MRATIBU WA UN NCHINI, ALVARO RODRIGUEZ ZIARANI MKOANI SINGIDA KUKAGUA MIRADI YA SHIRIKA HILO‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
IMG_4020
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone alipomtembelea na kufanya mazungumzo ofisini kwake jana mjini Singida.
Na Modewjiblog team, Singida
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Parseko Kone ofisini kwake kwa ajili ya kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mkoani humo.
Mratibu huyo yupo Mkoani hapa kwa siku mbili kukagua miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Katika siku yake ya kwanza atatembelea mradi wa afya ambao unashughulikia watu wanaoishi na VVU katika kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi. Pia atatembelea kikundi cha ufugaji nyuki kinachojihusisha na uzalishaji wa asali na utengenezaji wa mishumaa.
Aidha akiwa kijiji cha Puma atatembelea kambi waliokolazwa watu wenye ugonjwa wa Kipindupindu.
Katika ukaguzi wa miradi hiyo Mratibu huyo atapata nafasi ya kuzungumza na walengwa wa miradi hiyo ili kupata mafanikio na changamoto zilizojitokeza.
Katika siku yake ya pili na ya mwisho mkoani Singida Bw. Alvaro Rodriguez atatembelea mradi mkubwa wa ufugaji nyuki kisasa unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP).
Baada ya hapo atatembelea ujenzi wa hospitali ya rufaa inayoendelea kujengwa kijiji cha Mandewa nje kidogo ya mji wa Singida.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone alitoa Shukrani kwa Umoja wa Mataifa kwa misaada yake ya kuisaidia serikali katika kutatua kero mbalimbali za wananchi.
Hata hivyo ameomba Mashirika hayo yaendelea kusaidia katika Nyanja za upatikanaji wa ajira kwa vijana na masoko kwa wakulima.
Mratibu huyo baada ya kumaliza ziara yake mkoani Singida ataelekea mkoa wa Tabora ambapo ataanza ziara yake tarehe 3 mwezi Desemba na baada ya kumaliza mkoa wa Tabora atelekea mkoani Kigoma tarehe 4 hadi 6 nwezi Desemba.
Singida ni kati ya mikoa itakayounufaika na mpango mpya wa malengo ya maendeleo endelevu (Sustainable Development Goals-SDGs) unaotarajiwa kuanza kutekelezwa 2016-2030.
IMG_4026
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone akisalimiana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kulia) aliyeambatana na Bw. Rodriguez. Aliyeketi ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe.
IMG_4039
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa kwanza kulia) akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (wa tatu kushoto) pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mkoani humo. Wa kwanza kushoto ni Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes. wengine pichani ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa kwanza kulia).
IMG_4034
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone akisoma baadhi ya mambo yaliyomo kwenye kitabu cha 'Mwongozo wa wadau wa kilimo na mifugo' kilichoandaliwa na ofisini kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani). Kulia ni Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe.
IMG_4042
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akitoa maelezo ya lengo namba 3 ambalo ni 'Afya Njema na Ustawi' wakati wa kutambulisha malengo mapya ya maendeleo endelevu (Sustainable Development Goals-SDGs) kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone walipomtembelea ofisini kwake jana.
IMG_4065
Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe akioorodhesha mambo muhimu yanayotakiwa kufanyika katika mkoa wa Singida ili kufanikisha utekelezaji wa lengo namba 3 ambalo ni 'Afya Njema na Ustawi' kati ya malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) yanayotarajiwa kuanza kutekelezwa 2016-2030. Wanaoshuhudia tukio hilo kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan.
IMG_4072
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa kwanza kulia), Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa pili kulia) pamoja na Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes (wa tatu kushoto) wakimkabidhi Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez bango hilo lenye mambo muhimu yanayotakiwa kufanyika katika mkoa wa Singida ili kufanikisha lengo namba 3 kati ya malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) aliyeambatana kwenye ziara hiyo na Afisa a Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (katikati kulia).
IMG_4080
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (wa pili kulia), Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) kwenye bango maalum lenye rangi mbalimbali zinazowakilisha malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) yanayotakiwa kumfikia kila mwananchi nchini kwa ajili ya utekelezaji.
IMG_4086
Kutoka kushoto ni Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Mdala Fedes, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Festo Kang'ombe, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Katibu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bw. Sute pamoja na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan.
IMG_4096
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone (katikati) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu huyo wa mkoa.
IMG_4092
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone.
......AKIWA NJIANI KUELEKEA MKOANI SINGIDA......
IMG_3987
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwa ameambatana na Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (kulia) mara baada ya kusimamisha gari maeneo ya Babati mjini.
IMG_3988
Neema Mikaeli (22)akihamaki kuona watu waliokuwa wakimsogelea (hawapo pichani) katika eneo alilokuwa akifua nguo kwenye dimbwi la maji machafu ya mvua kama yanavyoonekana pichani.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini akiwa njiani kuelekea mkoani Singida alishtushwa kuona mkazi mmoja wa Babati mjini Neema Mikaeli (22) akifua nguo kwenye dimbwi la maji machafu ya mvua na kusimama na kuzungumza nae ambapo aligundua kuna tatizo la maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo pamoja na ukataji miti ambao unapelekea kuharibu mazingira.
Katika mazungumzo ya Neema alisema kuwa kuna mabomba ya maji yaliyowekwa zaidi ya miaka 3 sasa lakini hayatoi maji na hivyo kupelekea wao kutembelea umbali mrefu ambao kuna mto na wanatumia maji ya mto huo kupikia na kunywa.
Akiongea na Mikaela alimuhakikishia kwamba Umoja wa Mataifa utazidi kufanya kazi ka ukaribu na serikali ya Tanzania sambamba na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
IMG_3995
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Ofisa kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu wakizungumza na Mkazi huyo wa wilaya ya Babati mjini mkoani Manyara, Neema Mikaeli (22) aliyekuwa akifua nguo zake kwenye dimbwi hilo kutokana na kukosekana kwa maji katika eneo lao.
IMG_4000
Haya ndio maji ambayo hata sabuni ya unga haikolei yaliyokutwa yakitumiwa na Neema Mikaeli (22) (hayupo pichani) kufulia nguo zake.
IMG_3983
Neema Mikaeli (22) akiwa kwenye eneo la dimbi la maji ya mvua akiendelea kufanya usafi wa nguo zake.

MO APATA TUZO NYINGINE, ADHIHIRISHA TAMAA YA KUWATUMIKIA WATANZANIA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
IMG_3351
Mfanyabiashara maarufu ambaye pia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akitembea kwenye 'Red Carpet' mara baada ya kuwasili katika hotel ya Hilton Sandton jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwenye hafla ya utoaji tuzo iliyoandaliwa na jarida maarufu la Forbes na kutunukiwa tuzo ya "Forbes Africa Person Of the Year 2015".(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Na Modewjiblog team
MFANYABIASHARA na mtu mwenye taasisi ya kusaidia jamii, Mohammed Dewji maarufu kama Mo ametunukiwa tuzo ya jarida maarufu la Forbes ya "Forbes Africa Person Of the Year 2015" katika hafla iliyofanyika Novemba 27 mwaka huu jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mfanyabiashara huyo pia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Mohammed Enterprises T Ltd (MeTL Group) kampuni iliyoanzishwa na na baba yake katika miaka ya 1970 ambayo sasa imekua na kujikita katika viwanda vya nguo, usagaji nafaka, utengenezaji wa vinywaji baridi, usindikaji wa mafuta ya kula, usindikaji wa chai na kuendesha mashamba ya mkonge ambapo tayari anashea ya asilimia 40 ya soko.
Mo ametwaa tuzo hiyo kwa kuwashinda watu watano mashuhuri barani Afrika. Watu hao ni Nkosazana Dlamini Zuma, mke wa Kwanza wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma. Mama huyo kwa sasa ndiye Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU). Mwingine ni Rais wa sasa wa Nigeria, Muhammadu Buhari aliyetambuliwa kutokana na kuanzisha vita dhidi ya rushwa nchini mwake.
Aidha wapo Arumna Otei, mchumi mahiri raia wa Nigeria ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia. Pia alikuwemo Mwandishi maarufu wa vitabu wa Nigeria, Chimanda Ngozi Adichie ambaye moja ya vitabu vyake vinaelezea picha halisi ya Afrika inavyofikiriwa duniani.
Akitoa neno la shukurani baada ya kukabidhiwa kwa tuzo hiyo Mo, alisema anatoa tuzo hiyo kwa vijana wa Kitanzania kwani ndio nguvu kazi inayobeba uchumi wa nchi.
Mo ambaye kampuni yake ya MeTL inaongoza kwa kutoa ajira nchini, ikiwa imetoa ajira 26,000 kote katika viwanda vyake 31 vilivyopo nchini na katika mataifa matano ya Afrika, alisema amefurahishwa na tuzo hiyo ambayo anaitoa kwa vijana kwa kutambua pia wajibu mkubwa walionao katika kukabiliana na umaskini.
IMG_3317
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akifurahi jambo na baadhi ya wageni waalikwa nje ya ukumbi wa hafla hiyo ya utoaji tuzo iliyoandaliwa na jarida la Forbes.
Alisema ajira 26,000 zimegusa watu wengi nchini na kwamba ana matumaini makubwa ya siku za usoni kutoa ajira zaidi kutokana na biashara zake kuendelea kukua.
"Heshima yangu kubwa haitokani na utajiri, maana kama utajiri wako hauna msaada wala kugusa watu masikini hauna maana yeyote, hivyo basi heshima hii ni kutokana na kwanza bidhaa zangu kugusa maisha ya watu kila siku kuanzia sukari na majani ya chai asubuhi pamoja na unga wa ngano, lakini pia chakula cha mchana kwa unga wa sembe, mafuta ya kupikia na maji ya kunywa, bidhaa zote hizo za Mohammed Enterprises zinagusa maisha kila nyakati katika siku.
"Nina viwanda 31 ambavyo vimekuwa vikitengeneza bidhaa za Kitanzania na kuziuza kwa Watanzania kwa bei yenye unafuu mkubwa, mathalani tunauza maji kwa bei chini ya dola moja kwa shilingi za Kitanzania 200, hakuna hata Ulaya, nina kiwanda cha khanga na vitenge ambacho malighafi zake zote ni za Kitanzania, hivyo kuna kusaidia serikali kwa kulipa kodi ipasavyo, lakini pia kusaidia moja kwa moja ajira za Watanzania walio wengi ambao tatizo lao kubwa katika kundi la vijana ni ajira"
Alitumia fursa hiyo kumshukuru na kumpongeza baba yake kwa kumwita mjasiriamali shujaa ambaye alitoka kuanzia dereva wa malori baada ya kuhitimu kidato cha nne mwishoni mwa miaka ya 1960 hadi kufikia ubilionea. Alisema alipata maono ya utajiri hasa kutoka kwa baba yake huyo aliyekuwa akimshirikisha biashara tangu akiwa mdogo.
“Mwanaume mwenye ndoto huhitaji mwanamke mwenye maono. Na nimebarikiwa mwanamke ambaye kwa miaka 15 amekuwa akinipa sapoti isiyoyumba.
IMG_3362
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akibadilishana 'Business card' na mmoja wa wageni waalikwa katika hafla hiyo.
“Saira, nina shukurani nyingi kwako kwa kuwa nguzo ya familia yetu, mama wa heshima kwa watoto wetu watatu,” alisema Mo kwenye hafla hiyo.
Kwa utulivu, Mo alisema: “Baba, zawadi kubwa ambayo ulinipa katika maisha yangu ni muda wako, na kwa hilo nitakuwa mwenye deni la shukurani kwako siku zote za maisha yangu.”
Mo ambaye moyo wake wa binadamu ulimfanya awanie uwakilishi Jimbo la Singida Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kushinda nafasi hiyo na hivyo kuwawakilisha wanasingida kuanzia 2005 na 2015 amesema maisha ni changamoto kubwa inayobadilishwa kwa utumishi wenye nia ya dhati kwa umma.
Alisema alipowania uwakilishi alikuwa na sababu: “Nilikuwa na umri wa miaka 24, nilikwenda Singida kutoa heshima kwenye kaburi la marehemu babu yangu. Sikuwa nimefika huko tangu nilipoondoka nikiwa na umri wa miaka mitatu.
“Nilipokuwa njiani, nilimuona mzee akiwa na maji yenye rangi ya njano, machafu ambayo aliyatumia kwa kunywa. Nilishangaa, maana hali ile sikuwahi kufikiri kama ipo vile. Kipindi hicho nilikuwa nimemaliza Chuo Kikuu cha Georgetown, Marekani.”
Mo anasema kuwa aliingiwa na hisia kutaka kujua nini hasa alichokuwa anahitajika kufanya, alimfuata yule mzee aliyekuwa na maji yale, alipozungumza naye, aliwazungukia watu wengine na kuridhika kuwa ile ndiyo hali halisi, hapo ndipo fikra ya kwa nini agombee ubunge ilipoanzia.
Anasema kuwa baada ya kujiridhisha hivyo, alirudi kwa mzee wa kwanza, alizungumza naye na kumuuliza ni kwa nini shida ile ilikuwa haizungumzwi kwa upana katika mamlaka husika.
IMG_3434
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji pamoja na ujumbe wake alioambatana nao kutoka Tanzania.
“Nilipojitambulisha yule mzee alisema anamkumbuka babu yangu, kisha akanishauri nigombee ubunge, alinisisitiza mno ili nisaidie kuondoa lile tatizo la watu wa Singida kunywa maji machafu,” alisema Mo.
Anaeleza kuwa alipokuwa njiani kurejea Dar es Salaam, alilifikiria tatizo hilo kwa mapana zaidi, akalifanyia utafiti na kubaini kwamba katika kila watu 10, watatu walikuwa wakipoteza maisha kutokana na maradhi yanayosababishwa na maji machafu.
Anaendelea kusema kuwa aligundua kuwa Singida kulikuwa na tatizo kali la maji safi na salama. Anasema kuwa alibaini uwepo wa tatizo la elimu kuhusu matatizo ya maji.
Jambo lingine ambalo anasema aliligundua ni uwepo wa tatizo la huduma za afya. “Niliwafikiria watoto wangu, jinsi ninavyowapenda, na namna ambavyo kila mzazi anavyompenda mwanaye. Nilipingana na hali kuwa watoto wa Uingereza na Marekani wamependelewa zaidi. Maisha ni sawa bila kujali chochote,” anasema Mo.
IMG_3359
Sehemu ya ujumbe kutoka Tanzania uliombatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji kwenye hafla hiyo.
“Niliona lazima nitimize wajibu wangu. Kutimiza malengo yangu ya kusaidia jamii, kufanikiwa katika biashara. Mambo hayo mawili hisani na biashara nimeyaweka pamoja na ndiyo maana nimefika hapa leo, tunajivunia sana kuitwa METL nembo ya Watu. Katika miaka yangu 10 kama mbunge, nimefanya mabadiliko mengi. Nilikuwa na sababu ya kupata mkopo nafuu wa dola milioni 35, ambao ulisababisha kuwekwa kwa miundombinu ya maji safi na salama Manispaa ya Singida.
“Niliitumia MeTL, tuliweza kudhamini shughuli nyingi za maendeleo ya kijamii. Kuhusu elimu, nilifanikisha kujenga shule 15, zikawa 17, kabla ya hapo tulikuwa na shule mbili tu. “Kuhusu huduma za afya, hapa nimshukuru mke wangu kwa jitihada zake. Alikuwa Mwenyekiti wa taasisi ya Tumaini la Maisha ambayo imekuwa ikisaidia watu wengi, hasa watoto dhidi ya maradhi ya saratani.”
IMG_3469
Burudani mbalimbali zikiendelea ukumbini hapo.
IMG_3548
Mkurugenzi Mtendaji wa Jarida la Forbes Afrika, Sid Wahi akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa. Kulia ni Head of Events wa ABN Productions, Alexander Leibner.
DSC_4663
Mwanzilishi na mchapishaji wa jarida la Forbes Afrika, Bw. Rakesh Wahi ( wa pili kushoto) akikamkabidhi Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji (wa pili kulia) tuzo ya Heshima Barani Afrika "2015 Forbes Africa Person of the Year" iliyotolewa na Jarida la Forbes Afrika kwa kutambua mchango wake katika kusaidia jamii ikiwemo kutoa ajira kwa zaidi ya watu 26,000 nchini na mambo mengine yanayoigusa jamii. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Mtendaji wa Forbes Afrika, Sid Wahi (kulia) na MEC Panyaza Lesufi kutoka kitengo cha elimu, Gauteng Province (kushoto).
IMG_3780
Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akitoa neno la shukurani baada ya kukabidhiwa kwa tuzo, alisema anatoa tuzo hiyo kwa vijana wa Kitanzania kwani ndio nguvu kazi inayobeba uchumi wa nchi.
IMG_3776
IMG_3825
MO akiteta jambo na Mchumi mahiri raia wa Nigeria ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia, Arunma Oteh (kulia) ambaye walikuwa pamoja kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo hiyo ambapo pia alimpongeza sana.
IMG_3849
Pichani juu na chini MO akiendelea kupongezwa na wadau mbalimbali walioalikwa kwenye hafla hiyo.
IMG_3866
IMG_3875
Pongezi kwa MO zikiendelea kutolewa.
IMG_3889
IMG_3857
MO katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Jaguar Land Rover ambao ni miongoni mwa wadhamini wa sherehe za tuzo hizo.
IMG_3940
MO katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais wa Makampuni ya MeTL Group, Vipul Kakad mara baada ya kutwaa tuzo hiyo.
IMG_3925
Makamu wa Rais wa MeTL GROUP, Vipul Kakad na Shemane Amin wakipitia moja ya taarifa iliyowavutia kwenye jarida la Forbes Afrika.
IMG_3911
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Jaguar Land Rover ya Afrika Kusini wakipozi kwenye 'Red Carpet'.

MUULIZE MO!: TUANDIKIE MASWALI YAKO KUMUULIZA MOHAMMED DEWJI (CEO WA METL GROUP) TUTAKUWA NA MAHOJIANO NAYE HIVI KARIBUNI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
mo
Msomaji na mdau wa mtandao wako wa habari www.modewjiblog.com unakupa nafasi wewe kumuuliza maswali/swali lolote lile Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL Group, Mohammed Dewji. Maswali yote yatajibiwa na kutolewa ufafanuzi wa kina. Tutakuwa na mahojiano naye karibuni. Asanteni sana.
Utaratibu wa kumuuliza maswali ni kwa kukomenti kwenye post hii kisanduku cha maoni, Zingatia Kanuni na sheria ikiwemo kutotumia lugha zisizo rasmi.
Pia waweza kutoa maoni yako kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ukiwemo ukurasa wa Mohammed Dewji : https://www.facebook.com/mohammeddewjitz/
au Ukurasa wa Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL):https://www.facebook.com/MeTLGroup/photos

Polisi Singida yapiga marufuku maandamao ya UKAWA kupinga ushindi wa Rais mteule Dk. Magufuli

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
RPC
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Singida, Thobias Sedoyeka akizungumza na waandishi wa habari juu ya kupinga maandamano ya vyama vinavyounda Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupinga matokeo ya tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kumtangaza Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli.
Na Hillary Shoo, SINGIDA
JESHI la polisi Mkoani Singida limepiga marufuku maandamano yanayotarajiwa kuandaliwa na kufanyika chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ya kupinga ushindi wa Rais Mteule John Magufuli katika Wilaya zote za Mkoa huo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo, Kamanda wa Polisi (ACP) Thobias Sedoyeka alisema kuwa polisi wamepata taarifa za kiintelijensia kuwa (kesho) leo kuwa vyama hivyo chini ya mwavuli wa UKAWA, viko katika mipango ya chini kwa chini ili kufanya maandamano ya kupinga matokeo hayo ya Urais.
“Uchunguzi huo unaonesha kuwa maandamano hayo yatashirikisha makundi mbalimbali ya watu hususan zaidi vijana na kupita sehemu mbalimbali za Miji kabla ykuhitimishwa katika ofisi za CHADEMA Mkoa wa Singida.” Alisema Kamanda Sedoyeka.
“Sisi Jeshi la polisi Mkoani Singida tunasema kuwa maandamano hayo ni batili na hatuyaruhusu kwa namna yoyote ili huku tukiwataka viongozi wa vyama hivyo kutofanya hivyo kamwe na badala yake watumie njia stahiki za utawala wa kisheria ikiwemo kwenda kwenye vyombo ambavyo vinawajibika kushughulikia malalamiko yao.” Alisisitiza.
SEDOYEKA
RPC Singida Thobias Sedoyeka.
Hata hivyo alionya vijana kutojihusisha na maandamano hayo na badala yake waendelee na kazi zao za uzalishaji mali kwani jeshi la polisi halitasita kutumia nguvu za ziada pale itakapobidi kitendo ambacho huenda kikaathiri utendaji kazi wao pamoja na watu wengine ambao hawatahusika na maandamano hayo.
Hata hivyo Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Singida, Shaban Limu alisema walipeleka barua kwa OCD wa Wilaya zote za Mkoa wa Singida juu wa kufanya maandamano hayo ya amani, lakini wamezuiwa kufanya hivyo na Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Singida.
Aidha Limu alisema hivi sasa wanawasiliana na makao makuu ya CHADEMA, kupinga amri hiyo ya Kamanda wa polisi Thobias Sedoyeka kwani kikatiba ni halali kufanya maandamano bila kuvunja sheria za nchi, kwani kazi ya polisi ni kuwalinda wakati wakiandamana.
limu
Mwenyekiti wa (Chama cha CHADEMA) Mkoa wa Singida, Shaban Limu akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Singida juu ya hatua yao ya kupinga amri ya Kamanda wa polisi Mkoani humo Thobias Sedoyeka ya kuzuia maandamano yao kupinga ushindi wa Dkt. John Magufuli .
ofisi
Ofisi za CHADEMA Mkoa wa Singida (PICHA ZOTE NA HILLARY SHOO).
Mo Blog

TANGAZAO KWA WASAMALIA WEMA: MTOTO CAREEN ANAHITAJI MSAADA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mtoto Careen Modest Kassuw pichani, ana umri wa mwaka mmoja, amezaliwa ana tatizo la Moyo ukiwa na matundu mawili na valvu zake nyembamba  zimebana kiasi  hivyo analazimika kusafirishwa kwenda India kwa matibabu.

Wazazi wa mtoto huyo wanaomba msaada wako wewe Mtanzania kwa atakayeguswa ili wafanikishe gharama za matibabu ya mtoto Careen ambayo ni Shilingi Milioni 30 zinahitajika ili kuokoa maisha yake.
Ewe Mtanzania, ewe mzazi tunaomba mchango wako wa hali na mali, kwa atakayeguswa tunaomba utume mchango wako kwa mama mzazi wa mtoto huyo Eunice kwa namba0713 034866 au kwa namba 0715 083055
Mungu awabariki wote mtakaochangia kwa njia moja au nyingine.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa