Home »
 » Mfanyabiashara ajiua kwa risasi, mwingine achinjwa 
 
Mfanyabiashara ajiua kwa risasi, mwingine achinjwa 
            
				            
        
        
             
       
 
       
        
        
        
        
            
Watu
 wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti yaliyotokea 
mkoani Singida mwishoni mwa wiki likiwemo la mfanyabiashara kujipiga 
risasi kichwani na mwingine huchinjwa shingo, kutolewa koromeo na ulimi.
 
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, 
Geofrey Kamwela alisema katika tukio la kwanza, mfanyabiashara Mashaka 
Omari (30) alikutwa chumbani kwake Mtaa wa Ipembe akiwa amekufa baada ya
 kujipiga risasi kichwani. 
Alisema mfanyabiashara huyo alijiua kwa 
kutumia bastola yake yenye namba TZ CA 895101 ambapo polisi walikuta 
ganda moja la risasi iliyotumika lakini magazini ilikuwa na risasi 11," 
alisema Kamanda Kamwela. 
Uchunguzi wa awali unaonesha marehemu 
alikuwa na mgogoro kati yake na mtu mwingine ambaye hakutajwa kwa ajili 
ya masuala ya kiusalama hivyo kusababisha ajiue. 
"Marehemu aliacha 
ujumbe huo wa maandishi kwenye gari lake namba T664 EES aina ya Toyota 
RAV 4 ambalo alikuwa ameliegesha nje ya ofisi yake," alisema na kuongeza
 kuwa, uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea. 
Katika tukio 
lingine, mkazi wa Kijiji cha Sambaru, Wilaya ya Ikungi, Tatu Selemani 
(42), alichinjwa shingo na kitu chenye ncha kali na watu wasiofahamika 
saa 1:30 asubuhi. 
Kamanda Kamwela alieleza licha ya kuchinjwa shingo
 pia marehemu alitolewa koromeo, ulimi, kuchunwa ngozi usoni na kutolewa
 sikio la kushoto ambapo mwili wake ulikutwa umbali wa mita 80 kutoka 
nyumbani kwake. 
Alisema katika tukio hilo, mtu mmoja Amosi Shenan 
maarufu kwa jina la 'Babu', mkazi wa kijiji hicho ambaye ni mume wa 
marehemu, amekamatwa kwa mahojiano zaidi na uchunguzi bado unaendelea
Chanzo;Majira 
 
 
0 comments:
Post a Comment