Meneja
 wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende akitoa nasaha zake muda mfupi 
kabla hajatoa mikopo yenye thamani ya shilingi 18.9 kwa wajasiriamali wa
 kikundi cha Urafiki cha mjini Singida.Kulia (aliyekaa) ni katibu wa 
kikundi cha urafiki,Remiji Alex.
Meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibenda,akimkabidhi Remji Alex mkopo wa shilingi 500,000.
Meneja
 mikopo wa SIDO mkoa wa Singida, Ruben Mwanja akitoa mafunzo kwa 
wajasiriamali muda mfupi kabla ya kukabidhi mikopo yenye thamani ya 
zaidi ya shilingi 18.9 milioni kwa kikundi cha urafiki cha mjini 
Singida.
Meneja
 mikopo wa SIDO mkoa wa Singida, Ruben Mwanja (wa kwanza kulia) akiwa 
kwenye picha ya pamoja na wanakikundi cha wajasiriamali cha Urafiki cha 
mjini Singida.Kikundi hicho kilikopeshwa zaidi ya shilingi 18.9 milioni 
na watarudisha na fidia ya shilingi 1.8 kwa mwezi.(Picha na Gasper 
Andrew).
Na Nathaniel Limu
MENEJA
 mikopo wa shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) mkoa wa 
Singida,Ruben Mwanja,amewataka wajasiriamali kutumia mikopo yao vizuri 
na kwa malengo yaliyokusudiwa,na pia mikopo hiyo isaidie kuimarisha ndoa
 zao.
Mwanja
 aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mikopo 
mbalimbali yenye thamani ya shilingi 18,9 milioni kwa wanachama 39 wa 
kikundi cha Urafiki cha Singida mjini.
Amesema
 uzoefu unaonyesha wazi kwamba baadhi ya wanawake wanaobahatika kupata 
mikopo,hukorofishanana au kutengana kabisa wanaume wao.
“Pia
 wapo baadhi ya wanaume wakishapata mkopo wa kuendeleza biashara 
yao,hukimbilia kuoa mke mwingine”,amesema Mwanja na kuongeza;
“Nawasihi
 sana,mikopo ya SIDO isitumike kuongeza wake wengine au kuvunja ndoa za 
watu,itumike tu kuendeleza biashara ya mkopaji ili kupanua/kuongeza 
kipato cha mhusika”.
Kwa
 upande wake meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibenda,alikipongeza 
kikundi cha Urafiki kwa madai kwamba kina utamaduni mzuri wa kurudisha 
mikopo kwa wakati na bila matatizo.
Kibenda
 aliwataka wapige hatua zaidi kwa kuangalia uwezekano wa kuanzisha 
viwanda vidogo kama njia moja wapo ya kujiongezea kipato zaidi.
Mikopo
 iliyotolewa juzi,kima cha chini kilikuwa shilingi 300,000 na cha 
juu,kilikuwa ni shilingi 500,000 kwa mwanachama mmoja mmoja.Riba ya 
mikopo hiyo ni asilimia 1.8 kwa mwezi.
0 comments:
Post a Comment