Home » » Watatu wafariki kwenye matukio tofauti

Watatu wafariki kwenye matukio tofauti

DSC001791
Kamanda wa Polisi Mkoani Singida,SACP Geofrey Kamwela.
Na Nathaniel Limu, Singida
WATU watatu mkoani Singida wamefariki dunia katika matukio tofauti likiwemo la mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mng’imba Wilaya ya Mkalama kusombwa na maji ya mto wa Ndurumo.
Kwa Mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoani Singida,SACP Geofrey Kamwela mwanafunzi huyo ni Mwajuma Jumanne mwenye umri wa miaka tisa.
Amesema mwanafunzi huyo amesombwa na maji ya mto wa Ndurumo januari 28 mwaka huu saa sita mchana wakati akivuka mto wa Ndurumo akitokea shuleni akielekea nyumbani kwao.
 “Mwili wa mwanafunzi huyo ulionekana kesho yake saa nane mchana kandokando ya mto Ndurumo katika eneo la kijiji cha Kidaru wilaya ya Iramba”,amesema Kamwela.
Katika tukio jingine,kamanda huyo alisema Ng’washi Gembuya (30) mkulima na mkazi wa kijiji cha Mkiko wilaya ya Mkalama,alisombwa na maji ya mto huo huo wa Ndurumo.
 “Uchunguzi wa awali wa jeshi la polisi,umebaini kuwa marehemu amefariki dunia kutokana na kusombwa na maji yam to Ndurumo tangu januari 23 mwaka huu saa 12.00 jioni wakati anajaribu kuvuka mto huo huku akiwa amelewa pombe ya kienyeji”,alifafanua.
Wakati huo huo,Kamwela amesema mtu ambaye hafahamiki anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30 wa jinsi ya kike,amefariki dunia kwa kuuawa na watu wasiofahamika.
“Mwanamke huyo alikutwa amefariki dunia na mwili wake ukiwa umechomwa moto na kisha kutupwa kwenye daraja la kijiji cha Matipa manispaa ya Singida.Polisi inaendelea na uchubguzi kujua sababu ya mauaji na watu waliohusika”,amesema Kamanda Kamwela.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa