Home » » UWANJA WA NDEGE SINGIDA NI 'JIPU' NANI WA KULITUMBUA?

UWANJA WA NDEGE SINGIDA NI 'JIPU' NANI WA KULITUMBUA?

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
mfanyakazi  wa  kikosi  cha zimamoto na uokozi katika  uwanja  wa  ndege wa mkoa wa Singida akijiandaa  kwa kukifanyia majaribio  kifaa chake  cha  kuzimia moto wakati  ndege  iliyombeba balozi wa China nchini Dr  Lu Yong,ng ikiwasili katika  uwanja  huo jumapili ya May 29 wakati wa  ziara  yake wilayani Iramba
Hapa mfanyakazi  huyo akiwa pekee yake  huku akifanya kazi  tatu kwa  wakati mmoja kuelekeza ndege  hiyo ,kushika kifaa cha  kuzimia moto iwapo  hitirafu  itajitokeza na tatu kuweka gogo kwenye taili la ndege  baada ya kutua
Hapa  akielekea  kuelekeza eneo la  kutua
Hapa  akimwelekeza rubani wa  ndege hiyo huku  kulia kifaa kinachotumika kama gari la zimamoto na uokozi likiwa limeegeshwa kulia
Hapa  anakamilisha  kuelekeza eneo la  kutua anajiandaa kurudi  kuchukua kigogo kwenye gari  hili maalum ambalo kweli  bado mamlaka  ya  viwanja  vya ndege  vinapaswa  kulitazama   hili pasipo kusubiri majanga  ili  kuunda tume ya uchunguzi wa kitakachotokea
Ndege  ikiwa  imetua huku kifaa kinachotumika kama  gari la zimamoto na uokozi  kikiwa pembeni na mhudumu wa kifaa hicho  kushoto
Rubani  akimtazama  mfanyakazi  huyo mmoja anayefanya kazi  tatu kwa  wakati mmoja katika  uwanja wa ndege Singida
Hapa  akielekea  kuweka kigogo kwenye ndege  ushauri  wetu matukiodaimaBlog kwanza kwa kamati ya  ulinzi na usalama mkoa  wa Singida  kulitazama suala   hili la kiusalama kwa jicho la tatu kwani hatuombi jambo basi kutokea  ila ni  vema kinga  kuliko  tiba ,pili uongozi wa kiwanja  hicho  cha ndege kuongeza  wafanyakazi na hata  kuomba gari la kisasa katika uwanja  huo , tatu wizara  husika  kulitazama   hili na mwisho uongozi wa viwanja vya ndege nchini kutoka ofisini na kuzungukia  viwanja  vyote kikiwemo  hiki  cha Singida kuangalia changamoto  zake vinginevyo hili ni  jipu sasa ni nani wa  kujitolea  kulitumbua ?

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa