MO DEWJI FOUNDATION YAKABIDHI MATUNDU NANE YA CHOO BORA KWENYE SHULE YA MSINGI KIBAONI SINGIDA DSC01579

DSC01579
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida, Sundi Samike, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni zilizotolewa na MO Dewji Foundation (shilingi 14 milioni) na Doris Mollel Foundation shilingi 2.3 milioni).
DSC01583
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation mkoani Singida, Duda Mughenyi, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane shule ya msingi Kibaoni mjini Singida, chenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16. Duda amewataka wakazi wa manispaa ya Singida, kujenga utamaduni wa kuchangia kwa hali na mali, uboreshaji wa mazingira ya shule, ili kuvutia wanafunzi kupenda shule.
DSC01592
Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation ya jijini Dar-es-sa-laam, Doris Mollel, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane ya shule ya msingi Kibaoni mjini Singida chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni, kati ya fedha hizo, Mo Dewji Foundation imetoa shilingi 14 milioni na Doris Foundation shilingi 2.3 milioni.
DSC01596
Mwakilishi wa Mo Dewji Foundation mkoani Singida, Duda Mughenyi, (wa tatu kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation, Doris Mollel (wa pili kulia) wakielekea kuzindua choo bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni.
DSC01600
Mwakilishi wa MO Dewji mkoani Singida, Duda Mughenyi, (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundatin, Doris Mollel (wa tatu kushoto) kwa pamoja wakizindua choo bora kipya cha shule ya msingi Kibaoni chenye thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni. MO Dweji Foundation imechangia shilingi 14 milioni na Doris Mollel, shilingi 2.3 milioni.
DSC01603
Jengo la choo bora chenye matundu nane kilichojengwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi 16 milioni kwa ushirikiano wa MO Dewji Foundation na Doris Mollel Foundation kitakachotumiwa na wanafunzi 842 wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida. (Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
WAZAZI/WALEZI wakazi wa halmashauri ya manispaa ya Singida, wamehimizwa kujenga utamaduni wa kuchangia kwa hali na mali uboreshaji wa mazingira ya shule, kama njia moja wapo ya kuwavutia wanafunzi kuhudhuria shule.
Wito huo umetolewa na Mwakilishi wa MO Dewji Foundation mkoa wa Singida, Duda Mughenyi, wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi choo bora chenye matundu nane chenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16 kwa shule ya msingi Kibaoni mjini hapa, yenye jumla ya wanafunzi 842, kati yao wavulana ni 377 na wasichana ni 465.
Alisema uzoefu unaonyesha kwamba mazingira ya shule yakiwa safi, vifaa vya kufundishia na kujifunzia viwepo vya kutosha , maji safi na salama yawepo na vyoo bora vinavyokidhi mahitaji, hatua hiyo huwajengea mazingira mazuri wanafunzi , kujiendeleza kielimu.
Akifafanua, alisema shule ya msingi ya Kibaoni ilikaribia kufungwa kutokana na kukosa vyoo kwa ajili ya wanafunzi na wanafunzi,lakini Dewji Foundation na Doris Mollel Foundation, ilinusuru shule hiyo isifungwe baada ya MO Dewji Foundation kutoa shilingi 14 milioni na Doris Mollel kutoa shilingi 2,300,000.
Duda alitumia nafasi hiyo kuwataka wanafunzi wakitunze na kudumisha usafi wa choo hicho ili kiweze kutumika kwa muda mrefu.
Kwa upande wake Doris Mollel (Miss Singida 2014), alisema Foundation yake itaendelea kufadhili sekta ya elimu mkoani Singida kama njia ya kuwashukuru wakazi mkoani hapa kwa kumsapoti na kufanikisha kushinda nafasi ya Miss Singida mwaka jana.
Awali Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kindai tarafa ya Mungumaji iliyoanzishwa mwaka 1975,Sundi Samike,alishukuru uongozi wa Mo Dweji Foundation na Doris Mollel Foundation, kwa kuifadhili shule hiyo ujenzi wa choo na kuinusuru kufungiwa.
“Nitumie nafasi hii pia kulipongeza shirika la WaterAid Tanzania kwa uamuzi wake wa kufadhili ujenzi wa vyoo bora ambao ujenzi wake tayari umeishaanza.Aidha,nitoe wito kwa wazazi,wasaidie kwa hali na mali kuharakisha ujenzi huu”,alisema.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MAMA SAMIA AHUTUBIA SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

unnamed
Mbunge wa Manyoni Mashariki, John Chiligati, akimuombea kura Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM, John Magufuli, katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Viwanja vya Ofisi ya CCM wilaya ya Manyoni mkoani Singida, leo.(Picha na Bashir Nkoromo).

ABBAS MAZIKU: MFANYABIASHARA ANAYETAMANI KUFUATA NYAYO ZA BILIONEA MO DEWJI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

04.jpgk
Mfanyabiashara wa Kimataifa Abbas Maziku akiwa katika picha ya pamoja na Mfanyabiashara ambaye pia ni Bilionea kijana Barani Afrika, Mtendaji Mkuu wa kampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji, 'MO' amabaye anafuata nyayo zake katika kufikia malengo yake kibiashara.
Na Mwandishi Wetu
BIASHARA ya kusafirisha mazao ni miongoni mwa biashara zenye ushindani mkubwa kutokana na kutawaliwa na matajiri wenye asili ya Kiasia.
Kutokana na sababu hiyo imewafanya waafrika wengi kuwa na uthubutu katika biashara kwa kuhofia huenda wasifanikiwe na kujitanua kibiashara.
Mbali na ugumu huo lakini pia waafrika wengi hasa watanzania wamejikuta wakiishia kuwa wafanyabiashara ya kawaida na kupoteza fursa za kimataifa .
Kupoteza fursa muhimu za kimataifa kumefanya wakose fursa ambazo zingeweza kuwafanya wawe na mawazo mengine ya kuchangamkia fursa za kibiashara na kufikiri nje ya boksi.
Makala haya ndani ya mtandao huu yanaangazia mahojiano na mfanyabiashara wa kwanza wa kitanzania kufanya biashara ya kusafirisha Korosho kwenda nchini Vietnam aitwaye Abbas Maziku ambapo alielezea alipoanzia, vikwazo, mafanikio na matarajio yake kibiashara.

Alipoanzia

Maziku anasema alianza biashara ya kusafirisha mazao mnamo mwaka 2013 baada ya kuvutiwa na mjomba yake ambaye alikuwa na mashamba yaliyokuwa na mazao mbalimbali.
Miongoni mwa mazao ambayo Maziku alianza nayo na anaendelea nayo ni pamoja na Korosho, Ufuta, Mbaazi, Choroko, Mtama, Alizeti, Mashudu yapamba na pamoja na Pilipili Manga.

Anayapata wapi mazao?

Anasema mazao huyakusanya kutoka kwa wafanyabaishara wadogo wadogo ambao hukusanya mazao kwa wakulima pamoja na minada inayofanywa na vyama vya ushirika katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Dodoma, Singida, Shinyanga na Tanga ambayo hufanyika mara moja kwa kila wiki.

Anayasafirisha kwa njia gani?

Akizungumzia jinsi anavyosafirisha mazao hayo, Maziku anasema hutumia usafiri wa barabara kuyatoa mikoani hadi kuyafikisha kwenye maghala ambayo hutumia kuyahifadhi kabla ya kufungasha.
"Wakati wa kuyafungasha unapofika huwa nayafungasha kwa kutumia vibarua na katika vifungashio vyangu huwa na nembo inayoonyesha jina la kampuni yangu na baada ya hapo sampuli hupelekwa katika maabara za kupima kupima ubora wa mazao kimataifa iitwayo SGS na ndipo hufuatiwa na hatua ya mwisho ya usafirishaji ambayo huwa natumia Meli za mashirika mbalimbali ikiwemo IPTL, MAERSK na nyinginezo kwa ajili ya kwenda nchini Vietnam", anasema Maziku.
Anabainisha baada ya hatua zote hizo hufuata taratibu zinazotakiwa ikiwemo watu wa Mamlaka ya mapato T.R.A, wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo na Ufugaji, Wanasheria pamoja na maofisa wa usalama wa Taifa ambao uhakikisha hatua zote halali zimefutwa.
Maziku anaweka bayana kwamba kwa biashara za kimataifa taasisi kama Shirika la viwango TBS na mamlaka ya Chakula na Dawa huwa hawahusiki bali wahusika wakuu ni SGS.

Anajiendeshaje Kibiashara?

Maziku anajinasibu kuwa biashara ya mazao kupeleka nje ya nchi ni biashara yenye ushindani mkubwa hivyo anakumbuka alianza na mtaji wa sh 2,000,000 na sasa anazungumzia mtaji wa sh mil 200.
“Si rahisi kufika nilipofikia kwa sababu biashara hii ina ushindani mkubwa, ninashindana na matajiri wakubwa wenye uwezo wa kujipangia bei za mazao hivyo ingawa nimepiga hatua lakini bado ninahitaji kupanua biashara yangu zaidi na zaidi”, anasisitiza kwa hisia kali.
Anaeleza kuwa mwaka 2013 alipata hasara ya mamilioni ya pesa baada ya ubora wa mazao kupimwa na kuonekana upo kwenye kiwango cha 48 badala ya 51 inayotakiwa hivyo ilimpa wakati mgumu ambao aliyumba kibiashara kutokana na mtaji wake kukata hivyo ili mlazimu kuingia benki na kukopa pesa ambazo hadi sasa bado analipa deni hilo.
“Nilipata hasara kubwa sana ambayo hadi leo hii bado ninalipa hilo deni nililokopa benki ingawa pia fedha kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato ya biashara zingine ninazozifanya zinaendelea kuifanya biashara hii ya mazao kwenda nje ya nchi iendelee kuwepo” anasema Mfanyabiashara huyo wa kimataifa.

Kaimu Msimamizi wa uchaguzi Singida mjini atupilia mbali pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea wa CCM

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

DSC01221
Kaimu msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida mjini, Gerald Muhabuki Zephyrin,akizungumza na Modewjiblog juu ya uchaguzi ubunge jimbo la Singida mjini.(Picha na Gasper Andrew).
Na Nathaniel Limu, Singida
PINGAMIZI lililowekwa na Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA),jimbo la Singida mjini, dhidi ya mgombea wa CCM Mussa Ramadhan Sima kuwa fomu zake haziko sawa kwa mujibu wa kanuni,taratibu na sheria za uchaguzi,limetupiliwa mbali kwa madai kwamba halina mashiko.
Akizungumza na mwakilishi wa Modewjiblog ofisini kwake, kaimu msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida mjini,Gerald Muhabuki Zephyrin, alisema kuwa CHADEMA iliwasilisha pingamizi kwamba barua ya kumthibitisha Sima kugombea ubunge kupitia tiketi ya CCM, imesainiwa na mtu ambaye hakubaliki kisheria.
Akifafanua, alisema mgombea wa jimbo la Singida mjini kupitia CHADEMA, Msindai Mgana Izumbe, amelalamikia barua hiyo kuwa imesainiwa na  Mary Maziku, kwa madai sio katibu halisi wa mkoa wa Singida.
Gerald alisema katika  kujiridhisha kama kweli Maziku sio mtu stahiki wa kumuthibitisha mgombea wa CCM kwenye nafasi ya ubunge jimbo la Singida mjini,aliwasiliana na makao makuu CCM Lumumba jijini Dar-es-salaam,na kujibiwa kwa barua kwamba Maziku ndiye katibu wa CCM mkoa wa Singida.
“Mgombea Msindai ambaye alikuwa mwenyekiti CCM mkoa hadi kumalizika kwa mchakato wa kura za maoni,katibu wake wa mkoa kwa wakati huo, alikuwa Mary Chatanda ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mary Maziku kipindi cha mchakato wa kura za maoni unaendelea.Maziku ndiye aliyesaini barua ya kumthibitisha Sima”,alifafanua zaidi.
Katika hatua nyingine,Gerald ambaye ni mkuu wa idara ya utumishi na utawala manispaa ya Singida,amesema kuwa aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Singida mjini,Victoria John Msusu kupitia UPDP,ameeguliwa kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya kushindwa kutimiza masharti ikiwemo kushindwa kuwasilisha fomu kwa wamadai na kushindwa kulipa ada ya fomu shilingi 50,000.
Msimamizi amewataja wagombea wa ubunge wa jimbo la Singida mjini waliopitishwa na chama kwenye mabano kuwa ni ni pamoja na Sima (CCM),Jeremia Paulo Wandili (ACT Wazalendo),Msindai Mgana Izumbe (CHADEMA) na Mwanamvua John Haji (CUF).
Alisema kampeni zimeishaanza vizuri kwa amani na utulivu mkubwa na amewaoomba wagombea kufanya kampeni kwa ustarabu na kuzingatia kanuni,taratibu na sheria za uchaguzi.
“Matarajio ya wananchi wa jimbo la Singida mjini,ni kwamba oktoba 25 mwaka huu,wapige kura kuwachagua viongozi wanaoamini watawaletea maendeleo ya kweli na si vinginevyo”, alisema Gerald.

Mgana Msindai achukua fomu ya kugombea ubunge jimbo ya Singida mjini kwa tiketi ya CHADEMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
IMG-20150821-WA0001
Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa wenyeviti CCM mikoa ya Tanzania, Mgana Izumbe Msindai, akikabidhiwa fomu na msimamizi wa uchaguzi halmashauri ya manispaa ya Singida, Joseph Mchina ya kugombea ubunge jimbo la Singida mjini kupitia tiketi ya CHADEMA.
(Picha na Nathaniel Limu).
 

Nyalandu achukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Singida Kaskazini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

FOMU
Mgombea Ubunge Jimbo la Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu akichukua fomu ya kugombea Ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM kwa  MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA SINGIDA KASKAZINI, Mkurugenzi Mtendaji HAJJAT MWASUMILWE.
hotubA
Nyalandu akihutubia wananchi Kinyagigi.
kinyagigi
Lazaro Nyalandu akiwa Kinyagigi.
MAPOKEZI
Wananchi wa kijiji cha Kinyagigi wakimpokea Nyalandu.
 
 

Kijana tajiri Afrika ni Mtanzania

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mfanyabiashara tajiri kijana Mohamed Dewji
Mfanyabiashara maarufu nchini na Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohammed Dewji (pichani) kwa mara ya kwanza ameingia kwenye orodha ya mabilionea 29, akiwa tajiri kijana kuliko wote barani Afrika.
Jarida la Forbes la Marekani limemtaja Dewji (39), katika nafasi ya 24 ya matajiri wa Afrika akiwa na utajiri wa Dola 1.3 bilioni za Marekani (Sh2.34 trilioni) unaotokana na biashara mbalimbali anazozifanya kupitia kampuni yake ya Mohammed Enterprises (Metl Group).“Dewji alibadilisha biashara aliyoanzisha baba yake kutoka uuzaji bidhaa na kuwa na viwanda vya Metl,” inasema sehemu ya habari inayomuhusu bilionea huyo Mtanzania .
“Alinunua viwanda vya nguo na mafuta vilivyokuwa vinamilikiwa na Serikali kwa bei ndogo na kuvifanya viwe na faida zaidi kwa kutumia mtindo wa kisasa wa menejimenti,” inaongeza ripoti hiyo.
Metl ina viwanda vya kutengeneza nguo na bidhaa nyingine za matumizi ya binadamu vikiwamo vyakula, sabuni na vinywaji. Pia ina mapato yanayozidi Dola 1.4 milioni za Marekani (Sh2.5 trilioni) kwa mwaka.
Katika kampuni hiyo, ambayo imekuwa na ushindani dhidi ya kampuni kubwa nyingine kama Said Salim Bakhresa, Dewji anamiliki asilimia 75 ya hisa zote.
Kwa mujibu wa tovuti yake, Metl inaendesha shughuli za uagizaji na usafirishaji bidhaa kutoka na kwenda nje, uzalishaji unaohusisha nguo, vinywaji na vyakula, usagaji nafaka, nishati na petroli na utengenezaji baiskeli.
Pia inahusika na huduma za simu, fedha, kilimo na pia ina kitengo cha kontena kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Dewji anashika nafasi mbili juu zaidi ya kada maarufu wa CCM na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Igunga, Aziz Rostam (50) aliyewekwa nafasi ya mwisho.
Rostam amefungana nafasi ya 26 na mabilionea wa Nigeria, Abdulsamad Rabiu na Femi Otedola wenye utajiri wa Sh1.8 trilioni kila mmoja.
Orodha hiyo ya 29 bora inaoongozwa na bilionea wa Nigeria, Aliko Dangote akiwa na utajiri wa Dola 15.7 bilioni za Marekani (Sh28.2 trilioni), kiwango ambacho ni mara moja na nusu ya bajeti ya Serikali ya Tanzania ya mwaka 2014/15.
Forbes linamtaja Rostam kuwa na utajiri wenye thamani ya Dola 1 bilioni za Marekani (Sh1.8 trilioni), kiwango ambacho kimebaki pasi na mabadiliko kutoka orodha ya mwaka jana. Rostam anamiliki asilimia 35 ya hisa katika kampuni ya huduma za simu za mkononi ya Vodacom.
BBC

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa