Home » » Ofisi ya mtendaji Kondoa yafungwa

Ofisi ya mtendaji Kondoa yafungwa

OFISI ya mtendaji wa kijiji cha Salanka, kata ya Salanka, wilayani Kondoa, imefungwa kwa kukosa mtendaji wa kijiji kwa muda wa mwaka moja sasa.
Hali hiyo imeelezwa kuchangia wananchi kukosa huduma hivyo na kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo kwenye ofisi ya kata.
Mtendaji wa kijiji hicho alisimamishwa na mkutano wa kijiji kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za kijiji.
Akizungumza kwenye mkutano wa kijiji, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Khamis Majaliwa, alisema wamekuwa wakifuatilia suala hilo kwa muda sasa huku Ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Ndani wa halmashauri hiyo akifika mara moja na hadi sasa hajafika kijijini hapo kwa madai ya kukosa usafiri.
Katika mkutano huo, wanakijiji hao waliazimia kwenda kuonana na Waziri Mkuu kutatua tatizo hilo lililodumu kwa muda wa mwaka sasa licha ya viongozi mbalimbali kuulizwa na kukosa majibu.
Alipoulizwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Omar Kwang’, alisema kwa wakati huo alikuwa yuko nje ya ofisi akiwa likizo na kumtaka mwandishi kusuburi hadi atakaporudi ofisini ndipo atatoa majibu.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa