Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipozi kwa picha na Mwenyekiti wa
 Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba kushoto na Mama Sara Philipo 
mwenye nyumba hiyo wakati alipozungumza na chifu huyo leo, Katika ziara 
hiyo Kinana katika kijiji cha Kibampa na  kukagua miradi mbalimbali ya 
jamii hiyo ya Kihadzabe ikiwemo maji, mabweni ya watoto wa jamii hiyo 
pamoja na zahanati iliyopo katika kijiji cha Munguli kata ya Mwangeza 
wilaya ya Mkalama mkoani Singida.
 Mkuu wa Mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone amewajengea mabweni na 
kuwawekea mradi wa maji, Umeme na kuwafundisha kilimo cha mihogo na 
mazao mengine ili kuweza kujikimu kwa chakula kwani jamii ya kabila hilo
 inakula nyama, mizizi ya miti na asali.
Lakini
 pia vijana hamsini wa Kabila hilo wamejiunga na jeshi la wananchi kwa 
mpango mkuu wa mkoa wa Singida Ndugu Parseko Kone na  serikali kwa 
kuwaendeleza kielimu na kimaendeleo, kuna vijana wengine sitini 
wataingizwa jeshini ikiwa ni mkakati wa kuielimisha jamii hiyo ili 
kubadili maisha bila kuharibu mila yao.(PICHA NA JOHN 
BUKUKU-FULLSHANGWE-MKALAMA -SINGIDA)
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa 
Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba wakati alipotembelea na 
kujadiliana naye mawili matatu.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mama Sara Philipo mwenye nyumba
 hiyo wakitoka nje mara baada ya Kinana kuzungumza na Chifu Edward 
Mashimba.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward Mashimba
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi hao wa jamii
 ya Wahadzabe huku  Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Chifu Edward 
Mashimba akitafsiri  katika kijiji cha Kibampa kata ya Mwangeza. 
Baadhi
 ya wananchi wakiwa katika mkutano huo wakimsikiliza Ndugu Abdulrahman 
Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akiwahutubia.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika kazi ya kupanda 
mbegu ya muhogo na vijana wa Kihadzabe katika shamba darasa ililopo 
kijiji cha Kibampa kata ya Mwangezi ikiwa ni mafunzo ya kilimo kwa jamii
 hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia ngoma ya jamii hiyo wakati alipokuwa akiwasili kijiji cha Kibampa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kucheza ngoma ya asili ya jamii ya Kihadzabe.
Msafara
 wa  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukikatisha misitu na 
mabonde wakati ukielekea kata ya Mwangeza kijiji cha Kibampa ambako 
jamii hiyo inaishi.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaklimiana na vijana wa 
kisukuma aliowakuta wakipalilia shamba, vijana hao walimweleza Kinana 
kuwa wanahitaji serikali iwatengenezee barabara yao jambo ambalo 
litarahisha hata uuzaji wa mazao yao.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa maji katika 
kijiji cha Munguli ambao umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo 
anayetoa maelekezo ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher 
Ngubiagai.
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mabweni ya watoto wa 
jamii ya Kihadzabe yaliyojengwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko 
Kone  katika kijiji cha Munguli  mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua 
wanafunzi 60 wa kiume 30 na wakiume 30 yamejengwa maalum kwa ajili ya 
jamii kulia  ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Ndugu Christopher Ngubiagai.
Baadhi ya wananfunzi wa shule hiyo
Mwalimu
 Mkuu wa shule hiyo ya Munguli Athman Kinyere akisoma taarifa ya shule 
hiyo  kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
Hii ni moja ya nyumba zinazotumiwa na jamii hiyo ya Kihadzabe.
Baadhi ya wananchi wa jamii hiyo wakiwa katika mkutano 
Katibu
 Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mtambo wa Sola 
unaoendesha maji katika  mradi wa maji wa kijiji cha Munguli ambao 
umejengwa maalum kwa ajili ya jamii hiyo anayetoa 
0 comments:
Post a Comment