Home » » HALIMASHAURI YA MKALAMA SINGIDA YAPANGA KUKUSANYA BIL 19

HALIMASHAURI YA MKALAMA SINGIDA YAPANGA KUKUSANYA BIL 19

HALMASHAURI ya wilaya ya Mkalama mkoani Singida, inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi bilioni  19  kutoka  kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato katika mwaka  ujao wa fedha wa 2014/2015.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Hassan Mwachabuzi amebainisha hayo  katika taarifa yake  ya  mapendekezo ya mpango wa  bajeti kwa mwaka ujao wa fedha  kwenye kikao maalum cha  baraza la madiwani.

Amesema wanatarajia kukusanya zaidi ya shilingi milioni 600 kutoka vyanzo vyake vya ndani ya mapato, wakati Serikali kuu itawapatia ruzuku ya shilingi milioni  360 kufidia vyanzo vya mapato vilivyofutwa.

Amefafanua kuwa  Serikali kuu pia  itatoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni  11.8  kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa halmashauri hiyo  na  ruzuku nyingine ya zaidi ya shilingi bilioni 1.9 kwa matumizi yasiyo ya mishahara.

Mwachabuzi amesema Serikali kuu,  wafadhili, wahisani na wananchi, watachangia mapato ya zaidi ya shilingi  bilioni 4.6 bilioni, kwa ajili ya kugharamia miradi  mbalimbali ya maendeleo  katika  jamii.

Hata  hivyo pamoja na madiwani kupitisha mapendekezo  hayo ya bajeti, wamewataka watendaji kuimarisha  zaidi ukusanya mapato ya ndani na kubuni nyanzo  vingine  badala ya kutegemea zaidi Serikali kuu na wafadhili.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa