Home » » WATANO WAFA MAJI NA WENGINE 11 WANUSURIKA

WATANO WAFA MAJI NA WENGINE 11 WANUSURIKA

WATU watano wanahofiwa kufa maji na wengine 11 wamenusurika, baada ya gari waliyokuwa wakisafiria kusombwa na maji ya mto kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani mkoani Singida.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida Kamishina msaidizi mwandamizi Geofrey Kamwela, tukio hilo limetokea jana majira ya saa 3: 30 asubuhi katika Kijiji cha Kisimba Wilayani Iramba.
Amesema watu hao waliokuwa wakisafiri kwa gari yenye namba za usajili T.499 ATR aina ya Land rover 110 TDI, walikuwa wakijaribu kuvuka mto Nzalala kutoka eneo Doromoni kwenda Kiomboi Mjini.
Kamanda Kamwela amesema wakati dereva ambaye hajatambuliwa jina wala makazi akijaribu kuvusha, gari hiyo ilizimika katikati ya mto kabla ya kosombwa na maji ikiwa na abiria 16 ndani.
Amesema abiria 11 kati yao wameokolewa na kupelekwa hospitali ya Wilaya ya Iramba kwa matibabu, wakati juhudi za kufukua gari hiyo iliyofukiwa kwa mchanga mita chache kutoka eneo la tukio na kutafuta watu wengine watano ambao hawajulikani walipo zinaendelea kufanywa.
Dereva wa gari hiyo na kondakta wake wanasadikiwa kutoweka baada ya tukio hilo na polisi wanaendelea kuwasaka.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa