Kwa mujibu wa mkuu huyo, dhima ya kupata rasilimali na kuzitumia 
kikamilifu kwenye miradi yenye tija, husababisha ukuaji wa uchumi na 
kuongeza utajiri.
Dk. Kone amebainisha hayo juzi mjini Singida wakati akifungua semina 
ya siku mbili kwa wafanyabiashara na wajasiriamali juu ya soko la kukuza
 ujasiriamali (EGM) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Aque Vitae.
Alisema ni muhimu ieleweke wazi kwamba kuna uhusiano wa moja kwa moja
 baina ya mafanikio ya masoko ya mitaji na uchumi wa nchi na kusisitiza 
kwamba moja ya sababu ni serikali kuanzisha na kusaidia maendeleo ya 
Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Aidha, alibanisha kwamba kampeni hiyo imekuja wakati muafaka ambao 
serikali imepania kujenga sekta binafsi imara itakayokuwa injini ya 
uchumi wa taifa.
“Napenda kuchukua fursa hii kuwahakikishia kwamba serikali inatambua 
mchango wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya masoko ya hisa hapa 
nchini, mwamko kama huu unalenga kujenga uelewa kwa sekta binafsi na 
umma juu ya fursa zipatikanazo na soko la hisa zinaungwa mkono na 
serikali.
“Pia nitumie fursa hii kuwataka wadau na wahusika wote kwa ukamilifu 
wenu kutumia tukio hili ili kutumia fursa zipatikanazo kwenye soko la 
hisa,” alisema Dk. Kone.
Hata hivyo Dk. Kone alisema tafiti nyingi zimeonyesha kwamba 
upatikanaji wa mitaji ya wajasiriamali wadogo na wa kati ni changamoto 
kwa maendeleo ya kukua kwa shughuli za ujasiriamali na sekta hiyo kwa 
ujumla.
Awali Meneja Uhusiano wa kitaasisi kutoka DSE, Mary Mniwasa, 
alimweleza mkuu wa mkoa kuwa lengo la semina hiyo ni kampeni ya umma ya 
kupunguza umaskini hapa nchini.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Singida, Francis 
Mashuda, alisema wafanyabiashara wanakumbana na changamoto kubwa ya 
ukosefu wa mitaji.
Semina hiyo ilitarajiwa kuhudhuriwa na wafanyabiashara wa kada 
mbalimbali na wajasiriamali wasiopungua 65, imefadhiliwa na DSE chini ya
 uratibu wa TCCIA Mkoa wa Singida.
Chanzo;Tanzania Daimma 
0 comments:
Post a Comment