HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi  mkoani Singida, inatarajia kutumia 
shilingi bilioni 25.696 katika mwaka wa  fedha 2014/2015 kwa ajili ya 
matumizi ya kawaida na shughuli za maendeleo.
  Akisoma taarifa ya bajeti kwenye  kikao maalumu cha Baraza la Madiwani
 wa halmashauri hiyo jana, Makamu  Mwenyekiti Ally Nkangaa, alisema 
katika kipindi hicho kiasi cha sh bilioni  15.426 ni kwa ajili ya 
mishahara ya watumishi wake.
  Hata hivyo alisema katika bajeti  iliyopita halmashauri iliomba 
kuidhinisha kiasi cha shilingi bilioni 16.953  ambapo hadi kufikia mwezi
 Desemba mwaka huu, jumla ya shilingi milioni 512.322  zilikuwa 
zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo.
  Nkhangaa alisema katika utekelezaji  wa bajeti, zipo changamoto 
mbalimbali ambazo ni pamoja na baadhi ya vijiji na  kata kutochangia 
nguvu kazi na fedha.
Chanzo;Tanzania Dama 
0 comments:
Post a Comment