MAONESHO YA UTALII YA SANGANAI/HLANGANANI–(WORLD TOURISM EXPO) ZIMBABWE YAFUMBUA MACHO WATANZANIA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

IMG_4145
Pichani juu na chini ni Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kushoto) akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali za utalii na vivutio vyake nchini Tanzania kwa baadhi ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali vikiwemo vya utalii nchini Zimbabwe waliofika katika banda la Tanzania kwenye maonyesho ya nane ya Kimataifa ya Utalii Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) kupata taarifa mbalimbali za vivutio vya utalii wa Tanzania yaliyomalizika jana jijini Harare katika ukumbi wa hoteli ya Rainbow Towers.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)
IMG_4137 IMG_4168
Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kulia) akibadilishana mawazo na wananfunzi wa Belvedere Technical Teachers College nchini Zimbabwe, Francisca Chipuriro (kushoto) na Natalie Takavarasha (katikati) wakati walipotembelea banda la Tanzania kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali za utalii wa Tanzania na vivutio vyake siku ya ufunguzi rasmi wa maonyesho hayo yaliyomalizika juzi jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers.
IMG_4185
Wageni mbalimbali waliovutiwa na vivutio vya utalii nchini Tanzania wakiendelea kumiminika katika banda la Tanzania na kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kulia) ambapo hivi sasa Shirika la ndege la Fastjet limeanza safari zake jijini Harare kupitia Lusaka hadi Dar es Salaam kwa gharama nafuu kabisa itakayowezesha wananchi wa Zimbabwe kufanya safari za Tanzania kwa gharama nafuu kabisa.
IMG_4229
Meneja Masoko na Tehama wa kampuni ya Best Northern Tours and safaris nchini Tanzania, Mary Joel akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali za utalii zinazofanywa na kampuni yake kwa wageni waliofika katika banda la Tanzania wakati wa maonyesho hayo yaliyomalizika juzi jijini Harare.
IMG_4241
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah (wa pili kulia) akitoa maelezo yaliyomo kwenye vipeperushi vyenye taarifa mbalimbali za vivutio vya utalii nchini Tanzania kwa wageni waliotembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho nane ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare.
IMG_4191
Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel ya nchini Tanzania, Joseph Waryoba (kulia) akipata picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii nchini Zambia, Felix Chaila aliyembelea banda la Tanzania wakati wa maonesho ya siku tatu ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers ambayo yamemalizika juzi.
IMG_4195
Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel nchini Tanzania, Joseph Waryoba katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tanzania Travel Company ambayo pia imeshiriki maonyesho ya utalii nane ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare.
IMG_4205
Timu kutoka Tanzania ambayo imeshiriki maonyesho ya utalii nane ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare ikiongozwa na Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (wa pili kulia). Kutoka kushoto ni Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel nchini Tanzania, Joseph Waryoba, Meneja Masoko na Tehama wa kampuni ya Best Northern Tours and safaris nchini Tanzania, Mary Joel pamoja na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah (kulia).
Na Modewjiblog team, Harare
TIMU ya watanzania walioenda kuhudhuria maonesho ya utalii nchini Zimbabwe wamesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kujifunza uendeshaji wa sekta ya utalii.
Walisema katika ziara yao hiyo wamegundua kwamba Wazimbabwe kuanzia wanapompokea mgeni hadi anapofika hotelini wanaonesha kujali hali ambayo mgeni hawezi kusahau hata kidogo.
Aidha amesema kwamba hata mipangilio ya kwenda kwenye vivutio inafanyika katika hali ambayo huwezi kusahau hata kidogo.
Kutokana na mazingira hayo, wamesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kujifunza namna ya kupokea na kuishi na wageni na kuwatengenezea taswira ambayo hawatakaa wakisahau.
Hayo yamesemwa na Ofisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon katika mahojiano maalum na mtandao wa habari wa modewjiblog yaliyofanyika mjini Harare siku ya ufunguzi rasmi wa maonesho ya siku tatu ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers jijini Harare.
Solomon amesema ingawa hali ya Tanzania si mbaya, watendaji katika viwanja vya ndege na mahotelini wanaweza kuangalia namna Wazimbabwe wanavyojali kazi zao na tabasamu zao nyakati zote kwa wageni .
“Si kwamba kwetu kuna shida lakini unaona watu wanavyojituma hapa” alisema Esther Solomon na kuongeza kuwa aliona jinsi walivyojipanga vizuri na wafanyakazi walikuwa na uelewa wa hali ya juu.
Esther aliongoza kundi la watu watano wa Kitanzania walioalikwa na mamlaka ya utalii Zimbabwe (ZTA) kuhudhuria maonesho hayo.Tanzania iliweka banda lake pia katika maonesho hayo ya siku tatu yaliyomalizika juzi.
Makampuni ya mawakala wa utalii aliyoambatana nayo katika safari hiyo ni pamoja na Tanzania Travel Company, Cordial Tours and Travel, Mberesero Tented Camp na Best Northern Tours and safaris .
Alisema safari yao Zimbabwe pamoja na ushiriki wao katika maonesho pia walifika katika maeneo mbalimbali ya kitalii nchini yakiwemo maporomoko ya Victoria.
Aidha walipewa nafasi ya kukagua sehemu za malazi kwa ajili ya wageni.
Alisema katika maonesho hayo wamefanikiwa kupata wageni wengi wanaoulizia namna ya kufika Tanzania na pia ushirikiano wa makampuni katika sekta ya utalii.
“ Watu wengi wamekuja kututembelea. Na wengi ni watu weusi. Mwamko wao wa kutembelea vivutio ni mkubwa.” Alisema Esther na kuongeza kuwa wamebaini kwamba ipo haja ya watanzania kuhimizwa kutembelea vivutio kwani hata nchini Zimbabwe wanaotembelea vivutio ni wananchi wenyewe.
Alisema wengi waliofika katika banda la Tanzania waliulizia namna ya kufika visiwa vya Zanzibar na pia mbuga za Tanzania.
Aidha mawakala wengi waliulizia namna ya kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha utalii katika bara la Afrika.
Asilimia 80 ya watalii nchini Zimbabwe wanatoka bara la Afrika na waliobaki ndio wanatoka nje ya bara hili.

MINYUKANO YA UCHAGUZI TANGU 1958

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Hayati Mwalimu Julius Nyerere
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imepanga Oktoba 25 mwaka huu kuwa siku ambayo Watanzania watakuwa wanapiga kura kuwachagua viongozi wapya katika nafasi za udiwani, ubunge na urais.
Historia inaonyesha kuwa uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa 14 tangu nchi ianze kuwa na mfumo wa kuchagua viongozi wake.
Hata hivyo, tofauti na chaguzi zingine, uchaguzi wa mwaka huu utakuwa na changamoto mpya kwa chama tawala CCM, kutokana na kuwa vyama vinne vya upinzani; Chadema, CUF, NLD na NCCR-Mageuzi, vimeamua kuungana na kuunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vikiwa na lengo la kupambana na CCM kuhakikisha vinaing’oa madarakani.
Ukawa wamekubaliana kumsimamisha mgombea mmoja wa urais, ubunge katika jimbo husika na diwani kupambana na mgombea wa CCM.
 Historia ya uchaguzi
Historia ya uchaguzi nchini inaweza kugawanywa katika makundi matatu; Chaguzi tatu chini ya mfumo wa vyama vingi zilifanyika enzi za Tanganyika, chaguzi hizo mbili zilifanyika kabla ya uhuru mwaka 1958 na 1960  na uchaguzi wa tatu ulizofanyika Novemba Mosi mwaka 1962 baada ya uhuru, kabla ya Tanganyika kuungana na Zanzibar.
Baadaye kukafuatia miongo mitatu ya utawala wa chama kimoja na kulifanyika chaguzi sita; uchaguzi wa mwaka 1965, uchaguzi wa 1970, uchaguzi wa 1975, uchaguzi wa 1980, uchaguzi wa 1985 na uchaguzi wa mwaka 1990.
Mfumo wa vyama vingi ulirejeshwa nchini mwaka 1992 na tangu wakati huo kumekuwa na chaguzi nne; uchaguzi mkuu wa 1995, uchaguzi wa mwaka 2000, uchaguzi wa mwaka 2005 na uchaguzi wa mwaka 2010. Katika historia hiyo, kumekuwa na chama kimoja tu ambacho ndicho kimeendelea kutawala, CCM kilichoundwa mwaka 1977 baada ya muungano wa vyama viwili vya TANU na ASP.
 Uchaguzi wa kwanza uliofanyika nchini 1958 kwa ajili ya kuchagua wabunge ulikuwa ukijulikana kama uchaguzi wa karata tatu. Uchaguzi huo ndio uliopima ukomavu na nguvu ya Tanu kama sehemu ya maandalizi ya kuondokana na utawala wa kikoloni.
 Uchaguzi wa karata tatu
Uchaguzi huo ndiyo uliopima ukomavu na nguvu ya Tanu kama sehemu ya maandalizi ya kuondokana na utawala wa kikoloni.
Katika uchaguzi huo, wapigakura walitakiwa kuchagua mgombea mmoja kutoka kila kundi: Mwafrika, Mhindi na Mzungu, hivyo kupata wagombea watatu. Kwenye kitabu chake cha Modern History of Tanganyika alichotunga 1976, Mwanahistoria wa Kiingereza  John Iliffe alisema, uchaguzi wa aina hiyo ulidhaniwa kuwa ungemaliza migongano. Hata hivyo, serikali ya kikoloni iliweka sifa ya mpigakura kuwa ni pamoja na kipato cha Paundi 150 kwa mwaka, elimu ya miaka minane au kuwa na ofisi inayotambulika.
Mwanzoni sifa hizo zilipingwa na Tanu ambayo ilitishia kujitoa kwenye uchaguzi huo, ikisema kuwa Waafrika wengi maskini, wasiokuwa na ajira wangezuiwa kupiga kura. Lakini baadaye kikundi cha wanasiasa wa Tanu chini ya Mwalimu Nyerere, kiligundua kuwa kugomea uchaguzi huo kungechelewesha uhuru wa Tanganyika au kungetoa mwanya wa ushindi rahisi kwa chama pinzani cha United Tanganyika Party (UTP) kilichokuwa kikiendeshwa na walowezi wa kizungu.
Katika mkutano wake wa mwaka, uliofanyika Januari 1958, Tanu kilikubali kushiriki uchaguzi huo.  Wakati huo pia Tanu ilikuwa na migogoro ya ndani iliyosababisha mmoja wa waanzilishi wake, Zuberi Mtemvu, kujitoa na kuanzisha chama kipya cha African National Congress (ANC).
Pamoja na tofauti hizo, Tanu ilifanikiwa kupata ushindi mnono baada ya kupata viti 28 kati ya viti 30 vilivyokuwa vikishindaniwa.  Mwaka 1960 ulifanyika uchaguzi wa wabunge na Tanu kikaendeleza ushindi wake kwa kupata viti  70 kati ya viti 71 vilivyokuwa vikishindaniwa.
Tanganyika ilipata uhuru wake Desemba 9, 1961 na Mwalimu Nyerere akawa Waziri Mkuu chini ya usimamizi wa Malkia Elezabeth wa Uingereza. Januari mwaka 1962, Mwalimu Nyerere alijiuzulu wadhifa huo na Rashidi Kawawa akachukua nafasi yake. Nchi ikawa Jamhuri na ilianza kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi wa rais Novemba 1962. Katika uchaguzi huo wa rais, Chama cha Tanu kilikabiliana na Chama cha ANC na wapigakura milioni 1.8 walijiandikisha.  TANU ilishinda kwa asilimia 98.15 na Nyerere akawa Rais wa Tanganyika.
Baada ya uchaguzi huo Tanganyika ikawa taifa la chama kimoja cha siasa na mwaka 1964 iliungana na Zanzibar na kuunda Tanzania.
Wakati wa demokrasia ya chama kimoja, utaratibu wa uchaguzi uliokuwapo ni Kamati ya Utendaji ya Tanu kuchagua watu wawili na kuwapeleka kwa wapigakura kwa ajili ya kumpata mbunge. Lakini katika nafasi ya kiti cha urais, utaratibu huo ulikuwa unamhusisha mtu mmoja aliyechaguliwa na Mkutano Mkuu wa vyama vya Tanu na ASP.  Baada ya mtu huyo kupita, alitakiwa kuthibitishwa na mkutano wa uchaguzi. Wapigakura walikuwa wanapiga kura ya ndiyo au hapana.
Mfumo huo wa uchaguzi, ndiyo uliomchagua Mwalimu Nyerere bila kupingwa katika kipindi chote cha utawala wake yaani mwaka 1965, 1970, 1975 and 1980, akiwa anashinda kwenye chaguzi hizo kwa zaidi ya asilimia 90. Mwalimu Nyerere alistaafu mwaka 1985 na CCM ikamchagua Ali Hassan Mwinyi kuwa rais. Hata hivyo, kulikuwa na mabadiliko makubwa mawili, kabla ya uchaguzi wa mwaka 1985: kuanzishwa kwa mfumo wa ukomo wa uongozi kwa nafasi ya rais na kupungua kwa umri wa mpigakura kutoka miaka 21 hadi 18.
Mwaka 1992 nchi iliingia katika mfumo wa vyama vingi. Mwaka 1995, Tanzania ikaingia rasmi kwenye uchaguzi chini ya mfumo huo wa vyama vingi, ikiwa ni miaka 33 tangu uchaguzi wa kwanza ulipofanyika mwaka 1962. Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 1995, CCM ilimteua Benjamin William Mkapa na akashindana na watu watatu kutoka vyama vya upinzani: Augustine Mrema aliyekuwa anakiwakilisha Chama cha NCCR- Mageuzi. Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF na John Cheyo wa UDP. Katika uchaguzi huo Mrema ndiye aliyeonekana tishio kwa CCM, lakini mwishoni Mkapa alishinda uchaguzi huo kwa kupata wa asilimia 61 ya kura zilizopigwa na Mrema alipata asilimia 27.
Miaka mitano baadaye, Mkapa alishinda tena kwa asilimia 71, akifuatiwa na Profesa Lipumba aliyepata asilimia 16, NCCR haikusimamisha mgombea katika uchaguzi huo na Mrema ambaye wakati huo alikuwa ametoka NCCR na kujiunga na Chama cha Tanzania Labour (TLP) alipata asilimia saba.
Mwaka 2005 CCM ikamteua Jakaya Kikwete kuwa mgombea wake wa urais na alishinda kwa asilimia 80, akifuatiwa na Profesa Lipumba aliyepata asilimia 11. Rais Kikwete alifanikiwa kutetea nafasi yake hiyo mwaka 2010 alipopata asilimia 62, akifuatiwa na Dk Willibroad Slaa wa Chadema ambaye alikuwa wa pili baada ya kupata asilimia 27.
Mwaka huu, Watanzania wanaingia tena katika Uchaguzi Mkuu unaovishirikisha vyama vingi tena kukiwa na ushirikiano wa baadhi ya vyama vya upinzani.
Chanzo:Mwananchi
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa