Home » » Wazazi sasa kukamatwa kwa kushindwa kuandikisha watoto shule za sekondari

Wazazi sasa kukamatwa kwa kushindwa kuandikisha watoto shule za sekondari

DSC06329
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida na mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM mikoa nchini,Mgana Msindai, akihutubia wananchi na wana CCM waliohudhuria maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe.
DSC06307
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida, Mgana Msindai, akimkabidhi kadi mwanachama mpya aliyejiunga na CCM kwenye maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe.Maadhimisho hayo halifanyika kimkoa katika kijiji cha Zigiligi wilayani Iramba.
DSC06265
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida, Mgana Msindai, akipanda mti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe.
DSC06291
Baadhi ya wana CCM ana wananchi wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,waliohudhuria maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Zigiligi tarafa ya Ndago wilaya ya Iramba mkoa wa Singida.(Picha na Nathaniel Limu). 
Na Nathaniel Limu, Iramba
MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Singida,Mgana Msindai amewaagiza wakuu wa Wilaya kuwakamata na  kuwafikisha mahakamani wazazi na walezi wote ambao watoto wao  hawajaripoti  katika shule za Sekondari walizopangiwa.
Masindai ametoa agizo hilo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye kilele cha sherehe za maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe.Sherehe hizo zilizofana,zilifanyikia  katika kijiji cha Zigiligi Wilayani Iramba.
Amesema kuwa zipo taarifa  kwamba baadhi  ya wazazi /walezi wanawazuia watoto wao kwenda shule  kutokana na sababu mbalimbali.
Akifafanua,amesema “Ndugu zetu wafugaji wamekuwa mstari wa mbele kuwazuia watoto wao kwenda shule, ili waweze kuchunga mifugo na wengine, kuwaoza  kwa nguvu watoto wao kike tena wenye umri mdogo” .
Akisisitiza zaidi, Msindai ambaye pia ni Mwenyekiti wa wenyeviti CCM nchini,amesema haki za msingi ambazo mtoto anapaswa kuzipata, ni pamoja na elimu.
“Kwa hiyo, wakuu wa Wilaya nawaomba sana,hakikisheni wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na Sekondari, wanajiunga katika shule walizopangiwa mapema iwezekanyo, hata kama hawana ada”,amesema mwenyekiti huyo..
Msindai amesema endapo mwanafunzi hajajiunga na shule aliyopangiwa,ameacha shule kwa sababu yo yote ili ikiwemo ya ukosefu wa  ada, wote wapelekwe/warudishwe shule na kuanza masomo.
Wakati huo huo,amesema  wazazi na walezi wao wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma ya kushindwa/kuwazuia watoto wao kupata haki yao ya msingi ya elimu.

Kwa hisani ya Mo Blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2011. Singida Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogz za Mikoa