Mkurugenzi
 wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani Karmali na 
Mwenyekiti wa Mbao Fc Solly Zephania Njashi wakionyesha hati ya 
makubaliano ya Mkataba ikiwa ni mkataba wa udhamini wa timu hiyo kwa 
mwaka mmoja wenye thamani ya Milioni 140 sambamba na basi la wachezaji.
Mwenyekiti
 wa Mbao Solly Zephania Njashi akizungumza na waandishi wa habari baada 
ya kuingia makubaliano ya udhamini wa mkatabwa mwaka mmoja na na kampuni
 ya GF Trucks & Equipments wenye thamani ya Milioni 140, kushoto ni 
Mkurugenzi wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani 
Karmali 
Afisa 
Masoko wa Kampuni ya GF Trucks & Equipments Kulwa Bundala 
akizungumza na wanahabari baada ya kuingia mkataba na timu ya Mbao Fc 
wenye thamani ya Milioni 140 kwa mwaka mmoja.
Mkurugenzi
 wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani Karmali na 
Mwenyekiti wa Mbao Solly Zephania Njashi wakionyesha jezi za Mbao 
zitakazotumikia mwaka huu.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
UONGOZI
 wa klabu ya Mbao Fc umeingia mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya 
milioni 149 na kampuni ya GF Trucks & Equipments ikiwa ni udhamini 
wa timu hiyo kutoka Jijini Mwanza.
Kampuni
 hiyo imeridhishwa na maendeleo ya timu hiyo na kuamua kuwapatia 
udhamini kwani hawajawahi kushiriki katika udhamin i wa soka la Kiwango 
cha ligi kuu.
Mkataba
 huo uliosainiwa mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, 
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Imrani Karmali amesema kuwa mkataba 
huo ni wa kihistoria kwani unaenda kuleta na kukuza maendeleo ya mpira 
wa miguu nchini.
Karmal
 amesema kuwa, madhumuni makubwa ni kukuza vipaji vya mpira wa miguu na 
wanatarajiwa kuisaidia Mbao Fc kufikia malengo yao msimu huu, " 
tunafahamu usafiri umekuwa ni tatizo kwa klabu nyingi ndogo za Ligi Kuu 
na hicho kimetupelekea kuanza na basi msimu huu ambapo katika mkataba wa
 milioni 140 utajumuisha sambamba na basi hilo la wachezaji lenye 
thamani ya milioni 70,".
"uwezo
 waliouonesha katika ligi kuu na hata kuingia fainali ya kombe la FA 
ulituhamasisha kuifuatilia kwa ukaribu sana na tuna imani kwa msaada 
wetu Mbao itaendelea kufanya vizuri na si hao tu bali hata ajira kwa 
vijana zitaongezeka,"amesema Karmali.
Kwa 
upande wa Mwenyekiti wa Mbao Fc, Solly Zephania Njashi ameusifu mkataba 
huo na kusema kuwa utazidi kuleta chachu ya maendeleo katika klabu yao 
na hata kupunguza gharama za mahitaji kwa wachezaji.
Njashi
 ameishukurui kampuni ya GF Trucks & Equipments kwa mkataba huo na 
kuwaahidi mashabiki na wapenzi wa Mbao kuwa mwaka huu wataendelea 
kufanya vizuri na kuendelea kusalia katika Ligi kuu msimu ujao.
Baada 
ya kusaini mkataba huo, kampuni ya GF Trucks & Equipments i 
iliwakabidhi mfano wa jezi zitakazovaliwa na timu ya Mbao tayari zikiwa 
zimeshaweka nembo ya kamouni hiyo.
0 comments:
Post a Comment