Home » » Miradi miwili ya maji Wilaya ya Mkalama kutumia Sh799 mil

Miradi miwili ya maji Wilaya ya Mkalama kutumia Sh799 mil

Mkalama. Wilaya ya Mkalama mkoani Singida, inatarajia kutumia zaidi ya Sh799.4 milioni kwa ajili ya miradi ya maji katika Vijiji vya Ng’ang’uli na Iguguno vilivyopo kwenye mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).
Mradi wa Kijiji cha Ng’ang’uli, unatarajiwa kukamilika Januari mwakani, wakati ule wa Kijiji cha Iguguno utamalizika Aprili mwakani.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Edward Ole Lenga wakati akizungumzia utekelezaji wa miradi hiyo.
Alisema miradi hiyo ambayo itanufaisha wakazi 4,379 wa vijiji hivyo, ambapo mradi wa Ng’ang’uli ulianza Agosti mwaka jana na ule wa Kijiji cha Iguguno ulianza Septemba mwaka jana. “Hadi kufikia Novemba mwaka jana, utekelezaji wa mradi wa Ng’ang’uli ulikuwa umefikia aslimia 80 na ule wa Iguguno asilimia 30,” alisema Ole Lenga.
Aidha, alisema utaratibu wa kutumia mtaalamu mkandarasi wa nje umekuwa na matatizo mengi ya kiutawala ndani ya kampuni kiasi cha kusababisha baadhi ya miradi kuchelewa kukamilika.
“Utaratibu wa kutumia wataalamu washauri wa ndani, unaonekana kubadilisha sura ya utendaji kazi wa makandarasi. Ni muhimu kwamba usimamizi wa miradi ijayo utafanyika kwa utaratibu huu wa ndani,” alifafanua.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa