Home » » BASI LA SHABIBY LAPATA AJALI,28 WAJERUHIWA

BASI LA SHABIBY LAPATA AJALI,28 WAJERUHIWA

 ABIRIA 28 wakiwemo watoto wanne, wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya Shabiby namba T 930 BUW, aina ya Utom, walilokuwa wakisafiria kugongana na lori la mafuta na kupinduka katika Kijiji cha Kisaki.
Ajali hiyo imetokea jana mchana umbali wakilomita 10 kutoka mkoani Singida kwenda Dodoma wakati dereva wa basi hilo akijaribu kulipita lori upande wa kulia .
Lori hilo lenye namba RAA 486N, aina ya Mercedes Benz, lilikuwa likitokea Kigali, nchini Rwanda, kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Barimina Benjamin (37).
Inadaiwa basi hilo lilikuwa na abiria 48 ambapo dereva wake alikimbia baada ya ajali. Baadhi ya majeruhi waliozungumza na Majira, walisema majeruhi wa ajali hiyo ni pamoja na kondakta Thadey Mohando (34) .
Kondakta huyo anadaiwa kuvunjika miguu yote miwili na mkaguzi wa basi William Hofini (39) alipata majeraha usoni na kwenye mkono wa kulia .
Abiria wengine ambao walijeruhiwa walik imbizwa Hospitali ya Mkoa huo kwa ajili ya matibabu ambapo Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani kilifika eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa huo, Bi. Queen Mlozi, aliwataka madereva kuzingatia sheria za Usalama Barabarani ili kunusuru maisha ya watu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa , Dkt.Deogratius Banuba, alisema wamepokea majeruhi 28 wakiwemo watoto wanne lakini wawili wa melazwa akiwemo kondakta wa basi na Agatha Ally(20), mkazi wa Babati aliyeumia sehemu mbalimbali za mwili wake.

Chanzo:majira

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa