Home » » WAJUMBE WAUNGA MKONO PENDEKEZO LA RASIMU YA KATIBA

WAJUMBE WAUNGA MKONO PENDEKEZO LA RASIMU YA KATIBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Shamsi Vuai Nahodha
 
Wajumbe wa kamati namba mbili wamefanya marekebisho katika ibara ya 21 (3) kwa kueleza mtumishi wa umma atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria baada ya kusimamishwa kama ilivyopendekezwa kwenye rasimu ya katiba.
Ibara hiyo inasema: “Kiongozi wa umma ambaye anatuhumiwa kwa makosa ya: (a) kimaadili; (b) udhalilishaji wa mtu au wa kijinsia; au (c) wizi au ubadhirifu wa mali za umma, atasimamishwa kazi hadi suala lake litakapoamuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi au taratibu nyingine zinazowahusu viongozi wa umma.”

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Shamsi Vuai Nahodha (pichani), alisema wajumbe hao waliona ibara hiyo imetoa adhabu moja kwa moja na kwamba, katiba haipaswi kuadhibu moja kwa moja.

“Kifungu C tumebadilisha na kusema atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria, mtu ametuhumiwa anafukuzwa halafu akienda mahakamani akashinda itakuwaje, hivyo tumeweka atachukuliwa hatua,” alisema.

Alisema kifungu hicho kitasomeka kiongozi wa umma, ambaye anatuhumiwa kwa makosa ya wizi, rushwa au ubadhilifu wa mali ya umma atachukuliwa hatua.

Nahodha alisema sheria ndiyo itaainisha hatua za kuchukuliwa kwa mtumishi kuliko katiba kutoa adhabu, ambayo itakuwa hatari.

Alisema kamati yake inabadilisha baadhi ya maeneo bila kuathiri maudhui ili kuwa na katiba yenye lugha fasaha na siyo maneno yenye maana zaidi ya moja ili kila atakayeisoma apate maana iliyokusudiwa.

Kamati 12 za Bunge hilo zimejichimbia katika kumbi mbalimbali kujadili sura 15 za Rasimu hiyo kwa muda wa siku 16, huku baadhi ya kamati zikiwa katika sura ya tano na saba.
 
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa