WATU
 watano wanahofiwa kufa maji na wengine 11 wamenusurika, baada  ya  gari
 waliyokuwa wakisafiria  kusombwa na maji  ya mto  kufuatia mvua kubwa 
zinazoendelea kunyesha mkoani mkoani Singida.
Kwa
  mujibu wa Kamanda wa Polisi  mkoa wa Singida Kamishina msaidizi 
mwandamizi  Geofrey Kamwela,  tukio hilo limetokea jana  majira ya  saa 
3: 30 asubuhi katika Kijiji cha Kisimba Wilayani Iramba.
 Amesema  watu hao waliokuwa wakisafiri kwa gari yenye namba za usajili 
T.499 ATR aina ya Land rover 110 TDI,  walikuwa wakijaribu kuvuka  mto  
Nzalala kutoka   eneo Doromoni kwenda Kiomboi Mjini.
Kamanda
 Kamwela amesema wakati dereva  ambaye hajatambuliwa jina wala makazi 
akijaribu kuvusha, gari hiyo ilizimika  katikati ya mto kabla ya 
kosombwa na  maji ikiwa na abiria 16 ndani.
Amesema
 abiria 11 kati yao wameokolewa na kupelekwa hospitali  ya Wilaya ya  
Iramba kwa matibabu, wakati juhudi za  kufukua gari hiyo iliyofukiwa kwa
 mchanga  mita chache kutoka eneo la  tukio na kutafuta watu wengine 
watano ambao hawajulikani walipo zinaendelea kufanywa.
Dereva   wa gari hiyo na   kondakta wake wanasadikiwa kutoweka baada  ya  tukio hilo na polisi wanaendelea kuwasaka.
0 comments:
Post a Comment