Home »
 » BASI LA SHABIBY LAPATA AJALI,28 WAJERUHIWA
 
BASI LA SHABIBY LAPATA AJALI,28 WAJERUHIWA
        
            
 
       
        
        
        
        
            
 ABIRIA 28 wakiwemo 
watoto wanne, wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Shabiby namba T 
930 BUW, aina ya Utom, walilokuwa wakisafiria kugongana na lori la 
mafuta na kupinduka katika Kijiji cha Kisaki. 
Ajali hiyo imetokea 
jana mchana umbali wakilomita 10 kutoka mkoani Singida kwenda Dodoma 
wakati dereva wa basi hilo akijaribu kulipita lori upande wa kulia .
Lori
 hilo lenye namba RAA 486N, aina ya Mercedes Benz, lilikuwa likitokea 
Kigali, nchini Rwanda, kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Barimina 
Benjamin (37).
Inadaiwa basi hilo lilikuwa na abiria 48 ambapo dereva
 wake alikimbia baada ya ajali. Baadhi ya majeruhi waliozungumza na 
Majira, walisema majeruhi wa ajali hiyo ni pamoja na kondakta Thadey 
Mohando (34) . 
Kondakta huyo anadaiwa kuvunjika miguu yote miwili na
 mkaguzi wa basi William Hofini (39) alipata majeraha usoni na kwenye 
mkono wa kulia .
Abiria wengine ambao walijeruhiwa walik imbizwa 
Hospitali ya Mkoa huo kwa ajili ya matibabu ambapo Jeshi la Polisi 
Kikosi cha Usalama Barabarani kilifika eneo la tukio kwa uchunguzi 
zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa huo, Bi. 
Queen Mlozi, aliwataka madereva kuzingatia sheria za Usalama Barabarani 
ili kunusuru maisha ya watu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa , 
Dkt.Deogratius Banuba, alisema wamepokea majeruhi 28 wakiwemo watoto 
wanne lakini wawili wa melazwa akiwemo kondakta wa basi na Agatha 
Ally(20), mkazi wa Babati aliyeumia sehemu mbalimbali za mwili wake.
Chanzo:majira 
 
 
0 comments:
Post a Comment