Home » » TRA YAAGIZWA KUHARAKISHA UKAGUZI WA SUKARI NCHINI

TRA YAAGIZWA KUHARAKISHA UKAGUZI WA SUKARI NCHINI

 
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe
 
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imeiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuharakisha agizo la ukaguzi wa sekta ndogo ya sukari ili kupata ufumbuzi wa haraka.
 
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, akitoa maamuzi mara baada ya kuhojiana na TRA, alisema uingizwaji holela wa sukari una hatari kwa ukuaji wa viwanda vya ndani.
 
“Tunataka taarifa ili tuweze kuwa na mikakati endelevu ya kuzuia sukari ya magendo, unasababaisha sukari inayozalishwa na viwanda vyetu na miwa ya wakulima ina kosa soko,” alibainisha.
 
Hivi karibuni, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene, alipotembelea kiwanda cha sukari cha TPC mkoani Kilimanjaro, alielezwa jinsi sukari ya nje iliyojaa sokoni na wao kukosa pa kuiuza.
 
Alisema watakutana na Wizara zinazohusika kujadili na kuanza operesheni maalum kwenye maduka mbalimbali na kukamatwa sukari ya nje na ya viwandani inayouzwa kwa wananchi kwa bei ndogo.
 
CHANZO: NIPASHE
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa