Home » » Ikungi kutumia bil. 25/-

Ikungi kutumia bil. 25/-

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, inatarajia kutumia shilingi bilioni 25.696 katika mwaka wa fedha 2014/2015 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shughuli za maendeleo.
Akisoma taarifa ya bajeti kwenye kikao maalumu cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo jana, Makamu Mwenyekiti Ally Nkangaa, alisema katika kipindi hicho kiasi cha sh bilioni 15.426 ni kwa ajili ya mishahara ya watumishi wake.
Hata hivyo alisema katika bajeti iliyopita halmashauri iliomba kuidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 16.953 ambapo hadi kufikia mwezi Desemba mwaka huu, jumla ya shilingi milioni 512.322 zilikuwa zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo.
Nkhangaa alisema katika utekelezaji wa bajeti, zipo changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na baadhi ya vijiji na kata kutochangia nguvu kazi na fedha.
Chanzo;Tanzania Dama

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa