Singida watakiwa kuchangamkia Soko la Hisa

 WAJASIRIAMALI na wafanyabiashara mkoani Singida wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo Soko la Hisa la Dar es Salaam ili kuboresha na kuendeleza biashara zao.
Mwito huo ulitolewa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone wakati akifungua semina ya siku mbili juu ya Soko la kukuza ujasiriamali iliyofanyika ukumbi wa Aqua Vitae mjini hapa.
Dk Kone alisema kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam kupitia kitengo chake kipya kijulikanacho kama “Soko la Kukuza Ujasiriamali”, ni suluhisho la upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali kote nchini.
Alisema kuwa soko hilo litatoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili wajasiriamali katika upatikanaji wa uhakika wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo limekuwa likiwasumbua wajasiriamali na wafanyabiashara.
“Kwa hiyo basi, soko la kukuza ujasiriamali litasaidia kuleta msukumo wa utekelezaji sera mbalimbali za serikali zinazolenga kuondoa changamoto hizo na kuleta urahisi wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukuza biashara zao,” Dk Kone alisema.
Aidha, alieleza kuwa soko hilo linatarajiwa kulichangamsha soko kwa ujumla kupitia ongezeko la utoaji na uorodheshaji wa hisa, kupanua wigo na fursa za kuwekeza mitaji na kuongeza ari ya wananchi kujiwekea akiba.
Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa huo, baadhi ya faida ziletwazo na soko hilo ni kupunguziwa kodi katika gawio, kusamehewa kodi kwenye ongezeko la thamani ya mtaji na ushuru wa stempu na punguzo kodi ya makampuni.
Chanzo;Habari Leo

Wavamia nyumba, wazichoma moto

MWENYEKITI wa Kijiji cha Makunda, Kata ya Kyengege, wilayani Iramba kwa kushirikiana na watu wengine zaidi ya 50 wamevamia na kuchoma moto nyumba mbili za wakulima wakipinga kuwa si wazaliwa wa eneo hilo na kujipatia ardhi zaidi ya ekari 285.
Habari za uhakika kutoka katika eneo la tukio hilo zinaeleza tukio hilo limetokea juzi, saa 8:00 mchana katika mashamba ya kilimo Kijiji cha Makunda.
Kwa mujibu wa habari hizo, siku ya tukio watuhumiwa wakiwa na silaha za jadi walivamia makazi ya mkulima mwezao, Esau Talanzia (47) na kuchoma moto nyumba yake.
Pia walichoma magunia sita ya mahindi, magunia mawili ya alizeti godoro moja, fedha taslimu sh 450,000 na vitu vingine vilivyokuwemo, vyote vikiwa na thamani ya sh milioni 1.8.
Pia katika tukio hilo nyumba moja ya Matayo Kizaberga, mkulima na mkazi wa Makunda-Mbugani ilichomwa moto na vitu vyote vilivyokuwemo kuteketea.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu 25 akiwamo mwenyekiti wa kijiji wanashikiliwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.
Kamanda Kamwela alisema chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mashamba ambapo wanakijiji cha Makunda wanapinga waathirika hao kumiliki ekari 284 wakati si wazawa wa eneo hilo.
Alisema watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
Chanzo;Tanzania Daima

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu watakiwa kufika kijiji cha Kazamoyo


unnamed
Baadhi ya wananchi wakiwa wamehamishia makazi yao chini ya mti uliopo kwenye korongo kijiji cha Handa mpakani mwa Wilaya ya Chemba na Singida Vijijini mara baada ya nyumba zao kuchomwa moto na askari polisi na wale wa kikosi cha kupambana na ujangili kwa madai ya kuvamia hifadhi ya msitu wa mgori (PICHA NA HILLARY SHOO).
watoo

 Huyu ni mmoja wa watoto walionashwa na kamera yetu akiwa amelala hoi kwa kukosa chakula na huduma zingine, baada ya nyumba zao kuchomwa moto wakati wa operesheni ya kuwahamisha katika kitongoji cha Kazamoyo kwa madai ya kuvamia hifadhi, hata hivyo wananchi hao wameisha katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka nane toka mwaka 2005 , lakini sheria ya kuingiza eneo hilo kwenye msitu wa hifadhi ya mgori ilifanyika mwaka 2007, (PICHA NA HILLARY SHOO).
.Unyanyasaji dhidi ya wananchi wakithiri wilayani Singida
Na Hillary Shoo, Singida
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wametakiwa kufika katika kitongoji cha Kazamoyo kijiji cha Nguamuhanga tarafa ya Mgori Wilayani Singida vijijini na kujionea unyanyasaji dhidi ya wananchi wakati wa zoezi la kuwaondoa katika hifadhi ya msitu wa mgori.
Hayo yamesemwa juzi katika kitongoji hicho na baadhi ya wananchi walioamua kuhamia kwenye korongo na kuishi chini ya miti kama digidigi kunusuru maisha yao kutokana na vipigo kutoka kwa wa kikosi cha kupambana na ujangili Wilaya ya Singida na askari polisi.
Wamesema ni vyema kituo hicho wakafika mapema ili kuona jinsi ambavyo binadamu wanavyoishi maisha ya shida ta taabu kwenye eneo hilo kufuatia amri ya mkuu wa Wilaya ya kuhamisha kwa muda mfupi.
Wamesema eneo hilo wameishi zaidi ya miaka nane na kujenga makazi bora bila matatizo yoyote, lakini jambo la ajabu ni baada ya Wilaya ya Chemba na Sngida kuwekeana mipaka na kuonekana kuwa wako Singida.
“Wakati tuko kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba, tuliishi bila matatizo lakini baada ya kuhamia singida ndipo mambo yalianza kubadilika na kuambiwa kuwa tuko eneo la hifadhi, hii ni ajabu sana , Wilaya moja tuliishi vizuri hii nyingine haitutaki sasa tuende wapi.” Alihoji mmoja wa kina mama.
Licha ya kukosa huduma muhimu kama vile maji, mahema, vyoo baadhi ya kina mama na watoto walionekana wakiwa katika huzuni klubwa huku wengine wakiangua vilio baada ya kuwaona waandishi wa habari wakidhani kuwa ni askari.
Hata hivyo eneo hilo lina mbu wengi, jua kali na mbaya zaidi hivi sasa ni msimu wa mvua katika maeneo hayo, je swali la kujiuliza wataishije hapo wananchi hao zaidi ya 1,000 ambao nyumba zao zimechomwa moto.
Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Singida Qeen Mlozi amesema zoezi hilo linaendelea sanjari na kuhakikisha wanaondoka kwenye korongo hilo walimojificha.
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alitembelea eneo hilo la kusitisha zoezi la kuwahamisha mpaka pale kamati ya kudumu ya huduma za kijamii ya baraza la madiwani watakapokutana kutoa maamuzi sahihi juu ya wananchi hao.
Hata hivyo agizo hilo la Naibu Waziri limepingwa vikali sana na mkuu wa Wilaya ya Singida Mwalimu Qeen Mlozi kwamba Nyalandu hana mamlaka kisheria ya kusitisha zoezi hilo, na kwamba anayeweza kumwamuru kusitisha zoezi ni Mkuu wa Mkoa pekee na si vinginevyo.
Na Mo Blog



SINGIDA SASA YAJA NA MKAKATI WA KUIBUKA KIRIADHA



                             Picha zote kutoka maktaba ya Singida Yetu Blog

SINGIDA ni moja kati ya mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika mchezo wa riadha miaka ya 1980 na kutoa wanariadha mahiri ambao waliiwakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Mkoa huo ni wenye mandhari nzuri yenye mawe mawe pamoja na mto upande wa kushoto na kulia hususan pale unapofika mkoani hapo.
Hakika mkoa huu ni wenye vitu vingi, lakini kikubwa zaidi ni wakimbiaji wa riadha hususan maeneo ya Singida Vijijini ambako kama wakimbiaji hao wataweza kupewa vifaa maalumu kwa ajili ya kukimbia na wadau wa riadha wakajitokeza na kuchangia zaidi katika riadha, Tanzania itakuwa na medali nyingi na kupata heshima katika nchi mbalimbali duniani.
Nasema hivyo kwa sababu hivi karibuni Mbunge wa Singida Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliandaa mashindano ya riadha hususan vijijini kwa ajili ya kuibua vipaji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Shrika la African Wildlife Trust (AWT), Pratic Patel.

Mbio hizo zilizojulikana kwa jina la Singida Marathon za kilometa 21, zilianza rasmi Novemba 9, mwaka huu kwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 400 kutoka Singida Mjini na Singida Vijijini na zilianzia Kijiji cha Mitula, Kata ya Kinyagigi na kuishia Viwanja vya Shule ya Msingu Ntunduu (W) Singida Vijijini.
Mbio hizo zilikuwa za kilometa 21 ambazo ni nusu marathoni na kilometa 5 na mwisho kabisa ni kilometa 2.5 ambazo ziliwashirikisha watoto wa kiume na wa kike. Wakimbiaji walikuwa wamejiandaa wenyewe na walijiandikisha, lakini baadhi yao pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa viatu, lakini waliweza kumudu hali hiyo kutokana na mazingira waliyokua nayo na kuonesha vipaji vyao vilivyowashangaza wengi.

Inawezekana kukimbia bila viatu ni jambo lisiloruhusiwa, lakini kutokana na mazingira yenyewe ya vijijini hali hiyo haikuwa kikwazo kwa wakimbiaji hao kukimbia bila viatu ila walionesha kuwa wana moyo na nia ya dhati kuonesha vipaji vyao hakika ilikuwa faraja kubwa kwao kwani mwisho wa siku waliweza kuibuka washindi na wengine wakapata kifuta jasho.

Washindi hao ni Paulo Itambi ambaye aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ambaye alipewa zawadi ya Sh 300,000, Emmanuel Samson wa pili (Sh 200,000) na Samwel Ikungi wa tatu (Sh 100,000). Kwa upande wa wanawake, mshindi wa kwanza Fabiola William (Sh 300,000), Zakia Abdallah (Sh 200,000) na Winfrida Hassani (Sh 100,000).
Mbio za kilometa tano, washindi ni Gabriel Garado (Sh 200,000), Deo Lazaro (Sh 100,000) na Jonas John (Sh 50,000) huku wanawake ni Neema Kisuda (Sh 200,000), Pascalina Silvesta (Sh 100,000) na Christina Yuda (Sh 50,000) ambao washindi wa kilometa 2.5 wakiwa ni Julita Antony (Sh 100,000), Editha Gabriel (Sh 50,000) na Magreth Bernado (Sh 25,000).
Wanaume walikuwa ni Petro Pascal mshindi wa kwanza na kupewa Sh 100,000, Baraka Sebastian (Sh 50,000), Haji Swalehe (Sh 25,000) huku washindi wengine 400 kila mmoja akipewa Sh 10,000. Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Naibu Waziri Nyalandu, alikabidhi pia medali mbalimbali kwa washindi hao.

Aidha, alitoa changamoto kwa
wananchi hao kuacha tabia ya kuua tembo, bali wanastahili kulindwa na kuhifadhiwa ili kukuza uchumi na kufungua milango ya ajira.
Hata hivyo, baadhi ya washindi walimshukuru Nyalandu kwa kuamua kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua vipaji na kutoa rai kwa wadau wa riadha mkoani humo pamoja na sehemu mbalimbali kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuendeleza vipaji na kuibuavipaji vipya.

Fabiola ambaye ni mkimbiaji mashuhuri wa riadha na aliyeiletea sifa Tanzania, alisema awali alikuwa akikimbia mkoani Kilimanjaro, lakini hivi sasa yupo Singida ambako alihamia Singida Vijijini kwenye Jimbo la Nyalandu, ndio kwao alipozaliwa na anaona fahari kubwa kuona wilaya hiyo ina wakimbiaji wengi na ni wazuri, lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa kwa ajili ya kufanyia mazoezi.

Fabiola na wadau wengine wamemwomba Naibu Waziri pamoja na wadau wengine kushirikiana kwa pamoja ili kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuibua vipaji vya wakimbiaji waliopo maeneo ya vijijini.

Alisema mkoa huo una wanamichezo wengi, lakini hakuna klabu za michezo hali inayosababisha baadhi ya wanariadha kufanya mazoezi bila ya kuwa na vifaa maalumu, lakini walimpongeza Nyalandu kwa kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua wanamichezo wengi watakaoweza kuutangaza mkoa huo pamoja na Tanzania kwa ujumla pale yanapotokea mashindano ya riadha ya ndani na nje ya nchi.
KWA HISANI YA SINGIDA YETU BLOG


Kung’olewa kwa Zitto, Mkumbo: Chadema mikoani watofautiana

Wanachama wa Chadema mikoa mbalimbali nchini pamoja na wananchi wametoa maoni tofauti kuhusu uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho wa juzi kuwavua uongozi viongozi wake watatu; Naibu Katibu Mkuu wake Zitto Kabwe na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo na mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Singida
Kutoka mkoani Singida, uongozi wa chama hicho  jana ulifanya kikao cha faragha kujadili uamuzi wa chama hicho, huku baadhi ya wananchi wakiuelezea uamuzi  huo kuwa umetokana na pupa na kushindwa kuvumiliana, wengine wakitishia kujitoa katika chama hicho.
Kwa zaidi za saa 5 uongozi huo ulikuwa ukijadili hatua hiyo huku ukiahidi kutoa taarifa yake baada ya kikao hicho kilichokuwa kikiendelea hadi baada ya saa 7 mchana.
Habari zaidi kutoka Wilaya ya Iramba mkoani humo zinasema kuwa wanachama wa Chadema wilayani humo wametishia kurudisha kadi za chama hicho kilichokuwa kimeanza kujizolea umaarufu wakisema watafanya hivyo ikiwa Chadema ‘watalitosa jembe’ lao.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili walisema kuwa hatua hiyo inaweza kuipunguzia umaarufu Chadema na kwamba ustawi wa vyama vingi vya siasa unaponzwa na pupa, jazba hata kukosa uvumilivu.
“Kikundi hiki cha viongozi kinasababisha Chadema kumeguka kama tulivyosikia juzi. Kwa maoni yangu kabla hakijawavua uongozi Zitto, Dk Mkumbo na Mwigamba, kilikuwa kinashabikiwa na asilimia 90, hapa Singida, lakini baada ya tukio la juzi la kuwavua uongozi baadhi ya viongozi, nina hakika kinashabikiwa na asilimia 30 ya wananchi,” alisema Juma Mdida.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TLP Wilaya ya Singida, Athumani Nkii, alisema kuwa ustawi  wa vyama vingi vya siasa unaponzwa na vitendo vya pupa, jazba na ubinafsi wa baadhi ya viongozi wake baada ya majina yao kupata umaarufu,wakisahau kuwa umaarufu huo unachangiwa na chama husika.
“Kwa upande wa Kabwe Zitto, nadhani safari zake za nje ya nchi na suala la mapesa ya Uswisi, zitakuwa hazina baraka za Chadema. Kuhusu Dk Kitila Mkumbo, sina kabisa fununu ya madhambi yake,”alisema.
Rukwa
Barua ya kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti Chadema Tanzania Bara, Said Amour Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Mpanda imesambazwa  kwa wapiga kura wake na wananchi wa jimbo hilo ili  wafahamu sababu za msingi za yeye kujiondoa katika nafasi yake.
Katibu wa mbunge huyo, Joseph Mona, alipata taarifa za uamuzi huo wa ghafla, aliosema kuwa ni sahihi.
Chanzo;Mwananchi


KATA YA MTAMAA MANISPAA YA SINGIDA YAPATA NEEMA YA UMEME.


Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala 
(Picha Kutoka Maktaba Yetu)

Kata ya mtamaa manispaa ya Singida inatarajiwa kuunganishiwa nishati ya umeme wa grid wa taifa kupitia mradi wa umeme vijijini REA ili kukabiliana na umasikini wa kipato kwa wananchi wa kata hiyo.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala wakati akizungumza na wananchama wa CCM katika kata hiyo ambapo amesema upembuzi yakinifu juu ya mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu.
Amesema kuwa endapo umeme ukiunganishwa katika kata hiyo kutasaidia wananchi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ambazo zinategemea nishati hiyo na hatimaye kuondokana na umasikini wa kipato unaowakabili wakazi wa kata hiyo
Aidha Bw Mazala ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kuonyesha nia ya kuhitaji huduma hiyo kwa kujiandikisha hali ambayo itaongeza juhudi za mradi huo wa REA kwenda kasi kutokana na mahitaji ya idadi kubwa ya watu.
Na Singida yetu Blog

SEMA yagharamia ujenzi wa Vyoo katika shule tano za Manispaa ya Singida.


Meneja wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.

Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.

 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.

 Hayo yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya msingi Unyankindi Singida mjini.

 Amesema fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.

 “Vyoo hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja huyo.

 Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI (elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote vinavyohitajika.

 Amesema serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani ya fedha zilizotumika.

 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza
kero mbalimbali zinazoikabili sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu.Vyoo hivi ni bora mno na vitakuwa vimepunguza kwa kiwango kikubwa uhaba wa vyoo katika shule zetu za msingi”,amesema Majaliwa.

 Wakati huo huo, Naibu Waziri huyo ameuomba uongozi wa halmashauri ya manispaa ya Singida kusimamia matumizi ya vyoo hivyo ili viweze kutumika kwa muda mrefu zaidi.

Chanzo: Singida yetu 

Singida na mkakati wa kuibuka kiriadha


SINGIDA ni moja kati ya mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika mchezo wa riadha miaka ya 1980 na kutoa wanariadha mahiri ambao waliiwakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Mkoa huo ni wenye mandhari nzuri yenye mawe mawe pamoja na mto upande wa kushoto na kulia hususan pale unapofika mkoani hapo.
Hakika mkoa huu ni wenye vitu vingi, lakini kikubwa zaidi ni wakimbiaji wa riadha hususan maeneo ya Singida Vijijini ambako kama wakimbiaji hao wataweza kupewa vifaa maalumu kwa ajili ya kukimbia na wadau wa riadha wakajitokeza na kuchangia zaidi katika riadha, Tanzania itakuwa na medali nyingi na kupata heshima katika nchi mbalimbali duniani.
Nasema hivyo kwa sababu hivi karibuni Mbunge wa Singida Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliandaa mashindano ya riadha hususan vijijini kwa ajili ya kuibua vipaji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Shrika la African Wildlife Trust (AWT), Pratic Patel.
Mbio hizo zilizojulikana kwa jina la Singida Marathon za kilometa 21, zilianza rasmi Novemba 9, mwaka huu kwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 400 kutoka Singida Mjini na Singida Vijijini na zilianzia Kijiji cha Mitula, Kata ya Kinyagigi na kuishia Viwanja vya Shule ya Msingu Ntunduu (W) Singida Vijijini.
Mbio hizo zilikuwa za kilometa 21 ambazo ni nusu marathoni na kilometa 5 na mwisho kabisa ni kilometa 2.5 ambazo ziliwashirikisha watoto wa kiume na wa kike. Wakimbiaji walikuwa wamejiandaa wenyewe na walijiandikisha, lakini baadhi yao pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa viatu, lakini waliweza kumudu hali hiyo kutokana na mazingira waliyokua nayo na kuonesha vipaji vyao vilivyowashangaza wengi.
Inawezekana kukimbia bila viatu ni jambo lisiloruhusiwa, lakini kutokana na mazingira yenyewe ya vijijini hali hiyo haikuwa kikwazo kwa wakimbiaji hao kukimbia bila viatu ila walionesha kuwa wana moyo na nia ya dhati kuonesha vipaji vyao hakika ilikuwa faraja kubwa kwao kwani mwisho wa siku waliweza kuibuka washindi na wengine wakapata kifuta jasho.
Washindi hao ni Paulo Itambi ambaye aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ambaye alipewa zawadi ya Sh 300,000, Emmanuel Samson wa pili (Sh 200,000) na Samwel Ikungi wa tatu (Sh 100,000). Kwa upande wa wanawake, mshindi wa kwanza Fabiola William (Sh 300,000), Zakia Abdallah (Sh 200,000) na Winfrida Hassani (Sh 100,000).
Mbio za kilometa tano, washindi ni Gabriel Garado (Sh 200,000), Deo Lazaro (Sh 100,000) na Jonas John (Sh 50,000) huku wanawake ni Neema Kisuda (Sh 200,000), Pascalina Silvesta (Sh 100,000) na Christina Yuda (Sh 50,000) ambao washindi wa kilometa 2.5 wakiwa ni Julita Antony (Sh 100,000), Editha Gabriel (Sh 50,000) na Magreth Bernado (Sh 25,000).
Wanaume walikuwa ni Petro Pascal mshindi wa kwanza na kupewa Sh 100,000, Baraka Sebastian (Sh 50,000), Haji Swalehe (Sh 25,000) huku washindi wengine 400 kila mmoja akipewa Sh 10,000. Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Naibu Waziri Nyalandu, alikabidhi pia medali mbalimbali kwa washindi hao.
Aidha, alitoa changamoto kwa wananchi hao kuacha tabia ya kuua tembo, bali wanastahili kulindwa na kuhifadhiwa ili kukuza uchumi na kufungua milango ya ajira.
Hata hivyo, baadhi ya washindi walimshukuru Nyalandu kwa kuamua kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua vipaji na kutoa rai kwa wadau wa riadha mkoani humo pamoja na sehemu mbalimbali kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuendeleza vipaji na kuibuavipaji vipya.
Fabiola ambaye ni mkimbiaji mashuhuri wa riadha na aliyeiletea sifa Tanzania, alisema awali alikuwa akikimbia mkoani Kilimanjaro, lakini hivi sasa yupo Singida ambako alihamia Singida Vijijini kwenye Jimbo la Nyalandu, ndio kwao alipozaliwa na anaona fahari kubwa kuona wilaya hiyo ina wakimbiaji wengi na ni wazuri, lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa kwa ajili ya kufanyia mazoezi.
Fabiola na wadau wengine wamemwomba Naibu Waziri pamoja na wadau wengine kushirikiana kwa pamoja ili kuanzisha klabu za michezo ya riadha ili kuibua vipaji vya wakimbiaji waliopo maeneo ya vijijini.
Alisema mkoa huo una wanamichezo wengi, lakini hakuna klabu za michezo hali inayosababisha baadhi ya wanariadha kufanya mazoezi bila ya kuwa na vifaa maalumu, lakini walimpongeza Nyalandu kwa kuanzisha mashindano hayo maeneo ya vijijini ili kuibua wanamichezo wengi watakaoweza kuutangaza mkoa huo pamoja na Tanzania kwa ujumla pale yanapotokea mashindano ya riadha ya ndani na nje ya nchi.
Chanzo;Habari Leo

CCM SINGIDA YAAGIZA WANAOVAMIA MAKAZI YA WAHADZABE WAFUKUZWE

CHAMA Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Singida kimemuagiza mkuu wa Wilaya ya  Mkalama kuwaondoa kwa nguvu wavamizi wa hifadhi ya pori la Kipamba/Munguli wanamoishi na wananchi wa jamii ya  Kabila la Wahadzabe.
Wavamizi hao kutoka mikoa ya Arusha, Manyara, Shinyanga, Simiyu na Singida, wanadaiwa kufyeka  pori  hilo na kuchoma moto kwa shughuli za kilimo  na ufuagaji, hali iliyosababisha adha kubwa kwa jamii hiyo ambayo huishi kwa kutegemea mizizi, asali, matundapori na nyama  kama chakula chao kikuu.
Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM  mkoa wa Singida Mgana Msindai baada ya kuitembelea jamii hiyo inayoshi kwenye pori lililopo umbali wa zaidi ya Km 120 kaskazini mashariki mwa mji wa Singida.
Amesema ingawa kumekuwepo na tishio la  baadhi ya  wananchi kukinyima kura chama chake kwenye  chaguzi mbalimbali iwapo  wavamizi hao wataondolewa, lakini CCM haiwezi kukubali uharibifu huo wa mazingira uendelee na wahadzabe kukosa vyakula vya asili kwa kuogopa kupoteza kura.
Kutokana na hali hiyo bwana Msindai amemtaka mkuu wa Wilaya ya Mkalama kutumisha sheria zilizopo kuwaondoa kwa  nguvu  haraka wavamizi kwenye hifadhi hiyo kabla hawajasabisha uharibifu zaidi.

Walimu mbaroni wizi wa mitihani

Shukuru Kawambwa
 
Jeshi  la Polisi mkoani Singida linawashikilia walimu wawili wa shule ya sekondari, katika Tarafa ya Kirumi, Wilaya ya Mkalama, kwa kujihusisha na wizi wa mitihani ya kidato cha nne inayoendelea nchini kote.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea kati ya saa 3:00 na saa 3:30 juzi, katika Shule ya Sekondari Nkinto, iliyopo Tarafa ya Kirumi, wilayani humo.

Alisema walimu hao wanashikiliwa kwa tuhuma za udanganyifu wa mitihani hiyo iliyohusisha masomo ya Kiswahili na Fizikia.

Aliwataja walimu wanaoshikiliwa kuwa ni Mkuu wa Shule ya Nkinto, Monica Sebastian (30), na Agaloslo Otieno (32), ambao wote ni walimu wa shule hiyo.

Alisema mwalimu Otieno alikuwa msimamizi wa  mitihani kwenye Shule ya Sekondari ya Mwangeza, lakini alitumia simu yake ya kiganjani kuandika maswali na kumtumia mwalimu wake mkuu aliyemwacha katika kituo chake cha kazi (Nkinto).

Kamwela alisema baada ya Mwalimu Monica kupokea maswali hayo, alianza kuyapatia majibu kisha anapiga kambi kwenye moja ya choo cha shule yake.

Alisema baadhi ya wanafunzi waliomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda kujisaidia chooni na kwamba, walipokuwa wakifika walipewa majibu sahihi ya somo husika.

Kamwela alisema polisi walipata taarifa hizo kutoka kwa raia wema na kuandaa mtego, ambao ulimnasa Monica.
Alisema simu yake ilipochunguzwa, ilionekana kuwa na maswali hayo yaliyotumwa kutoka katika simu ya Mwalimu Otieno, aliyekuwa msimamizi wa mitihani kwenye shule nyingine.

Kutokana na hali hiyo, Kamwela alisema walimu hao watapandishwa kizimbani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika.
 
CHANZO: NIPASHE

WAJASILIAMALI TANGAZENI BIDHAA ZENU KUPITIA VYOMBO VYA HABARI!


DSC04183
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akizungumza kwenye hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ufugaji bora nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Kulia ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende.
DSC04172
Meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende akitoa taarifa yake kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Wa pili kulia (aliyeketi) ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
DSC04180
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akimkabidhi mfugaji wa nyuki cheti cha kumaliza mafunzo ya ufugaji bora nyuki yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Singida.
DSC04188
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,(aliyeketi katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafugaji Nyuki waliohitimu mafunzo ya ufugaji bora wa Nyuki.Wa kwanza kushoto (walioketi) ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende na kulia ni mwenyekiti wa wafugaji Nyuki (jina halikuweza kupatikana).(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
Serikali wilayani Singida, imewahimiza wajasiriamali na wafanyabiashara kujenga utamaduni wa kutangaza bidhaa zao kwenye vyombo vya habari ili pamoja na mambo mengine, waweze kujipatia soko la uhakika.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Wilaya hiyo Queen Mlozi,wakati akizungumza kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki na uchakataji wa asali.
Akifafanua amesema ushindani mkubwa wa biashara uliopo hivi sasa,mfanyabiashara atakayefanikiwa ni yule tu ambaye atatangaza biashara yake kikamilifu.
Mlozi amesema biashara bila matangazo,ni sawa na mtu asiye na biashara kwa sababu bidhaa zake,hazitajulikana.
Amesema pamoja na kujitangaza huko,kwanza wahakikishe bidhaa zao zina kuwa na ubora unaohitajika na pia wahakikishe wanashiriki maonyesho yanayoandaliwa na SIDO kanda ya kati.
Awali meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende, amesema kuwa SIDO inao mpango wa kuwaelimisha wafugaji na kuhakikisha uzalishaji wa zao la asali unazingatia ubora tangu mahali zao linapoanzia.
Kibende amesema ubora huo unaanzia eneo la ufugaji,uvunaji na ufungashaji,upatikanaji wa masoko ya ndani na ya nje ya nchi.
“SIDO imeona umuhimu wa kutoa mafunzo haya kwa kuzingatia kwamba walengwa tayari wameanza shughuli za ufugaji nyuki,ununuzi na uuzaji wa zao la asali”,alifafanua zaidi meneja Kibende.

Picha na Mo Blog

Matatani kwa kumbaka kikongwe



POLISI mkoani Singida inamshikilia mkazi wa Kijiji cha Wibia, Saidi Hamisi (30) kwa tuhuma za kumbaka bibi kizee mwenye umri wa miaka themanini, mkazi wa Kijiji cha Matongo, Wilaya ya Ikungi, mkoani hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kamanda wa jeshi hilo mkoani Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea juzi usiku na kumtaja aliyembaka bibi kizee huyo kuwa ni Saidi Hamisi.
Aidha, Kamanda Kamwela alifafanua pia kwamba tukio hilo la ubakwaji wa bibi kizee huyo lilitokana na ulevi wa kupindukia kwa mtuhumiwa.
Kamishna msaidizi huyo alisema “mtuhumiwa alifanya kitendo hicho kutokana na kuwa wakiishi nyumba moja na bibi huyo hivyo alipokunywa pombe na kulewa ndipo alipoona aende akamalize matatizo yake kwa jirani yake huyo,” alisema.
Kwa mujibu wa maelezo ya jamaa wa karibu wa mtuhumiwa huyo, inasemekana kwamba baada ya mtuhumiwa kumaliza kitendo hicho aliamua kuendelea kulala na bibi kizee huyo mpaka asubuhi ili aweze kuendelea tena na kitendo hicho asubuhi kabla ya kuondoka kwenda kuendelea na shughuli zake nyingine.
Aidha, Kamanda Kamwela alisisitiza kuwa majira ya saa 7:15 usiku wananchi walitoa taarifa kwenye kituo cha polisi ndipo jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa na kumhoji.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamwela, bibi kizee huyo amepelekwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi ili kujiridhisha iwapo amefanyiwa kitendo hicho cha kinyama na mjukuu wake na kama hajaambukizwa magonjwa ya zinaa.

Chanzo;Tanzania Daima

TRA Singida yazindua rasmi siku ya mlipa kodi.

Afisa elimu na huduma kwa mlipa kodi TRA mkoa wa Singida, Zakaria Gwagilo akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi ambayo yamezinduliwa rasmi juzi. Zakaria alitoa taarifa hiyo kwa niaba ya kaimu meneja TRA mkoa wa Singida Alistides Paulo.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Singida imezindua rasmi maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo ya kutoa misaada kwa makundi yenye mahitaji maalumu.
Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Singida, Alistides Paulo wakati akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa Mkoa wa Singida.
Katika taarifa yake hiyo iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Elimu na huduma kwa mlipa kodi Zakaria Gwagilo alitaja baadhi ya shughuli zitakazofanyika katika maadhimisho hayo kuwa ni pamoja na kutoa misaada kwenye wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ya Manyoni.
Paulo alitaja shughuli zingine kuwa watafanya semina kwa makundi mbalimbali ya walipa kodi na pia kuwatembelea walipa kodi kwenye vituo vya biashara na kuzungumza nao kuweza kufahamu matatizo yao.
“Katika kilele cha siku ya mlipa kodi Novemba nane mwaka huu baadhi ya walipa kodi watazawadiwa vyeti kutokana na kukidhi vigezo vya ubora wa kutunza kumbukumbu sahihi za biashara kulipa kodi sahihi na kwa wakati na ulipaji kodi kwa hiari”,amesema Kaimu Meneja huyo.
Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Paulo mkoa wa Singida unatarajia kuongeza makusanyo kutoka shilingi 4.19 kwa mwaka 2013/2014 zinatajiwa kukusanywa hadi shilingi 8.3 bilioni ifikapo mwaka 2017/2018.

Kwa mwaka huu ujumbe wa siku ya mlipa kodi ni “Tulipe kodi kwa matokeo makubwa sasa”.
Chanzo: mtandao wa Singida 
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa