Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Jeshi
 la Polisi Mkoani Singida, limefanikiwa kupunguza ajali za barabarani 
kutoka ajali 69 kwa kipindi cha mwaka 2016 hadi kufikia ajali 24 katika 
kipindi cha mwezi Januari mpaka Juni mwaka huu.
Hayo
 yamesemwa mwishoni mwa wiki na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa 
Singida, ACP Debora Magilingimba wakati akitoa taarifa ya uhalifu kwa 
Mkoa wa Singida ambapo amesema katika ajali hizo 24 zilisababisha vifo 
vya watu 29 na hapajakuwepo majeruhi kabisa.
ACP
 Magiligimba amesema kupungua kwa ajali kumetokana na Jeshi hilo kutoa 
elimu ya usalama barabarani mara kwa mara hasa katika maeneo ya 
vijijini, mitaani na hata katika mafunzo ya udereva.
Ameongeza
 kuwa jeshi hilo limekuwa likithibiti mwendo kasi katika barabara kuu, 
kuthibiti ulevi kwa upimaji wa kilevi kwa madereva wote wa vyombo vya 
usafiri na hivyo kupelekea ajali kupungua sana kwa Mkoa wa Singida.
“Pia
 tumeendelea kutoa elimu ya usalama barabarani mashuleni, vyuoni na 
katika  nyumba za ibada. Lengo ni kuiongozea jamii uelewa zaidi unaohusu
 masuala yote ya ulinzi na usalama, na sheria za usalama barabarani”, 
amefafanua.
Aidha,
 ACP Magiligimba amesema makosa madogo yamepungua kwa asilimia 0.8 
ambapo jumla ya makosa madogo 22,222 yameripotiwa katika kipindi cha 
januari hadi juni mwaka huu, ikilinganishwa na makosa kama hayo 22,403 
yaliyotokea kipindi kama hicho mwaka jana.
“Katika
 makosa hayo madogo, jumla ya wakosaji 21,836 walilipa faini mbalimbali 
zaidi ya shilingi milioni 655. Katika kipindi kama hicho mwaka jana 
jumla ya wakosaji 21,778 walilipa faini mbalimbali zaidi ya shilingi 
milioni 653.3. Faini hizo ni sawa na ongezeko la asilimia 0.3”, amesema 
kamanda huyo.
ACP
 Magiligimba ametaja baadhi ya mikakati mbalimbali ya 
kukabiliana/kupunguza zaidi uhalifu, wahalifu na ajali za barabarani 
kuwa ni kuendelea kutoa elimu ya usalama barabarani kupitia vyombo vya 
habari na kushirikiana na asasi mbalimbali katika kutoa elimu na 
matengenezo ya barabara.
“Vile
 vile tutaendelea kuimarisha ushirikiano zaidi na asasi zisizo za 
kiserikali, ikiwemo World Future Vocation, mabalozi wa usalama 
barabarani na SUMATRA. Pia tutashirikiana na TANROADS, halmashauri za 
wilaya na manispaa kushauriana namna ya kufanya matengenezo ya barabara 
katika maeneo yaliyoharibiwa au yenye kusababisha ajali za mara kwa 
mara”, amesema ACP Magiligimba.
0 comments:
Post a Comment