HALMASHAURI  ya Manispaa ya Singida, inatarajia kutumia sh bilioni 31.7 katika bajeti yake  ya mwaka wa fedha wa 2014/2015.
  Kaimu  Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Deus Luziga, alibainsha hayo 
alipokuwa akitoa  mapendekezo ya bajeti ya mwaka ujao wa fedha mbele ya 
kikao maalumu cha bajeti  cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwenye 
ukumbi wa mikutano wa manispaa  hiyo.
  Alisema  kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 Halmashauri ya Manispaa ya 
Singida imeandaa  bajeti yake kwa kuzingatia mwongozo wa bajeti wa 
taifa, sera ya taifa ya  kuondoa umasikini.
  Alisema  kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 15.287 ni mishahara ya 
watumishi, ruzuku  ya serikali kuu kwa matumizi mengineyo sh bilioni 
1.860, sh bilioni 11.621 ni  ruzuku ya miradi ya maendeleo wakati sh 
bilioni 2.986 ni mapato ya ndani.
  Alisema  wanatarajia serikali kuu itawapatia ruzuku ya sh milioni 181 kwa ajili ya  kufidia ushuru na kodi iliyofutwa.
  Kaimu  mkurugenzi huyo alisema bajeti ya Manispaa ya Singida 
imeongezeka kwa sh  bilioni 13 ambayo ni sawa na aslimia 43 ya lengo la 
kukusanya zaidi ya sh  bilioni 18.1 katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 
2013/2014.
  “Ongezeko  hili limechangiwa pamoja na kuongezeka kwa ajira mpya na 
nyongeza za mishahara  na kuongezeka kwa miradi ya maji ambayo maelekezo
 yake ni kutekeleza miradi  katika vijiji 20,” alifafanua.
  Aidha, alisema katika bajeti ya mwaka wa fedha  2013/2014 halmashauri 
iliidhinishiwa kutumia sh bilioni 18.125 kwa ajili ya  kutoa huduma 
mbalimbali ikiwemo mishahara ya watumishi.
  Hata  hivyo, alisema mapato ya ndani yameongezeka kutoka sh bilioni 
1.928 mwaka  2013/2014 hadi kufikia sh bilioni 2.986 kwa mwaka 
2014/2015.
Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment