WAZEE WA KIMILA WAHUSISHWE VITA DHIDI YA UKEKETAJI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

ZAIDI ya wanawake 9,000 mkoani Singida wamegundulika kuwa wamekeketwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Daktari Bingwa wa Ushauri wa magonjwa ya Wanawake na Uzazi mkoani hapa, Suleiman Mutani aliyasema hayo kwenye Jukwaa la Kitaifa la kuadhimisha Siku ya kupinga ukeketaji lililofanyika mjini hapa.

Dk Mutani alisema, idadi hiyo ya waliokeketwa ni sawa na asilimia 20.8 ya wanawake wote waliokwenda kujifungua kwenye vituo mbalimbali vya kutolea tiba mkoani humu, kati ya Januari 2013 na Desemba mwaka jana.
“Wanawake 9,386 walibainika kufanyiwa ukeketaji, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na ni ukiukwaji wa misingi ya haki za binadamu, licha ya kuwa na madhara makubwa ya kiafya” alisema Dk Mutani.

Alitaja madhara yatokanayo na ukeketaji kuwa ni pamoja na kuwa na uzazi pingamizi wakati wa kujifungua, wanawake kupata shida wakati wa hedhi, uwezekano wa kupata fistula, kuugua maradhi ya kujamiiana na kuhisi maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.

Dk Mutani alisema pia kuwa madhara hayo ni matokeo hasi yasababishwayo na jamii husika kuendelea kukumbatia mila hiyo potofu .
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa), Edda Sanga alisema, madhumuni ya jukwaa hilo ni kutoa fursa kwa wadau kujadili kwa kina utekelezaji wa maazimio ya miaka iliyopita na kupanga mikakati na njia bora zaidi za kukabiliana na mbinu mpya za ukeketaji.

Alitaja mikoa ambayo ni vinara wa ukeketaji na asilimia kwenye mabano kuwa ni Manyara (71), Dodoma (64), Arusha (59), Singida (51) na Mara (40).
Mikoa mingine ambayo pia inahusishwa na ukeketaji kutokana na watu wa makabila yanayoendesha vitendo hivyo kuhamia, ni Dar es Salaam, Pwani na Morogoro.

Hata hivyo, wadau waliohudhuria kikao hicho walisema kuwa, pamoja na mikakati mbalimbali, mbinu bora zaidi ni kuwawezesha ngariba kuwa na miradi ya kipato mbadala ili waache biashara ya kukeketa.

Aidha, walishauri wazee wa kimila katika maeneo husika wahusishwe kikamilifu katika vita dhidi ya ukeketaji kwa sababu wanaheshimika zaidi na wana ushawishi mkubwa kwa jamii.

Jukwaa hilo la siku mbili lililoandaliwa na Tamwa, limefadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA). Lilihudhuriwa na wadau kutoka mikoa minane ambayo baadhi ya makabila yake yanaendesha ukeketaji.
CHANZO: HABARI LEO.

BURUNDI YAWATAKA WATANZANIA KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFURI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Pombe Magufuri.

SERIKALI ya Burundi na chama tawala cha nchi hiyo CNDD-FDD imewataka Watanzania kumuunga mkono Rais John Magufuli katika azma yake ya kusimamia nidhamu ya viongozi na kuleta maendeleo kwa taifa.

Mkuu wa Wilaya ya Kibago mkoani Makamba nchini Burundi, Juma Albert alitoa kauli hiyo akiongoza ujumbe wa watu watano wa kiserikali na chama tawala cha nchini humo, waliohudhuria maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yaliyofanyika kimkoa kwenye kijiji cha Munzenze, wilayani Buhigwe mkoani hapa.

Albert alisema, Serikali ya Burundi na chama tawala cha CNDD- FDD imekuwa ikifuatilia mambo yanayofanywa na Rais Magufuli na kwamba, wanamuunga mkono kwa yale anayofanya ambayo yamekuwa na tija kwa uchumi wa Tanzania.

Alisema, Magufuli pia amekuwa akilenga kuimarisha uchumi wa nchi yake sambamba na ustawi wa jirani zake ikiwemo Burundi. Pamoja na hayo viongozi hao walitoa shukrani zao kwa wananchi wa Kigoma kuendelea kuwahifadhi ndugu zao katika kambi mbalimbali za wakimbizi, kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini mwao.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma, Dk Walid Kabouorou aliwataka viongozi wa upinzani kukubali kwamba uchaguzi umekwisha na CCM ndio mshindi.

Alisema, kutokana na hilo, hawana budi kuungana na kutekeleza Ilani ya CCM kwa kuhakikisha miradi ya maendeleo iliyopangwa kutekelezwa inafanikiwa. Awali, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya aliwataka wananchi kupeleka watoto wao shule ili kuunga mkono mpango wa Serikali wa kuondoa ujinga kwa Watanzania kutojua kusoma na kuandika.

Alisema, kumekuwa na tabia ya kuwaficha watoto walemavu na kuwanyima haki yao ya kupata elimu, hivyo aliitaka jamii kuwafichua wote wenye kuendekeza ukatili huo dhidi ya wenye ulemavu.
 CHANZO: HABARI LEO

RAIS MAGUFULI AHUTUBIA KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 39 YA CCM SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

RAIS MAGUFULI AOMBOLEZA POLISI WALIOKUFA AJALINI SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Rais John Magufuli.
Rais John Magufuli, amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jererali, Ernest Mangu, kufuatia vifo vya askari watatu waliopoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea juzi katika kijiji cha Isuna, wilayani Ikungi mkoani Singida.
 
Askari waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Inspekta Miraji Mwegelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerald Mtondo.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, Rais amesikitishwa na vifo vya askari hao, ambao wamekutwa na mauti wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
 
“Kupitia kwako Mkuu wa Jeshi la Polisi, natoa pole nyingi kwa familia za askari waliopoteza maisha, ndugu, jamaa na marafiki pamoja na askari wote wa jeshi hilo ambao wameguswa kwa namna ya pekee na msiba huu,” ilieleza taarifa hiyo.
 
Rais Magufuli pia amewatumia salamu za pole askari walioumia katika ajali hiyo, akiwamo Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarabi Mkoa wa Singida, Mratibu wa Polisi, Peter Magira na kuwaombea wapone haraka ili waendelee na majukumu yao ya kila siku.
CHANZO: GAZETI LA NIPASHE

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWATEMBELEA WAHADZABE NA KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO KWA JAMII HIYO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipozi kwa picha na Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba kushoto na Mama Sara Philipo mwenye nyumba hiyo wakati alipozungumza na chifu huyo leo, Katika ziara hiyo Kinana katika kijiji cha Kibampa na kukagua miradi mbalimbali ya jamii hiyo ya Kihadzabe ikiwemo maji, mabweni ya watoto wa jamii hiyo pamoja na zahanati iliyopo katika kijiji cha Munguli kata ya Mwangeza wilaya ya Mkalama mkoani Singida.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone amewajengea mabweni na kuwawekea mradi wa maji, Umeme na kuwafundisha kilimo cha mihogo na mazao mengine ili kuweza kujikimu kwa chakula kwani jamii ya kabila hilo inakula nyama, mizizi ya miti na asali.
Lakini pia vijana hamsini wa Kabila hilo wamejiunga na jeshi la wananchi kwa mpango mkuu wa mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone na serikali kwa kuwaendeleza kielimu na kimaendeleo, kuna vijana wengine sitini wataingizwa jeshini ikiwa ni mkakati wa kuielimisha jamii hiyo ili kubadili maisha bila kuharibu mila yao.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MKALAMA -SINGIDA)
2
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba wakati alipotembelea na kujadiliana naye mawili matatu.
3
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mama Sara Philipo mwenye nyumba hiyo wakitoka nje mara baada ya Kinana kuzungumza na Chifu Edward Mashimba.
4
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba
5
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi hao wa jamii ya Wahadzabe huku Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba akitafsiri katika kijiji cha Kibampa kata ya Mwangeza.
6
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo wakimsikiliza Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akiwahutubia.
7
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika kazi ya kupanda mbegu ya muhogo na vijana wa Kihadzabe katika shamba darasa ililopo kijiji cha Kibampa kata ya Mwangezi ikiwa ni mafunzo ya kilimo kwa jamii hiyo.
9 10
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia ngoma ya jamii hiyo wakati alipokuwa akiwasili kijiji cha Kibampa.
11
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kucheza ngoma ya asili ya jamii ya Kihadzabe.
13
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukikatisha misitu na mabonde wakati ukielekea kata ya Mwangeza kijiji cha Kibampa ambako jamii hiyo inaishi.
15
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaklimiana na vijana wa kisukuma aliowakuta wakipalilia shamba, vijana hao walimweleza Kinana kuwa wanahitaji serikali iwatengenezee barabara yao jambo ambalo litarahisha hata uuzaji wa mazao yao.
16
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa maji katika kijiji cha Munguli ambao umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo anayetoa maelekezo ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher Ngubiagai.
17
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mabweni ya watoto wa jamii ya Kihadzabe yaliyojengwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone katika kijiji cha Munguli mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 60 wa kiume 30 na wakiume 30 yamejengwa maalum kwa ajili ya jamii kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher Ngubiagai.
18
Baadhi ya wananfunzi wa shule hiyo
19
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya Munguli Athman Kinyere akisoma taarifa ya shule hiyo kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
20
Hii ni moja ya nyumba zinazotumiwa na jamii hiyo ya Kihadzabe.
21
Baadhi ya wananchi wa jamii hiyo wakiwa katika mkutano
23
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mtambo wa Sola unaoendesha maji katika mradi wa maji wa kijiji cha Munguli ambao umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo anayetoa

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA ALIPO WASILI MKOANI SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone wakati alipowasili mjini Singida tayari kwa maandalizi ya Maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM yanayotarajiwa kufanyika mjini Singida Jumamosi  Februari 6 mwaka huu kwenye uwanja wa michezo wa Namfua mkoani humo, wa pili kutoka kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na mkuu wa wilaya ya Singida mjini Mh. Said Amanzi. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kufanya Kazi”
(PICHA NA JOHN BUKUKU – FULLSHANGWE-SINGIDA)
2
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia jambo na Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone wakati alipowasili mjini Singida tayari kwa maandalizi ya Maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM yanayotarajiwa kufanyika mjini Singida Jumamosi  Februari 6 mwaka huu mkoani humo, kushoto ni Mh. Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
4
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akilakiwa na akina mama mbalimbali waliojitokeza kumpokea wakati alipowasili mjini Singida jana.
5
Akina mama na wana CCM mbalimbali wakiimba nyimbo za kumlaki Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili mkoani Singida jana. (P.T)

SERIKALI YARIDHISHWA WAHADZABE KUACHANA NA UJIMA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI wilayani Mkalama mkoani Singida imeridhishwa na kasi inayofanyika kuibadili jamii ya Wahadzabe kutoka kutegemea maisha ya ujima na kuanza kuishi maisha ya kawaida yanayoambatana na mabadiliko ya mazingira yaliyopo sasa.
Akizungumza na gazeti hili, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Christopher Ngubiagai kuhusu jamii hiyo ambayo chakula chao kikuu ni nyama, mizizi, matunda na asali ikiendelea kuishi kwenye viota katikati ya pori, alisema Halmashauri ya wilaya hiyo inafanya mapinduzi makubwa hasa kwa kufikisha elimu kwa watoto wao.
Wahadzabe ni miongoni mwa makabila madogo zaidi nchini linalopatikana kaskazini mwa Tanzania kando ya Ziwa Eyasi kwenye Bonde la Ufa na kupakana na uwanda wa Serengeti pia wapo katika wilaya ya Mkalama.
Jamii hiyo inayoaminika kuwa ni ya mwisho kabisa barani Afrika inayotegemea uwindaji kwa ajili ya kuishi, inatakiwa kubadilika taratibu kutokana na muingiliano wa kasi unaojitokeza na jamii ya wakulima na wafugaji wanaowazunguka.
Katika kuwezesha elimu kwa vijana, Halmashauri ya wilaya ya Mkalama inatoa chakula, nguo na kuendesha programu maalumu kwa ajili ya kuhudumia wanafunzi wa jamii hiyo waliopo katika shule ya msingi Munguli, kata ya Mwangeza iliyotengenezwa mahsusi kwa ajili ya watu wa jamii hiyo.
Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya alisema pamoja na kuwapo kwa wanafunzi wa jamii hiyo, shule hiyo pia hutumiwa na watu wengine ambao wapo hapo wa jamii ya Kisukuma, Wamang’ati na Wabarbaig.
Pamoja na halmashauri hiyo kutoa mambo hayo muhimu, taasisi za kijamii ikiwamo Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (Haydom - Mbulu) na asasi ya kiraia ya FFCC hutoa mchango wa chakula kuongeza nguvu kwa jamii hiyo kushiriki kikamilifu katika kupata elimu ya kawaida.
Ngubiagai alisema watoto wa jamii hiyo wana akili sana kutokana na jinsi wanavyoweza kushika kwa haraka kusoma, kuandika na kuhesabu na kwamba katika mtihani wa darasa la tatu, watoto wa jamii hiyo walishika namba moja hadi 10 huku Wahadzabe wengine wakifanya vyema katika stadi mbalimbali.
CHANZO ; HABARI LEO.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa