Naibu
 Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akiongozana na Mbunge wa Jimbo 
la Nzega Vijijini, Hamis Kigwangala (kulia) mara baada ya kuwasili 
kwenye Chuo cha Madini Dodoma, Kampasi ya Nzega ili kujionea hali ya 
eneo hilo.
 Naibu
 Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia) akikagua mazingira ya Chuo cha 
Madini Dodoma, Kampasi ya Nzega ili kujionea hali ya Kampasi hiyo.
 Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Isanga, Kata ya Lusu Wilaya ya Nzega (hawapo pichani).
 Naibu
 Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akiongozana na mwenyeji wake 
Mbunge wa Nzega Vijijini na Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii, 
Dkt. Hamis Kigwangala (kulia) walipofanya ziara kwenye Chuo cha Madini 
Dodoma, Kampasi ya Nzega ili kujionesa hali ya Kampasi hiyo.
 Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa pili kushoto) akikagua mazingira ya Chuo cha Madini Dodoma, Kampasi ya Nzega. 
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (katikati) alipotembelea Chuo Cha Madini Dodoma, kampasi ya Nzega
Serikali
 imetoa onyo kali kwa waliojinufaisha na kutumia ruzuku ya uchimbaji 
madini kinyume na makusudio yake ambao hadi sasa hawajarejesha licha ya 
kutakiwa kufanya hivyo.
Naibu
 Waziri wa Madini, Doto Biteko alitoa onyo hilo Februari 26, 2018 kwenye
 mkutano na wananchi na wachimbaji wadogo wa madini katika kijiji cha 
Isanga, Kata ya Lusu Wilaya ya Nzega. 
Awali
 kabla ya kutoa onyo hilo, wachimbaji hao waliiomba Serikali kuwapatia 
ruzuku ili iwasaidie katika shughuli zao za uchimbaji madini ndipo Naibu
 Waziri Biteko alipoweka bayana suala hilo la ruzuku.
Alisema
 Serikali ilisimamisha utoaji wa ruzuku kwa wachimbaji wadogo wa madini 
nchini baada ya kubaini kwamba imeshindwa kuleta mafanikio 
yaliyokusudiwa na kwamba ilikwishaagiza wale wote waliojipatia ruzuku na
 kuitumia kinyume na makusudio wanapaswa kuirejesha mara moja vinginevyo
 hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
“Wapo
 ambao tayari wameanza kurejesha na wengine bado hawajafanya hivyo. 
Ninawahakikishia wale ambao bado, tutawachukulia hatua kali za 
kisheria,” alisema Biteko.
Alisema haiwezekani watu wachache wasiokuwa na huruma kwa wanyonge wakatumia fedha ya Watanzania kinyume na makusudio yake.
Biteko
 alisema kuwa lengo la Serikali la utoaji wa ruzuku lilikuwa ni 
kuhakikisha wachimbaji wadogo wa madini nchini wanaweza kuendeleza 
machimbo yao kwa kufanya shughuli zenye tija kwao na Taifa kwa ujumla 
hata hivyo, makusudio hayo hayakufikiwa kama ilivyotarajiwa.
Alibainisha
 kuwa Serikali inakuja na mpango mwingine wa kuwasaidia wachimbaji 
wadogo kupata manufaa kutokana na shughuli zao lakini sio kuwapatia 
fedha kama ilivyokuwa hapo awali. “Tunanunua vifaa vya uchimbaji ambavyo
 vitatumika kuwasaidia na sio kuwapatia fedha,” alisema Biteko.
Aidha,
 Biteko aliwataka wachimbaji kote nchini kujiunga kwenye vikundi ili 
kujipatia manufaa mbalimbali ikiwemo urahisi wa kupata huduma za 
kifedha, kukopesheka na kuelimishwa njia bora na sahihi ya uchimbaji.
Alisema
 wachimbaji watakapojiunga wataweza kuwa na uchimbaji wenye tija na 
hivyo kutoa ajira nyingi kwa Watanzania wenzao, kulipa ushuru na tozo 
mbalimbali za Serikali na hivyo kujiletea maendeleo wao binafsi lakini 
pia maendeleo kwa Taifa kwa ujumla.
Katika
 ziara hiyo, Naibu Waziri Biteko aliambatana na mwenyeji wake Mbunge wa 
Jimbo la Nzega Vijijini na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis 
Kigwangala ambapo walitembelea maeneo ya Chuo cha Dodoma Kampasi ya 
Nzega (MRI) ambapo zamani palikuwa ni mgodi wa Reolute.






0 comments:
Post a Comment