Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na madiwani na wakuu 
wa idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati wa Baraza Maalumu la 
kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali.
Baadhi
 ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakifuatilia hoja wakati
 wa Baraza Maalumu la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za 
Serikali. 
Katibu
 Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi (wa kwanza kushoto) na 
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula wakiandika baadhi ya maoni na
 maelekezo katika Baraza Maalumu la kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti
 wa Hesabu za Serikali.
Mkurugenzi
 wa Halmashauri ya Iramba Linno Mwageni akimshukuru Dkt Nchimbi kwa 
kuwakumbusha kuwajibika katika Baraza Maalumu la kujadili hoja za 
Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali.  
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akimkabidhi Mwenyekiti wa 
Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Simioni Tiyosera baadhi ya mashuka 
yaliyotolewa na Rais Magufuli kwa ajili ya halmashauri yake. 
Mganga
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba Boniphace Richard akimshukuru Rais Magufuli 
kwa kuwapatia mashuka, vitanda na magodoro ambayo yamesaidia kupunguza 
uhaba wa vifaa hivyo na kuwaboreshea mazingira ya kufanya kazi.
MADIWANI
 wametakiwa kuacha mzaha wa kuwachekea na kuwaendekeza watumishi ambao 
wamesababisha Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kupata hati chafu ya 
Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za Serikali katika kipindi cha miaka 
mitatu mfululizo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ameyasema hayo jana wakati wa 
baraza maalum la madiwani la kujadili hoja 122 za mkaguzi na mdhibiti wa
 hesabu za serikali katika halmashauri hiyo.
Dkt
 Nchimbi amewaambia madiwani kuwa wao ndio wazawa na ndio wawakilishi wa
 wananchi hivyo wanapozembea kuwasimamia na kuwabana watumishi ili 
wafuate kanuni, sheria na miongozo, watakaoumia ni wananchi wao pamoja 
na halmashauri yao kukosa ruzuku ya serikali.
“Madiwani
 acheni mzaha wa kuwachekea hawa watumishi, unapoona hoja ujue kiwanda 
ni watumishi, lakini mmepata hati chafu miaka mitatu mfululizo hamshtuki
 tu kuna watu wana wanawahujumu? Au mnaweza kujiendesha bila ya ruzuku 
ya serikali? Semeni leo? Wananchi wamewaamini hebu watumikieni 
ipasavyo,” amesema Dkt Nchimbi.
Ameongeza
 kuwa halmashauri inapoendelea kupata hati chafu hiyo ni sifa mbaya kwao
 na hata kwa mkoa mzima kwakuwa watendaji wa ngazi za mkoani mpaka 
halmashauri wanaonekana wameshindwa kutekeleza wajibu wao vema.
Dkt
 Nchimbi amesema madiwani waweke utaratibu ili wakuu wa idara 
waliothibitishwa wabaki katika halmashauri hiyo kwa kipindi kirefu 
kwakuwa wamekuwa wakithibitishwa kisha wanahama jambo linalowafanya 
wakose wakuu wa idara wa kutosha na kubaki na wanaokaimu.
“Kuna
 baadhi ya watumishi wanaharibu tu kwakuwa wanajua watahama hapo, lakini
 ninyi madiwani na wananachi hamtaweza kuhama hapo ndio kwenu hivyo basi
 wekeni utaratibu tu, mkuu wa idara akithibitishwa abaki hapo kwa muda 
awatumikie wananchi au akitaka kuhama basi atafute wa kubadilishana 
naye”, amesisitiza.
Aidha
 Dkt Nchimbi amewataka watumishi kuacha uzembe, watumie fursa zilizopo 
katika kujiongezea kipato lakini wasifanye biashara na halmashauri huku 
akiwashauri kuwasikiliza viongozi wa dini ambao wanawahimiza uadilifu na
 uchapa kazi.
Naye
 Mkaguzi wa Nje wa Hesabu za Serikali Annamary Kakunguru amesema baadhi 
ya watumishi wa halmashauri hiyo wamekuwa wazito katika kujibu hoja, 
kufuta hoja pamoja na kufuata maoni ya mkaguzi wa Nje hivyo 
kuisababishia halmashauri kuwa na hoja nyingi zinazodumu kwa muda mrefu.
Kakunguru
 amesema watumishi wanapaswa kubadilika na kuwa na utendaji mzuri pamoja
 na kupeana ushirikiano ili kwa pamoja waweze kufuta hoja na kuweka 
mikakati mizuri ya kuzuia hoja.
Pia
 Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi amewaasa watumishi
 kufanya kazi kwa kufuata miongozo, sheria na kanuni ili kuepuka 
kutengeza hoja huku wakuu wa idara wanaokaimu wakitakiwa kufanya kazi 
kwa bidii ili utendaji wao uonekane.
Lutambi
 ameongeza kuwa utendaji wa ushirikiano ndio utaifanya halmashaur hiyo 
kusonga mbele huku akiwaeleza kuwa hoja za mkaguzi wa hesabu za serikali
 zinawakumbusha kuongeza uadilifu na usimamizi wa fedha na shughuli za 
serikali.
Kwa
 upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Iramba Linno Mwageni 
amemshukuru Dkt Nchimbi kwa kuwakumbusha kuwajibika ili waendane na kasi
 ya awamu ya tano ya hapa kazi tu.
Mwageni
 amemweleza Mkuu huyo kuwa siku nyingine asisite kuwaonya pale 
wanapoenda tofauti huku akiahidi kwa niaba ya watumishi kubadilika na 
kuongeza bidii katika utendaji na usimamizi wao.
Wakati
 huo huo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amekabidhi kwa niaba
 ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli 
vitanda vya kuzalia vitatu, vya kawaida 20, mashuka hamsini na magodoro 
hamsini  vyenye thamani ya shilingi milioni 25 kwa hospitali na vituo 
vya kutolea huduma za afya Wilayani humo.
Dkt
 Nchimbi amesema Rais Magufuli ameonyesha upendo wake kwa wana Iramba 
hivyo wasiogope kutumia huduma za afya katika vituo vya serikali kwa 
kuwa sasa huduma zimeboreshwa, huku akiwaasa wakunga wa jadi wawaache 
wajawazito wakajifungulie hospitali na vituo vya afya.
Ameongeza
 kuwa watoa huduma na madaktari sasa wameboreshewa mazingira ya kufanyia
 kazi hiyo wanapaswa kutoa huduma kwa uadilifu mkubwa na kwa bidii.
Mganga
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba Boniphace Richard amemshukuru Rais Magufuli 
kwakuwa walikuwa na upungufu wa mashuka 400, ambapo jitihada za Rais 
zimewapatia mashuka 150 huku wakipanga kununua mashuka 200 kwa mapato ya
 ndani.
Jitihada
 za Rais Magufuli zimeungwa mkono na Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, 
Katibu Tawala wa Mkoa, Mwenyekiti wa halmashauri na madiwani, Mkurugenzi
 wa halmashauri na watumishi ambao kwa pamoja wamechangia mashuka 96, 
magodoro matano na pesa shilingi elfu hamsini.
0 comments:
Post a Comment