Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mmoja wa majeruhi akipatiwa matibabu ya mkono katika hospitali ya Mkoa wa Singida mara baada ya kupata ajali ya lori iliyoua watu 6 katika kijiji cha Kijota Singida.
 Mmoja wa majeruhi akiwa amelazwa huku akiendelea kupatiwa matibabu ya mkono katika hospitali ya Mkoa wa Singida mara baada ya kupata ajali ya lori iliyoua watu 6 katika kijiji cha Kijota Singida.
Baadhi ya ndugu na jamaa wa majeruhi wa ajali ya lori iliyoua watu sita wakiwa nje ya wodi za wagonjwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida.
Watu
 sita wamefariki dunia huku wengine 42 wakijeruhiwa baada ya lori lenye 
namba za usajili T.806 AEL aina ya scania mali ya Abdalla Mussa (39) 
mfanyabiashara mkazi wa Mwenge mjini Singida, kuacha njia na kupinduka 
katika Kijiji cha Kijota, Singida.
Kamanda
 wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora Magiligimba amesema ajali hiyo 
imetokea Agosti 27 mwaka huu saa 1.30 usiku katika kijiji cha Kijota 
wakati likitokea mnadani katika kijiji cha Mtinko Singida vijijini, 
likielekea Singida mjini.
ACP
 Magiligimba ametaja chanzo cha ajali kuwa ni uzembe wa dereva wa lori 
hilo Jumanne Kidanka (32) Kamanda huyo amesema kuwa chanzo cha ajali 
hiyo ni uzembe wa dereva ambaye hakuwa makini akiwa anaendesha lori hilo
 lililosheheni abira na mizingo mingi.
Amewataja
 waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni Haji Jumanne (35), Mikidadi 
Mohammed (40) wote wawili wakazi wa kijiji cha Mrama na Musa Salimu (30)
 mkazi wa kijiji cha Mwakiti.
ACP
 Magiligimba amewataja wengine kuwa ni Allen Mwangu (38) mkazi wa wilaya
 ya Ikungi, Lucas Stephano (40) mkazi wa kijiji cha Mrama na Sharifa 
Omari (19) mkazi wa kijiji cha Ilongero.
Ameongeza
 kuwa majeruhi 20 wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida, kumi 
wamelazwa hospitali ya misheni ya Mtinko na wanne ambao hali zao ni 
mbaya, wamelazwa katika hospitali ya misheni ya Hydom mkoani Manyara.
Ameeleza
 kuwa baadhi ya majeruhi walipatiwa matibabu na kurejea makwao huku 
wengine waliolazwa wamevunjika mikono, miguu na sehemu mbalimbali ya 
miili yao.
“Hawa
 wenye hali mbaya ni Fadhili Jumanne (33) mkazi wa Kibaoni mjini 
Singida, Mikidadi Hamisi, Jafari Hamisi na Idrisa Ibrahimu, wote 
wamevunjika miguu. Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye hospitali 
misheni Mtinko”, amesema.
0 comments:
Post a Comment