Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kamanda
 wa Jeshi la Polisi Mkoani Singida, Thobias Sedoyeka akizungumza na 
waandishi wa habari juu ya kupinga maandamano ya vyama vinavyounda 
Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupinga matokeo ya tume ya Taifa ya Uchaguzi 
(NEC) kumtangaza Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. 
John Pombe Magufuli.
Na Hillary Shoo, SINGIDA
JESHI
 la polisi Mkoani Singida limepiga marufuku maandamano yanayotarajiwa 
kuandaliwa na kufanyika chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ya 
kupinga ushindi wa Rais Mteule John Magufuli katika Wilaya zote za Mkoa 
huo.
Akizungumza
 na waandishi wa habari ofisini kwake leo, Kamanda wa Polisi (ACP) 
Thobias Sedoyeka alisema kuwa polisi wamepata taarifa za kiintelijensia 
kuwa (kesho) leo kuwa vyama hivyo chini ya mwavuli wa UKAWA, viko katika
 mipango ya chini kwa chini ili kufanya maandamano ya kupinga matokeo 
hayo ya Urais.
“Uchunguzi
 huo unaonesha kuwa maandamano hayo yatashirikisha makundi mbalimbali ya
 watu hususan zaidi vijana na kupita sehemu mbalimbali za Miji kabla 
ykuhitimishwa katika ofisi za CHADEMA Mkoa wa Singida.” Alisema Kamanda 
Sedoyeka.
“Sisi
 Jeshi la polisi Mkoani Singida tunasema kuwa maandamano hayo ni batili 
na hatuyaruhusu kwa namna yoyote ili huku tukiwataka viongozi wa vyama 
hivyo kutofanya hivyo kamwe na badala yake watumie njia stahiki za 
utawala wa kisheria ikiwemo kwenda kwenye vyombo ambavyo vinawajibika 
kushughulikia malalamiko yao.” Alisisitiza.
RPC Singida Thobias Sedoyeka.
Hata
 hivyo alionya vijana kutojihusisha na maandamano hayo na badala yake 
waendelee na kazi zao za uzalishaji mali kwani jeshi la polisi 
halitasita kutumia nguvu za ziada pale itakapobidi kitendo ambacho 
huenda kikaathiri utendaji kazi wao pamoja na watu wengine ambao 
hawatahusika na maandamano hayo.
Hata
 hivyo Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Singida, Shaban Limu alisema 
walipeleka barua kwa OCD wa Wilaya zote za Mkoa wa Singida juu wa 
kufanya maandamano hayo ya amani, lakini wamezuiwa kufanya hivyo na 
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Singida.
Aidha
 Limu alisema hivi sasa wanawasiliana na makao makuu ya CHADEMA, kupinga
 amri hiyo ya Kamanda wa polisi Thobias Sedoyeka kwani kikatiba ni 
halali kufanya maandamano bila kuvunja sheria za nchi, kwani kazi ya 
polisi ni kuwalinda wakati wakiandamana.
Mwenyekiti
 wa (Chama cha CHADEMA) Mkoa wa Singida, Shaban Limu akizungumza na 
waandishi wa habari Mkoani Singida juu ya hatua yao ya kupinga amri ya 
Kamanda wa polisi Mkoani humo Thobias Sedoyeka ya kuzuia maandamano yao 
kupinga ushindi wa Dkt. John Magufuli .
Ofisi za CHADEMA Mkoa wa Singida (PICHA ZOTE NA HILLARY SHOO).
Mo Blog 
0 comments:
Post a Comment