Home » » NDOTO YA WEMA SEPETU KUWA MBUNGE YAYEYUKA

NDOTO YA WEMA SEPETU KUWA MBUNGE YAYEYUKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Haikuwa bahati yake. Safari ya Wema Sepetu kuelekea bungeni imefikia tamati.

Hiyo ni baada ya kushindwa kuwashawishi wanachama wa CCM mkoani mkoani Singida kumpa dhamana ya kuwawakilisha kwenye viti maalum vya ubunge.
Wema ameshindwa kupita kwenye kura za maoni za ubunge huo kwa kupata kura 90 tu. Aliyeongoza kwenye kinyang’anyiro hicho ni Aysharose Mattembe (311), Martha Mlata (235) na Diana Chilolo (182).
Wema amekubali kushindwa na kudai kuwa ushiriki wake umempa ujasiri zaidi.
“Nilivyoamua kugombea viti maalum, nilijua kuna kupata na kukosa. Awamu hii nimekosa, ila dunia bado inazunguka,” ameandika kwenye kwenye Instagram.
“Nawapongeza walioshinda. Nawashukuru mlioniunga mkono, Mungu aendelee kuwabariki kwa mapenzi yenu juu yangu, yananipa moyo. Nawashukuru pia wote mlionipinga maana mmeniongezea ujasiri na nina nguvu mpya ya kuthubutu upya,” ameongeza.
“2015 ni mwaka wa kipekee kwenye muamko wa vijana Tanzania. Bigger things loading.. Most of all Nilizaliwa nikiwa katika Chama Cha Mapinduzi na nitakufa nikiwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi…. Safari yangu ya Siasa ndo kwanza inaanza.”

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa