Home » » WANUFAIKA WA TASAF WAPANDE MIKOROSHO KUTUNZA MAZINGIRA NA KUJIONGEZEA KIPATO

WANUFAIKA WA TASAF WAPANDE MIKOROSHO KUTUNZA MAZINGIRA NA KUJIONGEZEA KIPATO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wasimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi hiyo.
Wasimamizi wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Singida (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi hiyo.
Mratibu wa Tasaf Mkoa wa Singida Patrick Girigo Kasango akiwa na Afisa Ufuatiliaji kutoka Tasaf Sinith Haule wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uwezeshaji wa kusimamia miradi ya ajira za muda kwa wasimamizi wa kutoka halmashauri na manispaa ya Singida.


Wanufaika wa mpango wa Kunusuru kaya masikini Tasaf, Mkoa wa Singida wametakiwa kupanda mikorosho ili waweze kutunza mazingira pamoja na kujiongezea kipato kutokana na zao la korosho.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya uwezeshaji kwa wasimamizi 67 wa miradi ya kutoa ajira za muda kwa wanufaika wa mpango wa Tasaf kutoka halmashauri na manispaa ya Singida.

Dkt Nchimbi amesema kutokana na kuwa ajira za muda kwa awamu hii zimelenga katika utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti hivyo amewataka Tasaf mkoa wa Singida kuwasiliana na Bodi ya Korosho waweze kupatiwa mbegu ili isipandwe miti mingine bali mikorosho.

Amesema kwa kufanya hivyo mkoa wa Singida utaweza kuwa mzalishaji mkubwa wa Korosho huku ajira hiyo ya muda ya kutunza mazingira kwa kupanda mikorosho, ikiwa imewatengenezea wanufaika hao ajira yao ya kudumu.

“Tukiweza kupanda mikorosho kwa zoezi hili la ajira za muda baada ya muda wanufaika hawa wataweza kuwa na kipato kikubwa kwa kuweza kuuza korosho zao, hii itakuwa ndio maana halisi ya mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo zinatakiwa pia zishiriki katika kukuza uchumi”, amesema na kuongeza kuwa,

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa