Home » » KESI ZA RUSHWA ZAONGEZEKA SINGIDA

KESI ZA RUSHWA ZAONGEZEKA SINGIDA

TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoani Singida, imepokea taarifa 102 za malalamiko dhidi ya  vitendo vya kuomba na kupokea rushwa katika  kipindi cha  kuanzia Januari  hadi Disemba mwaka Jana.

Mkuu wa taasisi hiyo mkoani Singida Joshua Msuya amesema hayo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, juu ya utekelezaji wa majukumu yake kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi disemba mwaka Jana.

Amesema kati ya taarifa hizo, 87 ziko kwenye uchunguzi wa hatua mbali mbali, taarifa 13 zilitolewa ushauri kwa walalamikaji na taarifa mbili, zimehamishiwa katika idara nyingine kwa hatua zaidi.

Akifafanua zaidi, mkuu huyo,amesema  kuwa taarifa hizo za mwaka jana, ni sawa na ongezeko la asilimia 11.7 ikilinganisha na taarifa 94 za mwaka juzi zilizofikishwa katika taasisi hiyo kuzuia rushwa.
Msuya amesema ongezeko hilo linatokana na jitihada zilizofanywa na TAKUKURU mkoa za kutoa  elimu kwa wananchi na makundi mengine ya kijamii ili kuwajengea ujasiri wa kufichua vitendo vya rushwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa