Home » » AFYA YA UZAZI: NAMNA YA KUCHUNGUZA HATUA ZA KUJIFUNGUA

AFYA YA UZAZI: NAMNA YA KUCHUNGUZA HATUA ZA KUJIFUNGUA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Moja ya malengo ya milenia ni kupunguza kama si kuondoa kabisa vifo vya kinamama na watoto vitokanavyo na ujauzito, wakati wa kujifungua na wakati wa kulea.
Hili litawezekana tu iwapo kutakuwepo na huduma bora zitakazohakikisha uwepo wa uzazi salama.
Zipo sababu nyingi zinazochangia vifo vya uzazi lakini vingi vinasababishwa na uzingatiaji dhaifu wa muongozo wa uzazi salama.
Mwongozo uliotayarishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jami unaaminika kuwa ni bora kuliko ile iliyoandaliwa katika nchi nyingine za Afrika Mashariki na Kati.
Hii inamaana kwamba mwingozo huo  ukizimamiwa vizuri na wadau wote basi tatizo hili litakwisha.
Si kila wakati vifo hivi vinatokea kutokana na sababu za miundo mbinu kwani baadhi yake hutokea hata sehemu ambazo miundo mbinu si mibaya kiasi cha kusababisha ucheleweshaji wa kufanya uamuzi sahihi. 
Kadi ya kliniki ya wajawazito imetayarishwa maalumu kuelezea hatua kwa hatua namna ya kumhudumia mama mjamzito.
Huduma hizo ni tangu anapopata ujauzito, kutunza ujauzito, kujifungua na hata kwa kipindi fulani kilichopendekezwa baada ya kujifungua.
Kadi  hii kama itatumika vizuri ni rahisi kugundua viashiria vyote vya hatari na hatimaye kuchukua hatua kwa muda muafaka.
Kadi hii imegawanywa katika sehemu kuu tano na zote ni muhimu.
Sehemu yenye jedwali la hatua za uchungu ndio mahususi kwa dalili na hatua za kujifungua.
Baada ya njia kufunguka hatua inayofuata ni kutoka kwa mtoto kwa kanuni maalumu.
Lakini kufunguka kwa njia mpaka kiwango cha mwisho  si kila wakati inamaanisha mtoto atatoka.
Hii ni ishara hatarishi na kama hatua za jedwali zimesimamiwa vizuri litaonyesha hivyo ili hatua stahiki zichukuliwe.
Huu ni mfano mmoja tu. Uchambuzi wa kina kuhusu kadi ya kliniki ya wajawazito umefanywa katika makala zilizotangulia katika gazeti hili.
Iwapo mototo atatoka salama hatua inayofuata ni  kutoka kwa kondo la nyuma.
Ni wajibu wa mtoa huduma kuhakikisha kuwa kondo hilo limetoka katika muda muafaka na pia kulikagua kama limekamilika.
Chanzo;Mwananchi 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa