Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akishiriki zoezi la kutengeneza chaki katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Miraji Jumanne Mtaturu akiwa amebeba ili kuzianika chaki alizotengeneza Mkoa Singida Dkt Rehema Nchimbi katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akikagua kiwanda cha kutengeneza jasi cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Wafanyakazi wa kiwanda cha Dober Color wakifungasha chaki, Meneja wa Kiwanda hicho amesema sehemu ya kufungasha chaki hiyo inafanywa na wanawake kwakuwa wako makini na haraka.
Mkuu
 wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amepiga marufuku Shule zote 
Mkoani Singida kuagiza chaki nje ya Mkoa kwakuwa kuna viwanda 
vinavyozalisha chaki bora mkoani hapa.
Dkt
 Nchimbi ametoa katazo hilo mara baara ya kufanya ziara katika viwanda 
viwili vinavyozalisha chaki katika halmashauri ya Itigi na kushuhudia 
chaki yenye ubora ikiwa imezalishwa kwa wingi na  ikiwa haijapata soko.
“Hawa
 wenye viwanda wamejitahidi kuzalisha chaki bora haina vumbi na inauzwa 
kwa bei sahihi lakini shule zetu badala ya kuja kununua hapa ambapo ni 
karibu wanaagiza Dar es salaam na mikoa mingine”, amesema na kuongeza 
kuwa,
“Yani
 mnasubiri chaki hii hii iende Dar es Salaam halafu mnainunulia kutoka 
huko, hii haikubaliki, kuanzia leo shule zote zinunue chaki hapa hapa 
ili tupunguze gharama pamoja na kuinua viwanda vyetu”.Dkt
 Nchimbi ameongeza kuwa Mikoa ya Jirani itakayonunua chaki katika 
Viwanda vya Singida, vitasafirishiwa chaki hiyo bure kama motisha kwa 
kuunga mkono viwanda hivyo.
Amezitaka
 halmashauri kushirikiana katika kuboresha mazingira ya utendaji wa 
viwanda hivyo hasa kwa kuangalia namna ya kuboresha barabara zinazoenda 
katika machimbo ya jasi yanayotumika kutengeneza chaki kwakuwa wenye 
viwanda wamekuwa wakilalamikia ubovu wa barabara hizo.
0 comments:
Post a Comment