OFISI ya mtendaji wa kijiji cha Salanka, kata ya Salanka, wilayani 
Kondoa, imefungwa kwa kukosa mtendaji wa kijiji kwa muda wa mwaka moja 
sasa.
  Hali hiyo imeelezwa kuchangia wananchi kukosa huduma hivyo na 
kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo kwenye ofisi ya 
kata.
  Mtendaji wa kijiji hicho alisimamishwa na mkutano wa kijiji kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za kijiji.
  Akizungumza kwenye mkutano wa kijiji, Mwenyekiti wa kijiji hicho, 
Khamis Majaliwa, alisema wamekuwa wakifuatilia suala hilo kwa muda sasa 
huku Ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Ndani wa halmashauri hiyo akifika 
mara moja na hadi sasa hajafika kijijini hapo kwa madai ya kukosa 
usafiri.
  Katika mkutano huo, wanakijiji hao waliazimia kwenda kuonana na Waziri
 Mkuu kutatua tatizo hilo lililodumu kwa muda wa mwaka sasa licha ya 
viongozi mbalimbali kuulizwa na kukosa majibu.
  Alipoulizwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Omar Kwang’, alisema kwa wakati huo 
alikuwa yuko nje ya ofisi akiwa likizo na kumtaka mwandishi kusuburi 
hadi atakaporudi ofisini ndipo atatoa majibu.
Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment