SINGIDA WAASWA KUTEKELEZA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI KWA WELEDI

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Dkt Zakia Mohamed Abubakar leo ametembelea mafunzo ya Waandishi Wasaidizi na Waendesha Vifaa vya Bayometriki watakao husika na zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Halmashauri ya Singida Vijijini mkoani Singida na kuzungumza nao wakati wa mafunzo yao ya siku mbili yaliyoanza leo Septemba 22 na kumalizika kesho Septemba 23, 2022.Akizungumza na Waandishi hao Wasaidizi na Waendesha Vifaa vya Bayometriki Dkt Zakia aliwataka kuzingatia mafunzo wanayopewa, dhamana waliyopewa ya kuendesha zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa weledi. Mafunzo hayo ni maandalizi...

"FANYENI KAZI KWA BIDII KWA MAENDELEO YA TAIFA" DAS PETER MASINDI

Katibu Tawala wilaya ya Mkalama Ndugu Peter Masindi amewataka watumishi wilayani Mkalama kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa bidi katika kuwaenzi mashujaa wa nchi waliopigana kwa ajili ya taifa la Tanzania.Kauli hiyo ametoa Julai 25, 2024 kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Mkalama wakati wa zoezi la usafi liliofanyika katika hosipitali ya wilaya ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Mashujaa nchini.Serikali inaleta fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi, tuwajibike pamoja katika kuhakikisha fedha hizi zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Kila mmoja katika nafasi yake atimize wajibu wake, huwezi kuwa shujaa kama ukishindwa kutimiza wajibu wako,...

“WAZAZI TUNA WAJIBU WA KUMLINDA MTOTO WAKIKE” DC MACHALI

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amefanya ziara ya kikazi kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Kijiji cha Nkinto kilichopo kata ya Nkito wilayani Mkalama.Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara, Leo Julai 29,2024 Mhe. Machali amewataka wazazi wa Kijiji cha Nkinto na wilayani Mkalama kwa ujumla kuwa mstari wa mbele kupinga mimba za utotoni hasa kwa wanafunzi. “Tunawajibu mkubwa wa kumlinda mtoto wakike, wananchi wenzangu tushirikiane pamoja kupambana dhidi ya tatizo la mimba mashuleni. Nawaomba sana mtoe ushirikiano pindi kesi za mimba zinapofika Mahakamani, wanaume achaneni na wanafunzi” Mhe....

MHE. JAMES MKWEGA AZINDUA ZAHANATI YA IGENGU

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhe. James Mkwega amezindua zahanati ya Igengu ikiwa ni mpango wa serikali wa kuhakikisha kila Kijiji nchini kinakuwa na zahanati.Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zahanati hiyo Julai 20,2024 katika Kijiji cha Igengu, Mhe. James Mkwega ameishukuru serikali pamoja na kwataka wananchi wa Kijiji hicho kulinda afya zao. “Serikali imefanya kazi kubwa, Rais Dkt. Samia kaleta Zahanati na kaleta Umeme. Nampongeza pia Mganga Mkuu wetu Dkt. Solomon Michael kwa kazi kubwa anayofanya lakini pia niwapongeze wananchi kwa kazi kubwa mliofanya. Niwasihi tulinde afya zetu, tuzingatie ushauri wa wataalamu...

BITEKO ATANGAZA KIAMA KWA WALIOHUJUMU RUZUKU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.  Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini, Hamis Kigwangala (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye Chuo cha Madini Dodoma, Kampasi ya Nzega ili kujionea hali ya eneo hilo.  Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia) akikagua mazingira ya Chuo cha Madini Dodoma, Kampasi ya Nzega ili kujionea hali ya Kampasi hiyo.  Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Isanga, Kata ya Lusu Wilaya ya Nzega (hawapo...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa