DIWANI wa Rungwa, Tarafa  ya Itigi, wilayani Manyoni, Singida, 
Edward Machapaa, amependekeza adhabu ya  kuchapwa viboko itolewe kwa 
watendaji wanaokula fedha za wananchi zilizotolewa  na serikali kwa 
ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo.
  Machapaa alitoa  pendekezo hilo kwenye mkutano maalumu wa Baraza la 
Madiwani wa halmashauri ya  wilaya hiyo uliofanyika mjini Manyoni 
alipokuwa akijadili hoja ya matumizi  mabaya ya fedha za miradi ya 
maendeleo.
  Alisema kumekuwepo  malalamiko mengi na ya mara kwa mara juu ya fedha 
za miradi kutumika vibaya au  hata kwa baadhi ya watendaji kula fedha 
hizo, hivyo umefika wakati wa kubadili  mbinu ya kutoa adhabu kwa kutoa 
adhabu ya viboko.
  “Ndugu mkurugenzi, kwa  hili hapa inatakiwa tutafute dawa, huyu mtu 
anayekula hela kama ni mtendaji  kwanini asichapwe bakora 12, ili 
akamuonyeshe mkewe?” alisisitiza Machapaa na  kusababisha madiwani 
wenzake pamoja na wakuu wa idara kuangua kicheko.
  Diwani huyo alitumia  fursa hiyo kuwashawishi madiwani wenzake 
kubadilika na kuonya kwamba endapo  hawatabadilika serikali itaendelea 
kutuma wakaguzi na adhabu ya kuwakata  mishahara itaendelea kuwepo mwaka
 hadi mwaka.
  Pia alipendekeza  watendaji hao wafukuzwe hata watatu kwa kuanzia na huenda wengine wakaogopa  baada kuona adhabu hiyo.
  Mkurugenzi mtendaji wa  halmashauri hiyo, Supeet Mseya, alisema katika
 kipindi cha mwaka 2013/2014  halmashauri hiyo ilipata mafanikio mengi 
na kuyataja baadhi kuwa ni kuendelea  kupata hati safi ya ukaguzi wa 
matumizi ya fedha na halmashauri kuendelea  kupata ruzuku ya CDG.
  Mafanikio mengine ni  kuboreshwa kwa huduma za afya kwa asilimia 95 
kwa kutoa kinga na tiba kwa ajili  ya magonjwa mbalimbali, uendelezaji 
wa ujenzi wa vituo vitatu vya afya katika  kata za Makuru, Mitundu na 
Itigi, ujenzi wa zahanati tatu katika vijiji vya  Ntope, Igwamadete 
Rungwa, na ukamilishaji wa hosteli nne katika shule za Itigi,  Makuru, 
Rungwa na Sanza.
 Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment