuyu, Tarafa ya Kintinku kuhusu kumalizika kwa tatizo la maji lililowakabili kwa muda mrefu.
Makala ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero, alivitaja vijiji vitakavyonufaika na mradi huo kuwa ni Kintinku, Lusilile, Ngaiti, Mvumi, Maweni, Chilejeho, Mtiwe, Chikuyu, Mwiboo na Mbwasa.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa tarafa hiyo, Diwani wa Viti Maalumu, Zinduna Abdallah (CCM), alimweleza naibu waziri huyo kwamba tatizo la maji limeharibu ndoa za watu.
Mhandisi wa Sekretarieti ya mkoa huo, Yunusi Rugeyamu, alisema sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa Singida ilikuwa na wakazi 1,370,637 na kwamba hadi Desemba mwaka jana wakazi 656,932 waishio vijijini wanapata maji.
Chanzo;Tanzania Daima  

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa