Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Ni marobota ya tumbaku yaliyohifadhiwa kwenye moja ya ghala la 
chama cha Msingi Mitundu,tarafa ya Itigi,wilayani Manyoni wakati wa 
uzinduzi wa soko la tumbaku lililofanyika hivi karibuni katika Kijiji 
cha Mitundu.
baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Itigi,wilayani manyoni 
Mkoani Singida wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa Kijiji cha 
Songambele,wakati wa mkutano maalumu wa baraza la madiwani.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi,wilayani Manyoni,Mkoani 
Singida,Ally Minja(wa pili kutoka kushoto) akiongoza mkutano maalumu wa 
baraza la madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya 
Kijiji cha Songambele.
 Mbunge wa jimbp la Manyoni magharibi,Yahaya 
Masare akichangia baadhi ya hoja kwa kutoa ufafanuzi kwa wajumbe wenzake
 wa mkutano huo.
 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Manyoni,Jumanne Ismaili 
akiwasilisha salamu za chama kwa madiwani na watendaji wa Halmashauri ya
 Itigi,kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Kijiji cha 
Songambele,tarafa ya Itigi,wilayani Manyoni.(Picha zote Na Jumbe 
Ismailly)
 
WAKULIMA
 wa zao la tumbaku katika Halmashauri ya Itigi,wilayani Manyoni,Mkoani 
Singida hawana soko la uhakika la kuuzia zao hilo kutokana na Makampuni 
yaliyokuwa yakinunua zao hilo kushindwa kuendelea kwa sababu ya madeni 
makubwa yanayovikabili vyama vya msingi vinavyolima tumbaku katika 
Halmashauri hiyo.
Afisa
 Maendeleo ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri 
hiyo,Renatusi Mtatina aliyasema hayo kwenye mkutano maalumu wa Barazaa 
la Madiwani wa Halmashauri hiyo wakati akijibu swali la diwani wa kata 
ya Rungwa,Charles Machapaa ambaye alitaka kufahamishwa shilingi milioni 
477 zitapatikanaji kwenye zao la tumbaku wakati serikali imeshusha 
ushuru wa mazao kutoka asilimia 5 hadi 3.
Aidha
 Mtatina alithibitisha kwamba ni ukweli usiopingika kwamba Halmashauri 
ya Itigi kwa mwaka huu bado haaijapata mnunuzi wa tumbaaku wala kampuni 
yeyote ile itakayonunua zao hilo na badala yake wakulima wataendelea 
kulima zao hilo na kwenda kuuza sehemu nyingine.
“Nia
 tunataraji kwamba watakuwepo wakulima ambao watalima lakini wanaweza 
wakauza sehemu nyingine lakini kwa Halmashauri ya Itigi hatujapata 
mnunuzi kwa hiyo patakuwa na changamoto kubwa katika kilimo cha 
tumbaku.”alisisitiza afisa huyo wa kilimo,umwagiliaji na ushirika.
Kwa
 mujibu wa Mtatina suala la matatizo ya vyama vya ushirika bado 
halijatatuliwa kwa sababu bado wana madeni makaubwa na ndiyo maana 
hawajapata mnunuzi wa zao hilo la tumbaku.
Katika
 swali lake la msingi,diwani wa kata ya Rungwa,Charles Machapaa 
alionyesha hofu ya kutofikiwa kwa malengo ya makusanyo ya mapato ya 
Halmashauri hiyo ya shilingi milioni 477 kutokana na serikali kushusha 
ushuru wa aina mbali mbali ya mazao,ikiwepo tumbaku,ushuru wa pamba 
pamoja na ushuru wa mazao mengineyo. 
Kwa
 upande wake Mweka hazina wa Halmashauri hiyo,Charles Mnamba akitetea 
hoja hiyo alisisitiza kwamba katika msimu ujao uzalishaji wa kilimo cha 
zao la tumbaku utaongezeka zaidi ikilinganishwa na wa mwaka uliopita na 
utaweza kufidia kiwango cha ushuru wa asilimia mbili kilichopunguzwa na 
serikali.
0 comments:
Post a Comment