Home » » TONE NA KILIMO: UFAHAMU UYOGA WA ASILI KUTOKA TANZANIA NA FAIDA ZAKE.

TONE NA KILIMO: UFAHAMU UYOGA WA ASILI KUTOKA TANZANIA NA FAIDA ZAKE.




Uyoga ni zao la viumbe hai viitwavyo kuvu (fungi). Tanzania inao utajiri mkubwa wa uyoga wa asili. Uyoga wetu wa asili hupatikana wakati wa msimu wa mvua tu. Hili ni tatizo kubwa kwa vile wananchi walio wengi hupenda kula uyoga wakati wote.

Kwa sababu ya upatikanaji wa uyoga kwa msimu, na kwa vile aina nyingine za uyoga wa kienyeji zina sumu, tumefanya jitihada za kuanzisha kilimo cha uyoga ili kukidhi mahitaji ya wananchi kwa mwaka mzima. Pamoja na kutoa lishe bora kwa watu, uyoga pia unaweza kuzalishwa kama zao la biashara.

UMUHIMU WA ZAO LA UYOGA.

Uyoga kama chakula una viinilishe vingi vilivyo muhimu kwa afya ya binadamu. Uyoga una protini kati ya 3-4. Pia una vitamini B, C, D na K. Uyoga pia una madini yanayohitajika katika mwili wa binadamu.

Uyoga ukitumika kama sehemu ya chakula cha familia mara kwa mara hutibu au kuzuia magonjwa kama vile saratani, vidonda vya tumbo, shinikizo la damu pia huongeza kinga ya mwili.

Kilimo cha uyoga huchangia pato la kaya na hutoa ajira. Kilimo hiki ni kizuri kwa wazee, akina mama na vijana kwa vile hakihitaji mtaji mkubwa kuanzisha na mavuno hupatikana baada ya muda mfupi. Aidha kilimo hiki hakihitaji eneo kubwa kama mawazo mengine kwani uyoga huoteshwa ndani ya banda.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa