Home » » MANYONI INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA

MANYONI INAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Aidha afisa elimu huyo alifa
 Ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Moses Matonya(wa kwanza kutoka kushoto) akiwa na Makamu Mwenyekiti,Jumanne Mlagaza wakiongoza mkutano wa baraza la Madiwani uliofanyika mjini Manyoni.
Na,Jumbe Ismailly MANYONI
HALMASHAURI ya wilaya ya Manyoni,Mkoani Singida inakabiliwa na changamoto mbali mbali katika sekta ya elimu ikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa huku kukiwepo ongezeko la uandikishaji la asilimia 67 na hivyo kuchangia kuwepo kwa  msongamano wa wanafunzi madarasani.
Afisa elimu msingi wilaya ya Manyoni,Salumu Ikambi alisema kiasi hicho cha asilimia 67 za uandikishaji ni kikubwa kutokana na idadi ya wanafunzi  walioandikishwa kufikia 7,176 kati ya lengo la kuandikisha jumla ya wanafunzi 11,000.
Aidha afisa elimu huyo alifafanua kwamba wanafunzi hao 7,176 wakiwemo wavulana 3,734 na wasichana 3,442 ni wengi ikilinganishwa na wanafunzi 2,967 waliohitimu elimu ya msingi mwaka jana.
“Mwaka jana waliomaliza elimu ya msingi walikuwa 2,967 kwa idadi hiyo utaona karibu mara tatu ya wale ambao wameandikishwa mwaka huu.”alibainisha Ikambi.
Kwa mujibu wa Ikambi alizitaja baadhi ya changamoto wanazokaniliana nazo kuwa ni idadi ya vyumba vya madarasa vilivyokuwepo mwaka jana ndivyo hivyo hivyo vilivyo mwaka huu na idadi ya wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi 60 lakini walioandikishwa ni 200.
Hata hivyo alisisitza pia kwamba pamoja na upungufu wa vyumba vya madarasa lakini kuna maeneo mengine pia bado yanakabiliwa na upungufu wa walimu na kutoa mfano kuwa darasa lenye wanafunzi 200 haliwezi kufundishwa na mwalimu mmoja.
Kwa upande wake afisa elimu sekondari Halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Ramlah Munisi alibainisha kwamba mpaka sasa ni asilimia 14 ya wanafunzi 2,018 bado hawajaripoti shule kuanza masomo yao ya kidato cha kwamba kutokana na sababu mbali mbali ikiwepo kubadili vituo kutokana na umbali wa kutoka wanapoishi hadi shule walizopangiwa.
Afisa elimu huyo hata hivyo aliweka bayana kuwa kwa mwaka 2018 Halmashauri ya wilaya ya Manyoni ilipokea wanafunzi 2027 waliojiunga na masomo ya kidato cha kwanza na kati yao,wanafunzi 9 wamepangwa katika shsule za vipaji maalumu.
Kwa mujibu wa Munisi mwenye dhamana ya kusimamaia elimu sekondari,wanafunzi 2,018 wamepangiwa shule za kata,ambapo kati yao 1,970 sawa na asilimia 82.5 wamesharipoti shuleni na asilimia 2.8 wameenda katika shule za watu binafsi.
Akifunga mkutano wa kawaida wa Baraza la Madiwani,Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Moses Matonya aliwakumbusha madiwani wajibu wao wa kwenda kusimamia mahudhurio ya wanafunzi wa shule za msingi pamoja na sekondari.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa