SHUKRANI ZA FAMILIA YA MAREHEMU MOHAMED MTATURU MKONONGO


Marehemu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongoenzi za uhai wake
 

Familia ya marehemu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo na mkewe Bi. Naiz Edriss Mavura pamoja na familia ya Mama Amina Mtaturu, Mheshimiwa DC Miraji Jumanne Mtaturu na Mzee Salum Chima; tunapenda kuwashukuru ndugu, jamaa na marafiki wote kwa upendo na faraja mliyowapatia na kwa kushiriki kwenu kikamilifu katika kufanikisha maziko ya mpendwa wetu, Ndugu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo (pichani), ambaye aliitwa na Mungu alhamisi, 21 Julai 2016 saa 1:40 asubuhi, kwa ajali ya gari.

Singida yazindua huduma tembezi za madaktari bingwa

 
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe amezindua huduma tembezi za madaktari bingwa humo na kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo za kibingwa.

Huduma zilizozinduliwa Wilayani Iramba katika hospitali ya Kiomboi zitahusisha huduma za za upasuaji, meno, macho, upasuaji wa mifupa, huduma za kibingwa za magonjwa ya watoto, wanawake na huduma za mionzi.

Mhandisi Mtigumwe amesema matarajio ya mkoa huo ni kuwa huduma tembezi za kibingwa zitasaidia kutambua na kutibu magonjwa mbalimbali kabla hayajafikia hatua ya usugu na kupunguza gharama za rufaa za wagonjwa kwenda nje ya mkoa.

“Huduma tembezi za kibingwa zitawasaidia wananchi kutambua uwepo wa huduma za kibingwa katika mkoa wa singida na kupata matibabu kwa gharama nafuu” alisema Mhandisi Mtigumwe.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. John Mwombeki akisoma taarifa ya hali ya afya Mkoa wa Singida amesema wazo la kuanzisha huduma tembezi za kibingwa limetokana na idadi kubwa ya operesheni zilizofanyika kwa mwaka 2015/2016 na pia mkutano wa wadau wa afya mkoani hapa kuafiki wazo la kuanzisha huduma hiyo.

"Kwa kipindi cha mwaka 2015/2016  jumla ya operesheni kubwa na ndogo 4,836 zimefanyika katika hospitali mbalimbali mkoani hapa, aidha Idara ya macho katika hospitali ya Mkoa imefanya jumla ya operesheni kubwa na ndogo 2,020" ameongeza Dkt. Mwombeki.

Dkt. Mwombeki amesema uwepo wa madaktari bingwa 11 mkoani Singida pia umekuwa chachu ya utekelezaji wa huduma hiyo huku Mkoa ukifanya jitihada za kuazima madaktari wengine katika mikoa jirani ya Dodoma na Manyara.

Baadhi ya wagonjwa waliohudhuria katika siku ya kwanza ya zoezi hilo huku huduma hiyo ikitarajiwa kufanyika kwa muda wa siku tano wilayani hapo wameeleza shauku na furaha yao ya kusogezewa huduma za kibingwa katika halmashauri zao.

"Nilikuwa naumwa jino ambalo limeota vibaya, niliambiwa nitaweza kufanyiwa operesheni katika hospitali kubwa kama Muhimbili lakini hawa madaktari wametusaidia , nimepata huduma haraka na kwa gharama nafuu, nawasihi wenzangu waje kwa wingi" amesema Bi Neema Josseph Mkazi wa Kijiji cha Kizaga Wilayani Iramba.

 Naye Mzazi wa mtoto Jonas Masaka amesema huduma za kibingwa zitamsaidia mtoto wake mwenye matatizo ya macho na hiyo kumpunguzia gharama ya kumpeleke katika hospitali kubwa kutibu tatizo la macho linalomsababisha mtoto huyo kushindwa kusoma vizuri.

Huduma  ya tembezi za kibingwa Mkoani Singida zitafanyika katika Wilaya zote tano za Mkoa nwa Singida na hvyo kupunguza wagonjwa wa rufaa watakaopelekwa hospitali za Bugando, KCMC na Muhimbili.

DC MTATURU AKEMEA SIASA TAKA ZINAZOCHANGIA KURUDISHA NYUMA MAENDELEO YA WANANCHI

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na watumishi wa Hospitali ya
Malkia wa Ulimwengu iliyopo Kijiji na Kata ya Puma
Dc Mtaturu akizungumza na viongozi wa ngazi ya juu katika Hospitali Teule ya Wilaya ya ikungi Makiungu mara baada ya kuwasili katika Hospitali hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akikagua jengo jipya linalojengwa kwa ajili ya wodi na baadhi ya Ofisi za Hospitali ya Malkia wa ulimwengu
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa  Hospitali ya Malkia wa ulimwengu, Na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Wilaya

DC MTATURU AMALIZA MGOGORO KATI YA MWEKEZAJI NA WANANCHI


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mang’onyi wakati wa kutatua mgogoro kati ya wananchi na muwekezaji Shanta Gold Mine
Wanachi Kijijini Mang’onyi wakisikiliza kwa makini maelezo ya Mkuu wao wa Wilaya
Baadhi ya viongozi wakisikiliza maelezo ya awali katika ufunguzi wa mkutano huo uliodumukwa zaidi ya masaa matatu
Dc Mtaturu akikemea tabia ya wanasiasa kutoa matamko ya kisiasa kwa maslahi yao binafsi huku wakiwa mbali na eneo la wawakilishi wao

DC MTATURU: SERIKALI IPO TAYARI KUCHUKIWA NA WAVIVU

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mirajji Jumanne Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki.
Mkurugenzi wa Taasisi inayojihusisha na kupunguza umasikini na kutunza mazingira nchini Tanzania (APEC), Respicius Timanywa akiwashukuru washiriki wote wa mafunzo hayo
Dc Mtaturu (Kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa APEC Respicius Timanywa zawadi ya kuku iliyotolewa na wahitimu wa mafunzo hayo

KUMEKUWA NA MATUMIZI MABAYA YA DEMOKRASIA KATIKA WILAYA YA IKUNGI




Na Mathias Canal, Singida

Ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo kwa kutumia nguvu na akili katika kukamilisha na kumiliki miradi ya kijamii imetajwa kuwa njia mojawapo itakayowafanya wananchi kuwa na uchungu na mali pamoja na maendeleo ya katika jamii husika.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu amesema kuwa kumekuwa na matumizi mabaya ya demokrasia katika Wilaya hiyo hususani katika shughuli za kijamii kama vile kuchangia ujenzi wa maabara jambo lililopelekea Wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika ujenzi wa maabara kwa ajili ya shule za sekondari zilizopo katika Wilaya ya Ikungi.

WAKUU WA IDARA WILAYANI IKUNGI, MAAFISA TARAFA, WATENDAJI WA KATA, VIJIJI NA WENYEVITI WA VIJIJI WAFUNDWA

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akiwasilisha mtazamo wa namna ambavyo anataka Wilayahiyo iwe

'Kupanda bodaboda bila helmeti ni kudhamiria kujiua'



Kutovaa helmeti kwagharimu maisha ya wapanda bodaboda Baadhi wapata ulemavu wa kupoteza kumbukumbu Polisi watangaza kiama kwa wasiovaa helmeti Na Shadrack Sagati BRUNO Sigala (24) amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI) kwa miezi mitatu tangu alipoanguka na bodaboda mkoani Singida.
Katika ajali hiyo alivunjika mikono yote, mguu moja na alitikisika ubongo na sasa hana kumbukumbu. Ingawaje huu ni mwaka 2016. Lakini Sigala kwa kukosa kumbukumbu, anasema ni mwaka 2018.
Hali kadhalika, wakati amelazwa wodini hapo kwa takribani miezi mitatu hadi sasa, yeye anadai kwamba ana miaka mitano tangu afikishwe katika wodi hiyo ya wagonjwa wa mivunjiko! Wauguzi wanaomhudumia wanaeleza kuwa Sigala anasubiri kufanyiwa upasuaji wa mikono na mguu baada ya kuhamishwa kutoka katika wodi inayoshughulika na majeraha ya kichwa.
"Alipoanguka na bodaboda aliumia vibaya kichwani, migugu pamoja na mikono. Alipofikishwa hapa madaktari waliangalia kipaumbele kwanza ni ubongo, baada ya kupata ahueni katika majeraha yake ya kichwa ndipo alipohamishiwa katika wodi hii ili aendelee na matibabu ya miguu na mikono," anasema Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi.
Bruno Sigala ni kielelezo cha waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda ambao wanaanguka na kuumia vibaya kichwani kutokana na kutovaa kofia ngumu ya kinga yaani helmeti kwa kimombo.
Kijana huyo alikuwa anafanya biashara ya kubeba abiria kwa pikipiki na aligongwa na gari katika ajali iliyomfikisha Muhimbili. Katika ajali hiyo, Sigala aliumia kichwani, akajing’ata ulimi na kuvunjika mikono yote na mguu mmoja. Akijieleza kwa kubabaisha anakiri kuwa hakuwa amevaa kofia wakati anaendesha pikipiki.
"Sikuwa najua umuhimu wa kofia hiyo, kwani mafunzo yenyewe ya kuendesha nilijifunzia tu mitaani, nikaanza biashara ya kubeba abiria."
Kofia ngumu zimetengenezwa kwa lengo la kumlinda mwendesha bodaboda asiumie kichwa pale apatapo ajali. Baadhi ya kofia hizi zinatengenezwa zikiwa na sehemu ya kupitishia hewa, kufunika uso usiathirike kwa kioo maalumu ambacho hata kikivunjika hakileti madhara kwa mvaaji pamoja na kulinda masikio.
Mwendesha pikipiki yuko hatarini kupoteza maisha pale apatapo ajali kama hakuvaa kofia ngumu. Tafiti zinaonesha kuwa kofia ngumu hupunguza hatari ya mwendesha pikipiki kuumia kichwa pale apatapo ajali kwa asilimia 69 na inapunguza kifo kwa asilimia 42.
Takwimu zilizopo katika Taasisi ya Mifupa (MOI) ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambazo zinahusisha miezi sita, Machi 15 hadi Septemba 15, 2011, zinaonesha kwamba wapanda bodaboda wengi wanaojeruhiwa vibaya pale ajali za pikipiki zinapotokea, ni wale wasiovaa helmeti.
Wengi wao wanajeruhiwa vibaya kichwani. Daktari bingwa wa Magonjwa ya Mifupa katika Taasisi ya MOI, Dk Bryson Mcharo, anasema katika utafiti wake wa miezi 6 ukihusisha majeruhi wapatao 722, amebaini kuwa nusu ya majeruhi hao walipanda pikipiki bila kuvaa helmeti.
"Katika utafiti huo nilibaini kuwa madereva pikipiki ambao wanaona umuhimu wa helmeti ni wale ambao angalau wamepitia mafunzo ya udereva na wana leseni, lakini wengi wa majeruhi ambao hawakuvaa kofia hawana leseni na pia hawana mafunzo ya kuendesha pikipiki,” anaeleza Dk Mcharo.
"Karibia nusu ya majeruhi hao, asilimia 46, waliumia kichwani jambo linaloonesha kwamba madereva wengi na abiria wao hawazingatii uvaaji wa helmeti," anasema Dk Mcharo.
anasema kati ya majeruhi hao madereva wa pikipiki ndio wengi na zaidi ya nusu, asilimia 51.8, hawakuvaa helmeti.
Kwa mujibu wa Dk Mcharo, nusu ya majeruhi hao, walipata ajali baada ya kugongana au kugongwa na magari na asilimia 7 waligongana kati ya pikipiki na pikipiki huku asilimia 27 ni majeruhi waligongwa na pikipiki.
Mkuu wa Kitengo cha Dharura katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk Juma Mfinanga, anasema mwaka 2015 walipokea majeruhi 8,400 waliotokana na ajali za barabarani kiwango ambacho ni asilimia 61 ya majeruhi wote wa ajali waliofikishwa katika kitengo hicho.
Dk Juma anafafanua kuwa kati ya majeruhi hao asilimia 71 walikuwa ni madereva, asilimia 46 walikuwa ni abiria wakati asilimia 39 walikuwa ni waenda kwa miguu. Anasema kwa mwaka huu kuanzia Januari hadi Julai pekee, majeruhi wa pikipiki waliofikishwa kwenye kitengo hicho ni 4,900 kiwango ambacho ni sawa na asilimia 64 ya majeruhi wote wa ajali za barabarani.
Anasema nusu ya ajali hizo (asilimia 51) ni majeruhi waliotokana na ajali za pikipiki, huku idadi ya wanaume ni mara tatu ya wanawake ya majeruhi wote waliofikishwa hospitalini hapo.
Dk Juma anasema majeruhi walioumia kichwani walikuwa ni asilimia 42 na kati ya hao asilimia 8 hadi 10 ni wagonjwa waliojeruhiwa vibaya na kupona kwao ni kwa kudra za Mwenyezi Mungu, huku asilimia 85 hadi 88 ni wale ambao wameumia kwa kiwango cha kati na asilimia 61 ya majeruhi hao walivunjika mifupa mirefu ambayo ni mikono na miguu.
Majeruhi waliohamishiwa katika taasisi ya mifupa ni asilimia 89.1 ya majeruhi wa pikipiki waliopokelewa kituoni hapo mwaka 2015. Kuhusu gharama, Dk Juma anasema gharama zinatofautiana kulingana na hali ya mgonjwa, lakini akasema kwa wastani hospitali inatumia zaidi ya Sh 650,000 kwa mgonjwa mmoja anayefikishwa katika kitengo cha tiba ya dharura kwa ajili ya kumtibia wakati wa dharura.
Uvaaji wa helmeti kwa dereva na abiria wa pikipiki ni moja ya masharti yaliyowekwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) wakati wa kutoa leseni kwa dereva wa pikipiki.
"Lazima awe na helmeti na abiria wake pia atatakiwa kuvaa kofia ya kujikinga wakati wote na kwamba kofia hiyo inatakiwa kuwa na alama ya eneo la utoaji huduma ya usafiri," inasema kanuni ya usafirishaji ya pikipiki za magurudumu mawili na matatu ya mwaka 2010.
Kanuni hiyo inatoa masharti kwamba dereva wa pikipiki ya magurudumu matatu kwamba haruhusiwi kubeba idadi ya abiria zaidi ya mmoja, dereva wa pikipiki anatakiwa kuvaa kofia ngumu ya kujikinga wakati wote yeye na abiria wake.
Lakini jambo hilo halifanyiki. Pikipiki nyingi zinazobeba abiria zinatisha, unaweza kukuta dereva na abiria wake hawajavaa helmeti, au dereva anayo lakini abiria hana. Wakati mwingine unaweza kukuta dereva kavaa na abiria kaishikilia mkononi au kuipakata.
Hili limechangia dereva na abiria kupoteza maisha pindi inapotokea ajali.
Hili ndilo limemfanya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kutahadharisha kwamba kupanda pikipiki bila kuvaa kofia ngumu ni dhamira ya kujiua, kwa sababu dereva na abiria wakipata ajali ni rahisi kupoteza maisha kwa kupigiza kichwa chini.
Makonda anawataka madereva wa bodaboda na abiria wao kuvaa helmeti. “Nimeshawasiliana na kamati yangu ya usalama barabarani mkoa. Hili nitalisimamia kikamilifu lazima wote wawe na helmeti,” anasema Makonda.
Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Barabara wa Sumatra, Johansen Kahatano, anasema sheria ya Sumatra ya pikipiki inamtaka dereva wake avae helmeti wakati wote, kushindwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria kwa makusudi. Kuhusu madai ya abiria kutopenda kuvaa hizo kofia, Kahatano anasema kwamba amekuwa anawashauri waendesha pikipiki wasipakie abiria ambao hawataki kuvaaa kofia ngumu.
"Usimamizi ni mgumu. Lakini tunaendelea kutoa elimu kwamba abiria akipanda pikipiki aone umuhimu wa kuvaa helmeti na kuthamini maisha yake. Hilo ni jambo la lazima. Sisi kama mamlaka tuna kazi ya kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuvaa kofia ," anasema Kahatano.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, hataki kumung’unya. Uvaaji wa kofia ngumu helmeti kwa waendesha pikipiki na abiria wao ni lazima. Yule ambaye atakaidi agizo hilo atakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria. Itaendelea kesho. Inserts "Karibia nusu ya majeruhi hao, asilimia 46, waliumia kichwani jambo linaloonesha kwamba madereva wengi na abiria wao hawazingatii uvaaji wa helmeti" “Majeruhi walioumia kichwani walikuwa ni asilimia 42 na kati ya hao asilimia 8 hadi 10 ni wagonjwa waliojeruhiwa vibaya na kupona kwao ni kwa kudra za Mwenyezi Mungu.” “Kupanda pikipiki bila kuvaa kofia ngumu ni dhamira ya kujiua, kwa sababu dereva na abiria wakipata ajali ni rahisi kupoteza maisha kwa kupigiza kichwa chini.”

Chanzo Gazeti la Habari leo

DC MTATURU ATENGA SIKU YA JUMAPILI KUKAGUA SHUGHULI ZA MAENDELEO

 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akisisitiza jambo katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo Wilayani humo
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa