Home » » Mfanyabiashara ajiua kwa risasi, mwingine achinjwa

Mfanyabiashara ajiua kwa risasi, mwingine achinjwa

Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti yaliyotokea mkoani Singida mwishoni mwa wiki likiwemo la mfanyabiashara kujipiga risasi kichwani na mwingine huchinjwa shingo, kutolewa koromeo na ulimi.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Geofrey Kamwela alisema katika tukio la kwanza, mfanyabiashara Mashaka Omari (30) alikutwa chumbani kwake Mtaa wa Ipembe akiwa amekufa baada ya kujipiga risasi kichwani.
Alisema mfanyabiashara huyo alijiua kwa kutumia bastola yake yenye namba TZ CA 895101 ambapo polisi walikuta ganda moja la risasi iliyotumika lakini magazini ilikuwa na risasi 11," alisema Kamanda Kamwela.
Uchunguzi wa awali unaonesha marehemu alikuwa na mgogoro kati yake na mtu mwingine ambaye hakutajwa kwa ajili ya masuala ya kiusalama hivyo kusababisha ajiue.
"Marehemu aliacha ujumbe huo wa maandishi kwenye gari lake namba T664 EES aina ya Toyota RAV 4 ambalo alikuwa ameliegesha nje ya ofisi yake," alisema na kuongeza kuwa, uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.
Katika tukio lingine, mkazi wa Kijiji cha Sambaru, Wilaya ya Ikungi, Tatu Selemani (42), alichinjwa shingo na kitu chenye ncha kali na watu wasiofahamika saa 1:30 asubuhi.
Kamanda Kamwela alieleza licha ya kuchinjwa shingo pia marehemu alitolewa koromeo, ulimi, kuchunwa ngozi usoni na kutolewa sikio la kushoto ambapo mwili wake ulikutwa umbali wa mita 80 kutoka nyumbani kwake.
Alisema katika tukio hilo, mtu mmoja Amosi Shenan maarufu kwa jina la 'Babu', mkazi wa kijiji hicho ambaye ni mume wa marehemu, amekamatwa kwa mahojiano zaidi na uchunguzi bado unaendelea

Chanzo;Majira

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa