Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Ni Mwenyekiti wa Bodi ya ESTL,Bi Rose Mjema akiwasilisha mada kwa washiriki wa mafunzo ya kupinga vitendo vya ukeketaji huku akitoa tahadhari juu ya madhara yatokanayo na vitendo hivyo vya ukeketaji.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).
Ni baadhi ya Mangariba na wakunga wa jadi kutoka katika Tarafa ya Mgori,wilayani Singida ambao wameamua kuachana na shughuli za kukeketa baada ya kupatiwa elimu na Shirika lisilokuwa la kiserikali la ESTL la Mkoani Singida,wakitoa ushuhuda kwenye uzinduzi wa mradi wa kutokomeza ukeketaji kwa wanawake katika Mkoa wa Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.
Na Jumbe Ismailly SINGIDA 
SHIRIKA
 lisilokuwa la kiserikali la Empower Society Transform Lives (ESTL) la 
Mkoani Singida limesema kwamba ukeketaji wa wanawake na watoto ni tatizo
 kubwa Afrika,Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi 28 zinazotajwa 
kuendeleza mila hiyo mbaya.
Hayo
 yalisemwa na Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo Mkoani Singida,Joshua Ntandu
 kwenye risala aliyosoma wakati wa uzinduzi wa mradi wa kutokomeza 
ukeketaji katika vijiji 14 vilivyopo katika kata za Itaja,Mgori,Ntonge 
na Ughandi,uliofadhiliwa na The Foundation For Civil Society na 
kufanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.
Aidha
 Ntandu alifafanua kwamba inakadiriwa kuwa Tanzania ina zaidi ya 
wanawake milioni 7.9 waliogundulika kuwa wamekeketwa huku Mkoa wa 
Singida ukishika nafasi tano za juu za mikoa inayoongoza kwa ukeketaji 
hapa nchini.
Alisema
 tafiti zinaonyesha pia kwamba vitendo hivyo vinaendelea kuongezeka 
katika Mkoa wa Singida na sababu kubwa zinazotajwa ni pamoja na imani 
kwamba ukeketaji ni sehemu ya makuzi ya mtoto wa kike na kwamba humzuia 
mtoto wa kike asiingie katika mahusiano ya mapenzi kabla ya kuolewa.Hata
 hivyo Ntandu alisisitiza kuwa jamii pia huamini kwamba ukeketaji ni 
tiba ya ugonjwa unaojulikana kama lawalawa kwa watoto wa kike (Vaginal 
or Urinary Tract Infection (UTI).
“Kadhalika
 kuna mbinu mpya ambayo imeshamiri ya ukeketaji wa watoto wachanga mara 
tu wanapozaliwa na kabla ya kufikia umri wa mwaka mmoja,na hii hufanywa 
ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya dola”alisisitiza
 Mtendaji mkuu huyo wa ESTL.
Akizindua
 mradi huo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida,Afisa Ustawi wa
 jamii wa Mkoa wa Singida,Shukurani Mbago,pamoja na kusikitishwa na 
mbinu mpya iliyoshamiri ya ukeketaji wa watoto wachanga,alizitaja baadhi
 ya sababu za kuongezeka kwa vitendo hivyo kuwa ni imani kuwa ukeketaji 
ni sehemu ya makuzi ya mtoto wa kike na kwamba kumzuia mtoto wa kike 
asiingie katika mahusiano ya mapenzi kabla ya ndoa.
“Jamii
 pia huamini kuwa ukeketaji ni tiba ya ugonjwa ujulikanao kwa jina la 
lawalawa kwa watoto wa kike mara tu wanapozaliwa na kabla ya kufikia 
umri wa mwaka mmoja.”alifafanua Katibu tawala huyo wa Mkoa.
Kwa
 upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya ESTL Mkoa wa Singida,Rose Mjema 
aliweka bayana kwamba mpaka sasa wameshaunda kamati za kutokomeza 
ukeketaji katika ngazi za vijiji na kata kutokana na watu waliopo katika
 ngazi hizo kuonyesha utayari wa kufanyakazi na wao.
Kwa
 mujibu wa Mjema wajumbe waliopo katika kamati hizo ni ni vijana tu kwa 
ngazi ya kata na vijiji,viongozi wa jadi,wakunga wa tiba asilia na 
wakunga wa jadi kwa kuwaandalia vikundi vya kupiga vita masuala ya 
ukeketaji kwenye maeneo yao.
Naye
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida,Elia Digha akizungumza 
na washiriki wa semina hiyo alishauri kwamba ili kukabiliana na vitendo 
hivyo kuanzia ngazi za serikali za vijiji pamoja na Halmashauri waanze 
kuandaa sheria ndogo itakayosimamia udhibiti wa ukeketaji katika 
Halmashauri ya wilaya hiyo.
0 comments:
Post a Comment