Home » » SIKIKA YAWAGAWA MADIWANI KONDOA

SIKIKA YAWAGAWA MADIWANI KONDOA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
BAADHI ya madiwani katika Halmashauri ya Wilaya Kondoa, wamejitokeza kupinga uamuzi uliofikiwa na Baraza la Madiwani wa kulifukuza Shirika la Sikika wilayani humo.
Wakizungumza na gazeti hili hivi karibuni, madiwani hao walisema uamuzi huo hauna afya kwa maendeleo ya wilaya hiyo, kwani shirika hilo lilikuwa likisaidia kuonyesha udhaifu uliopo katika idara ya afya.
Kwa mujibu wa madiwani hao, uamuzi wa shirika hilo kufukuzwa ulianza kutengenezewa mazingira kwa madiwani wa CCM kufungwa na msimamo wa kichama juu ya shirika hilo.
Diwani wa Kata ya Kondoa Mjini, Hamza Mafita (CCM), alisema Sikika ni jicho la pili ambalo kama lingetumiwa vizuri lingeweza kuwasaidia madiwani kuona uchafu mahala ambapo wameshindwa kuufikia.
“Kuhusu Sikika mimi nilijua shirika hili litafukuzwa tu kwa sababu ya viongozi wetu kupenda kulinda ufisadi. Katika bajeti ya mwaka 2012/2013 miradi ya afya shughuli namba 12 ilitengewa bajeti ya sh milioni 17 kwa ajili ya kukarabati vizimba vya kuchomea takataka.
“Ilikuwa ni kwa ajili ya vituo vya afya vya Hamai na Mrijo. Kizimba cha Hamai kilijengwa chini ya kiwango thamani yake hata milioni mbili hakifiki, Mrijo kule hicho kizimba chenyewe hakipo,” alisema.
Diwani wa Viti Maalumu, Hija Suru (CCM), alisema uamuzi wa shirika hilo kufukuzwa ulikuwa na msukumo ndani yake wenye sura inayotiliwa shaka dhidi ya madiwani.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Suruke, Jafari Ganga (CUF) alisema uamuzi huo ulifanywa na madiwani wa CCM lakini madiwani wa upinzani walipiga kura ya kukataa shirika hilo kufukuzwa.
“Kikao cha Julai 26 kilihudhuriwa na madiwani 36 madiwani 26 wa CCM walishikizwa kupiga kura ya kuiondoa Sikika madiwani 10 wa upinzani tulikataa,” alisema.
Wakijibu madai hayo, Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Hisdory Mwalongo na Mwenyekiti wa halmashauri, Khamis Mwenda walitetea msimamo wao na kusema kuwa hatua zilizochuliwa dhidi ya shirika hilo ni sahihi.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa