HALMASHAURI ya wilaya ya Mkalama mkoani
Singida, inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi bilioni  19  kutoka
 kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato katika mwaka  ujao wa
fedha wa 2014/2015.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Hassan
Mwachabuzi amebainisha hayo  katika taarifa yake  ya 
mapendekezo ya mpango wa  bajeti kwa mwaka ujao wa fedha  kwenye
kikao maalum cha  baraza la madiwani.
Amesema wanatarajia kukusanya zaidi ya
shilingi milioni 600 kutoka vyanzo vyake vya ndani ya mapato, wakati Serikali
kuu itawapatia ruzuku ya shilingi milioni  360 kufidia vyanzo vya mapato
vilivyofutwa.
Amefafanua kuwa  Serikali kuu
pia  itatoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni  11.8  kwa ajili
ya mishahara ya watumishi wa halmashauri hiyo  na  ruzuku nyingine ya
zaidi ya shilingi bilioni 1.9 kwa matumizi yasiyo ya mishahara.
Mwachabuzi amesema Serikali kuu,
 wafadhili, wahisani na wananchi, watachangia mapato ya zaidi ya shilingi
 bilioni 4.6 bilioni, kwa ajili ya kugharamia miradi  mbalimbali ya
maendeleo  katika  jamii.
Hata  hivyo pamoja na madiwani
kupitisha mapendekezo  hayo ya bajeti, wamewataka watendaji
kuimarisha  zaidi ukusanya mapato ya ndani na kubuni nyanzo 
vingine  badala ya kutegemea zaidi Serikali kuu na wafadhili.
0 comments:
Post a Comment