HATIMAYE WANANCHI WANAOTAKIWA KUPISHA MRADI WA SHANTA GOLD MINE WILAYANI IKUNGI WATEKELEZEWA MALIPO YAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +25576505639

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu akielezea utaratibu wa ulipaji fidia kwa wanufaika.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na wananchi mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd. 



Na Mathias Canal, Singida


Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida huenda ikaanza uchimbaji wa madini ya dhahabu hivi karibuni baada ya kuanza kulipa fidia ya zaidi ya Bilioni 1.6 wanufaika wa awamu ya pili inayohusisha wananchi kutoka Vijiji vitatu vya Mang'onyi, Sambaru na Mulumbi.


Kampuni hiyo tayari imekamilisha ulipaji wa awamu ya kwanza kwa kulipa zaidi ya Milioni 900.2 Wanufaika waliolipwa fedha hizo wanaotokana na mazoezi mawili ya uthamini yaliyofanywa kwenye eneo la mradi kwa ajili ya upanuzi wa kambi.


Malipo hayo yatakamilisha umiliki wa maeneo hayo kwa Kampuni ya Shanta Gold mining kwa ajili ya uchimbaji na kuwafanya wananchi hao kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu pasina kinyongo chochote.


Malipo hayo ya awamu ya pili na ile ya kwanza yamelipwa kwa wanufaika wote wa fidia katika Vijiji vyote vilivyopo Katika Kata ya Mang'onyi yanaondoa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa maeneo mbalimbali waliopo kwenye eneo la mradi huo waliotaka kufahamu hatima ya malipo yao.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi na wawakilishi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa kampuni hiyo inapaswa kutumia muda mfupi katika ulipaji wa fidia kama ilivyofanya katika awamu ya kwanza.


Alisema kuwa Kampuni hiyo ya uchimbaji imeanza kutekeleza sheria ya madini inayoelekeza miezi sita kabla ya kuanza uchimbaji wawekezaji wanapaswa kuanza kulipa fidia.


Naye Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu alisema kuwa kampuni yake imeanza kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu mwezi Disemba 2016 ya kuwalipa wanufaika hao fidia ambayo ni hatua muhimu ya utekelezaji wa mradi huo.


Alisema kuwa malipo yanafanywa na kampuni hiyo chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya sambamba na wenyeviti wa serikali za vijiji vyote vilivyopo ndani ya mradi.


Kuanza kwa uchimbaji wa madini katika eneo hilo kutaibua ajira nyingi kwa wananchi Wilayani Ikungi na Taifa kwa ujumla jambo litakalosaidia ukuzaji wa pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.


Katika Awamu ya Kwanza Kampuni ya Shanta Gold Mining Ltd iliwalipa wanufaika 92 wenye umiliki wa Viwanja 121 thamani yake ikiwa ni Shilingi 902,412,247.00 Hulu awamu hii ya Pili wakilipwa Wamiliki 114 wenye Viwanja 156 vyenye thamani ya Shilingi 1,663,112,018.01


Aidha, Kuanzia leo Septemba, 2017 wanufaika wa fidia wameanza kufanya uhakiki wa malipo yao na ufunguaji Akaunti kwa ajili ya malipo ikiwa ni matakwa ya kisheria.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mang'onyi Ndg Mohamed H. Ramadhani alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kutoa maagizo ya kulipwa haraka fidia za kila wanufaika Jambo ambalo limetekelezeka kwa haraka katika kipindi Cha muda mfupi.


Sambamba na hayo aliongeza kuwa Mkuu huyo wa Wilaya anafanya kazi kubwa katika kuwaunganisha wananchi wote ili kupata stahiki zao na kufurahia Rasilimali za Nchi yao.
9. o.

JAFO: WATENDAJI MSILETE LELEMAMA USIMAMIZI MIRADI YA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki (CCM) Mhe Daniel Mtuka
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakikagua chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akitembelea na kukagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimshukuru Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo kwa ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua chumba cha dawa katika Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Mwingine ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu
  
Na Mathias Canal, Singida

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mhe Seleman S. Jaffo (Mb) amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida kuanza haraka Mradi wa Ujenzi wa Chumba Cha upasuaji, na Ujenzi wa wodi ya kisasa.

Naibu Waziri Jaffo ametoa maagizo hayo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa kituo Cha afya Kintinku mara Baada ya kutembele na kujionea uduni wa upatikanaji wa Huduma katika kituo hicho.

Alisema Mradi huo utaambatana na Ujenzi wa maabara kwa ajili ya vipimo kwa wagonjwa, Ujenzi wa eneo la kuchomea taka na Ukarabati wa eneo la kuhifadhia maiti.

Jafo ameonyesha kukerwa na ucheleweshwaji wa kuanza Ujenzi huo licha ya serikali kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2017/2018 zitakazotosha kukamilisha Ujenzi wote.

Alisema katika awamu ya Pili zitatolewa fedha kiasi cha shilingi milioni 220 zitakazotumika kununua vifaa vyote katika Chumba Cha upasuaji na vifaa tiba kwa ujumla.

Naibu Waziri Jafo alisema kitendo Cha kuchelewa kuanza Ujenzi huo kinachelewesha kuwapatia huduma bora wananchi ambayo inahubiriwa na serikali ya awamu tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli.

"Haiwezekani Rais anatoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya Afya halafu kuna watu wachache wanashindwa kusimama vizuri fedha Hizo Jambo ambalo linapelekea serikali kulaumiwa na wananchi" Alisema Jaffo

Katika hatua nyingine Mhe Jaffo alimuagiza mhandisi wa Maji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Vijijini Eng Gasto Mbondo kutekeleza mpango wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji kupitia Mradi wa kisima Cha Kintinku/Lusilile kilichopo Kijiji Cha Mbwasa (Mbwasa Well Field) kwani eneo Hilo linaonekana kuwa na maji ya kutosha.

Akikagua mradi huo Mhe Jaffo alisema tatizo kubwa kwa wananchi Ni pamoja na changamoto sugu ya upatikanaji Huduma za maji hususani vijijini na kukamilika kwa mradi huo utapunguza umbali na muda wanaotumia wananchi kutafuta maji. 

Awali Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Eng Gasto Mbondo akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji alisema kuwa Mradi huo wa maji wa Kintinku/Lusilile utakapokamilika unatarajia kuhudumia watu wapatao 45,417 kwa kuongeza 19.2% kutoka 42.1% iliyopo mpaka 61.3% na utakuwa na Vituo 81 vya kuchotea maji (DPs).

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utasimamiwa kwa karibu na ofisi yake ili kuongeza Hamasa na tija.

Pia alisema katika Mradi wa Ujenzi wa majengo kwa ajili ya kituo Cha Afya Kintinku asilimia kubwa ya mafundi watatoka katika Wilaya ya Manyoni ili kutoa ajira kwa wananchi husika.

MWISHO.

MARUFUKU SHULE MKOANI SINGIDA KUNUNUA CHAKI NJE YA MKOA-RC NCHIMBI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akishiriki zoezi la kutengeneza chaki katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Miraji Jumanne Mtaturu akiwa amebeba ili kuzianika chaki alizotengeneza Mkoa Singida Dkt Rehema Nchimbi katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akikagua kiwanda cha kutengeneza jasi cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Wafanyakazi wa kiwanda cha Dober Color wakifungasha chaki, Meneja wa Kiwanda hicho amesema sehemu ya kufungasha chaki hiyo inafanywa na wanawake kwakuwa wako makini na haraka.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amepiga marufuku Shule zote Mkoani Singida kuagiza chaki nje ya Mkoa kwakuwa kuna viwanda vinavyozalisha chaki bora mkoani hapa.

Dkt Nchimbi ametoa katazo hilo mara baara ya kufanya ziara katika viwanda viwili vinavyozalisha chaki katika halmashauri ya Itigi na kushuhudia chaki yenye ubora ikiwa imezalishwa kwa wingi na ikiwa haijapata soko.

“Hawa wenye viwanda wamejitahidi kuzalisha chaki bora haina vumbi na inauzwa kwa bei sahihi lakini shule zetu badala ya kuja kununua hapa ambapo ni karibu wanaagiza Dar es salaam na mikoa mingine”, amesema na kuongeza kuwa,

“Yani mnasubiri chaki hii hii iende Dar es Salaam halafu mnainunulia kutoka huko, hii haikubaliki, kuanzia leo shule zote zinunue chaki hapa hapa ili tupunguze gharama pamoja na kuinua viwanda vyetu”.Dkt Nchimbi ameongeza kuwa Mikoa ya Jirani itakayonunua chaki katika Viwanda vya Singida, vitasafirishiwa chaki hiyo bure kama motisha kwa kuunga mkono viwanda hivyo.

Amezitaka halmashauri kushirikiana katika kuboresha mazingira ya utendaji wa viwanda hivyo hasa kwa kuangalia namna ya kuboresha barabara zinazoenda katika machimbo ya jasi yanayotumika kutengeneza chaki kwakuwa wenye viwanda wamekuwa wakilalamikia ubovu wa barabara hizo.

MHE KINGU AWAOMBEA MAJI WAKAZI WA JIMBONI KWA LISSU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Ikungi mara baada ya kupita Ofisi za Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akielekea Manispaa ya Singida kwa ajili ya mapumziko, Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu (Kushoto) akimfatilia kwa makini Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe wakati wa kikao cha pamoja na watumishi wa Wilaya ya Ikungi, Mwingine ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Ikungi Ndg Elieza

Na Mathias Canal, Singida

Pamoja na Changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wananchi katika Jimbo la Singida Mashariki Wilayani Ikungi Mkoani Singida lakini uhaba wa upatikanaji wa huduma ya maji ni kikwaz kikubwa kwa wananchi kwani wanatumia umbali na muda mrefu kutafuta maji.


Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu ametoa ombi hilo mbele ya Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe wakati akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Ikungi kwenye kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu.

Mhe Kingu alisema kuwa Jimbo lake lina changamoto ya maji ambayo kwa kiasi kikubwa serikali inaendeleza juhudi za kuzitatua, huku akisema kuwa katika Jimbo jirani la Singida Mashariki linaloongozwa na Mhe Tundu Lissu hali ni mbaya zaidi katika upatikanaji wa miundombinu ya maji kwa wananchi wake.

Alisema kuwa hivi karibuni alipita katika jimbo hilo na kujionea adha inayowakumba wananchi jambo amablo lilimfanya kujipanga kuwaombea maji wananchi hao katika kipindi cha Bunge lijalo.

Alisema kuwa wananchi hao wamebaki wakiwa utadhani hawana muwakilishi wa Jimbo kwa kipindi cha miaka 10 jambo ambalo linafanya kuteseka na huduma za utafutaji maji kwa kutumia muda mwingi na umbali mrefu.

Aidha, Mhe kingu alisema kuwa pamoja na changamoto ya upatikanaji wa maji Katika Jimbo la Singida Mashariki lakini pia jimbo hilo linakumbwa na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu ambayo ni pamoja na uhaba wa vyumba vya madarasa, Nyumba za walimu, Maabara, Matundu ya vyoo na mabweni.

Hata hivyo alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kuanzisha mkakati wa pamoja wa kuanzisha Mfuko wa Elimu Ikungi utakaowashirikisha wananchi pamoja na wadau wa elimu kuchukua hatua madhubuti ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto na hatimaye kuwafanya wanafunzi waweze kuongeza ufaulu.

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe ameanza ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Singida ambapo atatembelea na kukagua Miradi ya Maji na vyanzo vya uboreshaji upatikanaji wa maji. 

MWISHO

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI SINGIDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe (Kulia) akizungumza jambo na Mwenyeji wake Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu mara baada ya kuwasili mkoani singida tayari kwa ziara ya kikazi ya siku nne.
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe (Mwenye suti nyeusi) akielekea kujionea Chanzo cha Mradi wa maji wa Kintinku/Lusilile katika Kijiji Cha Mbwasa Kata ya Makutupora, Tarafa ya Kintinku Wilayani Manyoni, kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Kushoto kwake ni Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki Mhe Daniel Mtuk.
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe alipotembelea Chanzo cha Mradi wa maji wa Kintinku/Lusilile katika Kijiji Cha Mbwasa Kata ya Makutupora, Tarafa ya Kintinku Wilayani Manyoni

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akizungumza jambo mara baada ya kutembelea Chanzo cha Mradi wa maji wa Kintinku/Lusilile katika Kijiji Cha Mbwasa Kata ya Makutupora, Tarafa ya Kintinku Wilayani Manyoni
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akikagua ujenzi wa eneo maalamu litakalotumika kwa ajili ya kuhifadhi umeme kwa ajili ya kusafirisha maji kuelekea katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Manyoni katika eneo la Mitoo.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza jambo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe kukagua utekelezaji wa ilani uchaguzi ya CCM 2015-2020
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akisisitiza jambo mbele ya wananchi, Kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu
Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe (Kulia) akisalimiana na wananchi wa Kitongoji cha Kaloleni mara baada ya kuwasili katika eneo hilo kujionea hali ya upatikanaji wa maji.
Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki Mhe Daniel Mtuka (Kulia) akizungumza jambo mbele ya Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe (Kushoto) wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua miradi ya vyanzo vya maji.
Mfereji wa Skimu ya Umwagiliaji kijijini Itagata ukiwa katika hatua nzuri za ujenzi
Bwala la Skimu ya Umwagiliaji lililogomewa na wananchi wa kijiji cha Itagata mara baada ya kubaini kuwa linavuja kutokana na mashimo yaliyopo yanayopelekea upotevu wa maji.

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Itagata, Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuhusu namna bora ya kukamilisha Mradi wa Ujenzi wa Bwala la Skimu ya Umwagiliaji.
 
Na Mathias Canal, Singida

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe ameanza ziara ya kikazi Mkoani Singida ambapo atatembelea na kukagua Miradi ya Maji na vyanzo vya uboreshaji upatikanaji wa maji.

Naibu Waziri Mhe Kamwelwe amepokelewa na Mwenyeji wake Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Ambaye Ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu katika Kijiji Cha Mbwasa Kata ya Makutupora, Tarafa ya Kintinku Wilayani Manyoni.

Mara Baada ya mapokezi hayo Mhe Naibu Waziri alianza shughuli ya kukagua Mradi wa chanzo cha maji Kintinku/Lusilile ambapo amewasihi wananchi kutunza mazingira hususani misitu ya asili kwani ndio chanzo cha upatikanaji wa maji.

Mhe Kamwelwe ameelekeza wananchi kulinda na kutunza vyanzo vya maji Sambamba na kutoa taarifa za uharibifu wa vyanzo vya maji na ukataji ovyo wa miti na uharibifu wa mazingira.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli imekusudia kufikia Mwaka 2020 wananchi waweze kupata maji kwa urahisi katika maeneo wanayoishi tofauti na hali ya upatikanaji wa maji kwa hivi Sasa kwa wananchi wanaotumia umbali mrefu kutafuta maji.

Aliwasihi wananchi kuvitunza vyanzo hivyo vya maji kwani pindi vitakapoanza kufanya kazi vitapunguza ukali wa uhaba wa upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Manyoni na Mkoa wa Singida kwa ujumla.

Alisema kuwa katika Bajeti ya kipindi Cha mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Vijijini imetengewa shilingi Milioni 611 huku eneo la Mamlaka ya Mji wa Manyoni ikiwa imetengewa zaidi ya Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya upatikanaji wa maji utakaopelekea Wilaya ya Manyoni kufikia 50% ya upatikanaji wa maji.

Mhe Kamwelwe aliwataka wakurugenzi kutekeleza miradi mbalimbali katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa ukarabati wa miradi ya maji, Uchimbaji wa visima virefu, na Ukarabati wa pampu zinazotumia upepo (Windmill).

Sambamba na hayo pia Mhe Naibu Waziri alikiri kuwa zipo changamoto mbalimbali zinazosababisha kutopatikana kwa maji ya kutosha ambapo ameahidi kuzifanyia kazi kwa haraka ambazo Ni pamoja na uchakavu wa miundombinu ya mabomba hasa eneo la usambazaji, Taasisi nyingi za serikali kutolipa Ankara zao za za maji, Kupandana kwa gharama za uendeshaji na Mamlaka kutokuwa na vyanzo vyake vya fedha.

Akiwa Kijijini Itagata, Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kutembelea Mradi wa Ujenzi wa Bwawa na Skimu ya Umwagiliaji, Mhe Naibu Waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe aliagiza Uongozi wa Umwagiliaji Kanda ya Kati Dodoma kufika Mjini Singida ndani ya siku mbili ili kubaini changamoto ya kukwama kwa Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Itagata lililokataliwa na wananchi kutokana na kuvuja kwake mnamo Septemba 2015 mara Baada ya kukamilika.

Mradi wa Ujenzi wa Bwala la Skimu ya Umwagiliaji katika Kijiji Cha Itagata ukikamilika utaweza kuhudumia Hekta zipatazo 160 katika eneo tambarare kwa ajili ya Kilimo Cha Umwagiliaji hususani zao la mpunga, Mazao ya Bustani na Vitalu vya kuoteshea Miche ya Tumbaku kwani eneo Hilo Lina udongo rafiki kwa Kilimo hicho.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa