Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkazi
 wa kijiji cha Shiponga, Hanang Mkoani Manyara anayedaiwa kuwa jambazi, 
Hamisi Athumani (32), amefariki dunia baada ya kupigwa risasi kiunoni na
 askari polisi wakati akiwa katika harakati ya kutoroka.
Kamanda
 wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa, ACP Debora Magiligimba, amesema tukio 
hilo limetokea Agosti 25 mwaka huu saa nane mchana, huko katika kijiji 
cha Mgori tarafa ya Ngimu wilaya ya Singida.
Amefafanua
 kuwa Hamisi (marehemu) alipigwa risasi na askari polisi wakati 
akijaribu kuwatoroka mara baada kuonyesha bunduki aina ya rifle yenye 
namba 7358 na risasi zake tano.
Amesema
 bunduki hiyo iliyokuwa imekatwa mtutu na risasi zake tano zilikuwa 
zimefichwa kwenye soksi, vitu hivyo vilikuwa vilihifadhiwa kwenye mfuko 
wa sandarusi, na kufichwa chini ya jiwe.
ACP
 Magiligimba amesema Agosti 23 mwaka huu, mtuhumiwa alikamatwa na 
wananchi wa kijiji cha Ngamu, na kufikishwa katika kituo cha polisi cha 
kijiji hicho kwa tuhuma ya kujihusisha na matukio ya ujambazi.
“Kesho
 yake mtuhumiwa alihojiwa na kukiri kujihusisha na matukio ya ujambazi 
wa kutumia silaha katika mikoa mbalimbali. Pia aliahidi kuwapeleka 
askari kuwaonyesha mahali alikoificha silaha anayoitumia kwenye matukio 
hayo ya ujambazi,” amesema ACP Magiligimba.
Kamanda
 huyo amesema Agosti 25 mwaka huu saa sita mchana, askari polisi wakiwa 
na mtuhumiwa, walikwenda katika pori la kijiji cha Mgori mahali 
alipokuwa ameficha bunduki hiyo aina ya rifle.
“Mara tu baada ya kuwaonyesha askari hao silaha hiyo na wakati askari wanaendelea kufanya upekuzi katika eneo hilo, mtuhumiwa alijaribu kutoroka askari kwa kukimbia” amesema na kuongeza.
“Askari
 mmoja alifyatua risasi tatu hewani akimtaka asimame, lakini hakutii. 
Ndipo alipompiga risasi moja iliyompata sehemu ya kiunoni”.
Amesema
 jereha hilo la risasi lilisababisha mtuhumiwa Hamisi avuje damu nyingi,
 na hivyo kufariki dunia wakati akikimbizwa hospitali ya mkoa kwa 
matibabu.
“Jeshi
 la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kutoa wito kwa wananchi waote 
kutoa taarifa zitakazosaidia kubaini wahalifu katika maeneo yao ili 
hatua ziweze kuchukuliwa kudhibiti vitendo vya kihalifu,” amesema kamanda huyo.

0 comments:
Post a Comment