Home » » RC ASISITIZA WANANCHI KUSOMEWA MAPATO NA MATUMIZI

RC ASISITIZA WANANCHI KUSOMEWA MAPATO NA MATUMIZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

SERIKALI za vijiji mkoani Singida zimetakiwa kuwasomea wananchi wake kwa mujibu wa taratibu taarifa za mapato na matumizi ya makusanyo mbalimbali wanayofanya ili kuondoa malalamiko yoyote yasiyo ya lazima.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone alitoa agizo hilo katika Kata ya Kindai wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya maabara kwenye shule mbalimbali za sekondari zilizopo Manispaa hiyo.
Mkuu huyo wa Mkoa alilazimika kutahadharisha hilo baada ya baadhi ya wananchi kulalamika mbele ya yake kuwa uongozi wa kata hiyo hauna utamaduni wa kuwasomea taarifa za mapato na matumizi kwa mujibu wa taratibu na kuna ubadhirifu mkubwa.
Chanzo;Habari Leo

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa