Home » » MWANZA WAIKUBALI WINDHOEK WAFURAHIA MPANGO WA KIWANDA CHA MABIBO BIA WA KUJENGA KIWANDA

MWANZA WAIKUBALI WINDHOEK WAFURAHIA MPANGO WA KIWANDA CHA MABIBO BIA WA KUJENGA KIWANDA



Chupa za Windhoek zinavyoonekana.
 Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira akizungumza na wadau na wanahabari wa jiji la Mwanza wakati wa Promosheni ya Bia za Windhoek iliyofanyika leo usiku katika Hoteli ya Villa Park Resort jijini humo.
 Mshauri Mkuu wa Fr James Rugemalira, Aniki Kashasha akizungumza na wadau wa jiji la Mwanza pamoja na wanahabari kuhusu bia za windhoek Lager na Windhoek Draught.
  Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira (katikati), akiwa amekaa na viongozi mbalimbali meza kuu. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni inayosambaza Gas ya Oryx jijini Mwanza ya Top Kihanja Co Ltd, Christopher Kilaja, Mshauri Mkuu wa Fr James Rugemalira, Aniki Kashasha, Fr James Rugemalira, Mwanasheria Tamy Henry na Michael Thomas ambaye pia na Mwanasheria. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Mwanahabari wa Kituo cha Televisheni cha Star TV, Yvone Kamuntu akiuliza swali katika promosheni hiyo.
 Mdau wa Windhoek Mertus Rutashobwa naye alikuwa ni miongoni mwa waalikwa waliopata fursa ya kuizungumzia bia ya Windhoek.
Ofisa Mipango wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Victor Maleko akizungumza katika promosheni hiyo kwa niaba ya wanahabari wa mkoa wa Mwanza.




 Wanahabari wakiwa kwenye promosheni hiyo.
 Wageni waalikwa wakiwa kwenye promosheni hiyo.
 Hapa wadau wa Windhoek wakibadilishana mawazo.


 Warembo hao walikuwepo kupata Windhek katika promosheni hiyo.
 Wanahabari wakichukua taarifa mbalimbali katika 
promosheni hiyo.
 Majadiliano yakiendelea.




 Wadau wakiendelea kupata Windhoek.
 Wadau wa Windhoek ndani ya Villa Park Resort 
katika promosheni hiyo.
 Hapa shughuli imepamba moto waalikwa wakimsikiliza Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr.James Rugemalira.

Dotto Mwaibale

WAKAZI wa jiji la Mwanza na mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa, wamefurahishwa na uwekezaji unaotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Bia ya Mabibo (MBL) kwa ajili ya kujenga kiwanda cha bia za Windhoek.

Wakizungumza katika promosheni iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza juzi katika  ukumbi wa Villa Park Resort, wanachi hao walionesha kuguswa na uwekezaji huo na kushauri kijengwe kiwanda hicho jijini Mwanza.

Walisema kujengwa kwa kiwanda hicho kutachochea kasi ya maendeleo  ya kiuchumi na kuongeza ajira kwa vijana wa Kanda ya Ziwa.

Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira alisema lengo la kufika Mwanza ni kupata mawazo mapya na ushauri wa nini kifanyike katika uwekezaji huo jijini humo.



“Tumeamua tuje Mwanza na kuomba ushirikiano wenu na rai yangu ni kupata maoni yenu ili tukipata fursa tuwe na viwanda vidogo vidogo,lakini si sawa na Tanzania Breweries (TBL),maana hatuwezi kushindana nao,” alisema Rugemalira.

Alisema ushindani wa haki ni lazima kila mtu apate haki ya kushinda,na wataka waweke misingi hiyo kwanza katika mikoa ya Mwanza, Kagera, Mbeya na Mtwara kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo.

Aliwataka wananchi wa kanda ya ziwa kuwaonesha  na kuwaunga mkono ili wazalishe kinywaji cha windhoek Mwanza badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi kama ilivyo sasa,ambapo kinywaji hicho kinagizwa kutoka nchini Namibia.

“Mtu anaweza kunipa ushauri au akaniamuru atakavyo ili nijitambue na ni vema kukubaliana na ushindani  bila hivyo hatuwezi kupata maendeleo na malengo ya kampuni yetu ni kushirikiana na serikali kukabiliana na uhaba wa ajira kwa Watanzania kwa kujenga viwanda hivyo ”alisema Rugemalira.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Mabibo Bia (MBL), Kanda ya Ziwa, Godfrey Mwangungulu alisema Bia ya Windhoek imewahi kushinda medali za juu saba  kwa ubora Barani Afrika tangu ianze kuzalishwa mwaka 1920.

"Bia ya Windhoek ilishinda tuzo hizo mfufulizo kuanzia mwaka 2007, 2008, 2009,2010,2011,2012  na 2013. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa