MKAZI wa 
Kijiji cha Mwasutianga, Kata ya Irisya, wilayani  Ikungi, Singida, 
Mwanahamisi Mwangu (72), amekufa baada ya kupigwa mateke na ngumi na 
mumewe, Salehe Mohammed (75) kutokana na ugomvi baina ya marehemu na mke
 mwenzie wakigombea ndoo ya maji.
Tukio hilo limetokea Januari mosi mwaka huu, saa 7 mchana wakati wakiwa shambani wakipanda mazao.
Kamanda wa 
Polisi wa Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alisema siku ya tukio 
Mwanahamisi alikuwa shambani na mumewe pamoja na mkewe mdogo, Fatuma 
Ramadhani (55). Walikuwa wakipanda mtama, lakini ghafla ulizuka ugomvi 
wa kugombea ndoo iliyokuwa na maji.
Alisema katika ugomvi huo kila mmoja akidai  ndoo hiyo ni mali yake, ndipo mume wao alipoamua kuingilia ugomvi huo.
“Mtuhumiwa mzee Salehe katika 
ugomvi huo alikuwa upande wa mke mdogo ndipo alianza kumpiga mateke na 
ngumi mkewe mkubwa Mwanahamisi na kusababisha kifo chake papo hapo,” 
alisema Kamwela.
Alisema polisi wanamshikilia mtuhumiwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani muda wowote baada ya upelelezi kukamilika.
Katika tukio jingine, Shauri 
Samwel (22) mkazi wa Kijiji cha Tyeme, wilayani Iramba, amefariki dunia 
baada ya kunywa vidonge vya kuhifadhia nafaka.
Alisema
 tukio hilo lilitokea Desemba 31 mwaka jana, saa 12 jioni katika 
zahanati ya Kijiji cha Tyeme wakati Shauri akiendelea kupatiwa matibabu.
Kamanda Kamwela alisema chanzo cha kunywa vidogo hivyo  ni hofu aliyokuwa nayo Shauri kutokana na kumtia ujauzito binamu yake.

0 comments:
Post a Comment