Aidha afisa elimu huyo alifa
 Ni
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Moses Matonya(wa kwanza 
kutoka kushoto) akiwa na Makamu Mwenyekiti,Jumanne Mlagaza wakiongoza 
mkutano wa baraza la Madiwani uliofanyika mjini Manyoni.
Na,Jumbe Ismailly MANYONI 
HALMASHAURI
 ya wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida inakabiliwa na changamoto mbali 
mbali katika sekta ya elimu ikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa huku 
kukiwepo ongezeko la uandikishaji la asilimia 67 na hivyo kuchangia 
kuwepo kwa  msongamano wa wanafunzi madarasani.
Afisa
 elimu msingi wilaya ya Manyoni,Salumu Ikambi alisema kiasi hicho cha 
asilimia 67 za uandikishaji ni kikubwa kutokana na idadi ya wanafunzi  walioandikishwa kufikia 7,176 kati ya lengo la kuandikisha jumla ya wanafunzi 11,000.
Aidha
 afisa elimu huyo alifafanua kwamba wanafunzi hao 7,176 wakiwemo 
wavulana 3,734 na wasichana 3,442 ni wengi ikilinganishwa na wanafunzi 
2,967 waliohitimu elimu ya msingi mwaka jana.
“Mwaka
 jana waliomaliza elimu ya msingi walikuwa 2,967 kwa idadi hiyo utaona 
karibu mara tatu ya wale ambao wameandikishwa mwaka huu.”alibainisha 
Ikambi.
Kwa
 mujibu wa Ikambi alizitaja baadhi ya changamoto wanazokaniliana nazo 
kuwa ni idadi ya vyumba vya madarasa vilivyokuwepo mwaka jana ndivyo 
hivyo hivyo vilivyo mwaka huu na idadi ya wanafunzi waliomaliza elimu ya
 msingi 60 lakini walioandikishwa ni 200.
Hata
 hivyo alisisitza pia kwamba pamoja na upungufu wa vyumba vya madarasa 
lakini kuna maeneo mengine pia bado yanakabiliwa na upungufu wa walimu 
na kutoa mfano kuwa darasa lenye wanafunzi 200 haliwezi kufundishwa na 
mwalimu mmoja.
Kwa
 upande wake afisa elimu sekondari Halmashauri ya wilaya ya 
Manyoni,Ramlah Munisi alibainisha kwamba mpaka sasa ni asilimia 14 ya 
wanafunzi 2,018 bado hawajaripoti shule kuanza masomo yao ya kidato cha 
kwamba kutokana na sababu mbali mbali ikiwepo kubadili vituo kutokana na
 umbali wa kutoka wanapoishi hadi shule walizopangiwa.
Afisa
 elimu huyo hata hivyo aliweka bayana kuwa kwa mwaka 2018 Halmashauri ya
 wilaya ya Manyoni ilipokea wanafunzi 2027 waliojiunga na masomo ya 
kidato cha kwanza na kati yao,wanafunzi 9 wamepangwa katika shsule za 
vipaji maalumu.
Kwa
 mujibu wa Munisi mwenye dhamana ya kusimamaia elimu sekondari,wanafunzi
 2,018 wamepangiwa shule za kata,ambapo kati yao 1,970 sawa na asilimia 
82.5 wamesharipoti shuleni na asilimia 2.8 wameenda katika shule za watu
 binafsi.
Akifunga
 mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani,Mwenyekiti wa Halmashauri ya 
wilaya ya Manyoni,Moses Matonya aliwakumbusha madiwani wajibu wao wa 
kwenda kusimamia mahudhurio ya wanafunzi wa shule za msingi pamoja na 
sekondari.
0 comments:
Post a Comment